Tunatumia ID fake hapa JF ili kuficha uhalisia wetu(ukiacha verified users),ila naamini hiyo ID unayoitumia haujaichagua kwa bahati mbaya lazma itakuwa na maana kubwa kwako.
Mfano mimi Chinga One nimejiita hivi kwa kuwa nimetokea Mtwara hata Avator yangu ni alama kubwa ya mkoa wa Mtwara ukifika viwanja vya Mashujaa utaikuta hiyo Sanamu,lakini pia nimejiita hilo jina kwa kuwa nilikuwa karibu sana na Straika hatari sana Mohamed Hussein Daima Mmachinga (Chinga One) enzi za utotoni.....Je wewe hiyo ID yako ina maana gani?
Nina tabia za kujitegemea kama paka, na napenda kufanya mambo yangu mengi usiku wakati kumetulia. Sipendi dhambi na napenda sana haki ndio kisa cha utakatifu wa Paka Mweusi.