Je, Julian Assange ni Shujaa au Msaliti?

Je, Julian Assange ni Shujaa au Msaliti?

Inategemea ni jambo gani!
Tafuta basi hata interview aliyoifanya mke wake Leo kwenye Hard talk ya BBC,huenda ukaongeza maarifa kuliko hivyo ulivyo mtupu!
Hata Snowden raia wa Marekani wanamuona shujaa!
shida sio nan kumuona shujaa ila taratibu zinasema kutoa usiri wa mtu huo ni uhalifu , kama ana malalamiko mahakama zipo
 
Hapo kwenye mwanadada Chelsea Manning umekosea kidogo. Huyo alikuwa ni mwanaume mwanajeshi aliyezaliwa Kwa jina la Bradley Edward Manning. Jina la Chelsea Elizabeth Manning alilipata baada ya kubadili jinsia na kuwa mdada (gender reassignment), na hili amelifanya baada ya kuwekwa lupango kwa hilo kosa ulilotaja.
Nlichanganya lakini ungesoma mpaka mwisho kuna sehemu nimeeleza humo katikati wakati nazungumzia kuhusu kushitakiwa na kufungwa kwa chelsea
 
Kutoka kuniita Mtupu hadi kunikumbusha kuwa Jf ni sehemu ya kubadilishana mawazo🙁. sawa, ila mimi ndiye nilipaswa nikukumbushe la Jf kuwa sehemu ya kubadilishana mawazo ila sikufanya hivyo.
Mimi nilitaka kujua nini hasa kimekufanya ujisikie uko full maarifa baada ya kusikiliza hiyo interview.
Nimekwambia nimeongeza maarifa Kwa kuisikiliza hiyo interview!Mfano,nilikuwa sijui kuwa kumbe alipokuwa hifadhini ubalozi wa Ecuador,CIA walipenyeza microphones za Siri mpaka sehemu anakolala!So hata vikao vyake vya legal issues,walikuwa wanasikiliza hao hao wamarekani wanaotaka kumfungs miaka 175 baada ya kutoboa Siri zao za war crimes huko Afghanistan!
Kipindi kinarudiwa Sasa hivi BBC!
 
Back
Top Bottom