Je, juhudi za kupambana kuzuia dawa asili za kulevya kama bangi na miraa zina matokeo yoyote?

Kutumia mijihela kibaaaao kwenda kuhangaika na majani ambayo yanajiotea tu huko kwenye mapori bila hata kupandwa nao ni ufisadi wa aina yake pia.
 
WE JAMAA INAONYESHA UNASTRESS NA MAISHA KAMA ID YAKO KWENYE PICHA YANI MJUAJI WA WAJINGA
 
Asante kwa somo,mimi ni mdogo tu nimezaliwa 1984. Nimeelewa somo lako na nina NGO inayohusiana na masuala haya haya,nilitaka kuoata tu uwiano wa juhudi za kupambana na upatinakani wake ki urahisi mtaani..upande wa elimu juu ya ubaya na madhara umefaulu kushusha matumizi japo sijaona imepunguza kushusha upatikanaji. Naomba elimu zaidi hapo kaka.
 
Yes kaka. Nimeongelea si kwa upana kwenye sehemu ya upatikanaji, ila nimekuonyesha kupitia, trafficking, of which zina work hand in hand. Ndio mzigo unapatkana ila kwa kiasi kidogo sana kulinganisha na nyuma.
Kama miaka hiyo ulikua duniani hopefully kufika mwaka elfu mbili, uliona mambo haya yalivyokua moto compared with past 5 years.
 
Data kamili, miaka 11 iliyopita (2012-2023)DCEA walikamata madawa ya kulevya takribani 606,000, lakini mwaka 2023 ulitia fora kwa kukamatwa, Kilo Gram 1,965,340.52, na imefanikiwa Kuzuia uingizaji wa Kg 157,738. Kwa mwaka mmoja, mwaka huu 2024, April zilikamatwa dawa kilo 700, ukipiga hesabu ukamataji , mapambano ni ya hli ya juu.
Refer moja ya comment yangu, nikasema drug arrests imeshuka, ila inabaki pronounced tu. Kwa miaka hii ya karibuni waliokamatwa hawazidi 15,000 . Hvo haya yote ni matokeo ya juhudi ya kupambana na dawa za kulevya, hiyo miraa na bangi, ambayo unakuta hiyo ndio inakamatwa kweli kweli
 
Hapo napata mwanga sasa, ilikuwa inaniletea mkanganyiko kwenye tafiti yangu,maana juhudi zikipungua pia,na takwimu za ukamataji lazima zitapungua,na pia upatikanaji na isambazaji utaongezeka,acha niendelee kupata maoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…