Je, kelele za Tozo za Benki zitazima mapema kama kelele za Tozo za miamala?

Je, kelele za Tozo za Benki zitazima mapema kama kelele za Tozo za miamala?

Chulumeshy

Member
Joined
Jul 27, 2022
Posts
17
Reaction score
11
Lawama na kelele zinazoendelea kuhusiana na uanzishwaji wa tozo za miamala na za kifedha sasa zimekuwa kama kelele za chura akiwa kwenye maji kwani hayamzuii tembo kuyanywa maji apatapo kiu.

Lawama na malalamiko mengi yameanza mwaka 2021 baada ya serikali kuanzishwa kwa tozo mbalimbali kwa lengo la kuinua uchumi wa Taifa kwa kasi jambo lililopelekea kupandishwa kwa tozo katika makampuni ya simu na hata taasisi za kifedha kama vile benki.

Lakini mwanzoni watumiaji wakubwa wa huduma hizi walilalamika kwa kuwa makato ni makubwa sana na kudai makato hayo yaweze kupunguzwa jambo ambalo limekuwa kama kelele zisizokuwa na faida kwani japokuwa kuna madai na malalamiko mengi kuhusiana na kupandishwa kwa kodi na tozo lakini bado watumiaji wengi wamezidi kutumia huduma hizo huku takwimu zikioneshwa kwamba matumizi hayo yanazidi kupanda kama BoT

1661335556751.png


Na hat idadi ya mawakala imeongezeka jambo linaloonesha kuwa watumiaji wanazidi kutumia kwa kasi na wamekubaliana na tozo hizo.
1661335657575.png

Hata hivyo, hivi karibuni tozo za miamala ya kibenki nayo imeanzishwa huku watu wengi wakilalamikia madai hayo na wakati huo huo takwimu zilizotolewa na BoT zinaonesha kuwa watumiaji wa miamala ya kibenki ni wachache kuliko watumiaji wa miamala ya Makampuni ya simu.
1661335717132.png

Swali linabaki Je, kelele hizi zitakuwa ni za bure kama za tozo za miamala ya simu au zitafanyiwa kazi na watumiaji kwa ujumla na wakati bado watu wanatumia kwa kasi huku takwimu zinaonesha kuwa kila siku inazidi tu kupanda?
 
Ili kupinga hili kunaitishwa na waungwana: "kila mtu atokee nyumbani kwake kivyake vyake apinge kwa nguvu zake." Kwamba litaondoka.

Hiyo ndiyo Tanzania ya wajinga kwenye ubora wake.

Cc: mwanawao, Kalunya, antimatter
 
Wabongo kazi kupiga domo tu, je mmefanya action zozote kupinga tozo? Zaidi kupiga domo tu
 
Ya bank yameshapoa sasa tupo kwenye Ving'amuzi. Baada ya ving'amuzi tunaingia kwenye matumizi ya TIN kuanzia umri wa miaka 18
 
Lawama na kelele zinazoendelea kuhusiana na uanzishwaji wa tozo za miamala na za kifedha sasa zimekuwa kama kelele za chura akiwa kwenye maji kwani hayamzuii tembo kuyanywa maji apatapo kiu.

Lawama na malalamiko mengi yameanza mwaka 2021 baada ya serikali kuanzishwa kwa tozo mbalimbali kwa lengo la kuinua uchumi wa Taifa kwa kasi jambo lililopelekea kupandishwa kwa tozo katika makampuni ya simu na hata taasisi za kifedha kama vile benki.

Lakini mwanzoni watumiaji wakubwa wa huduma hizi walilalamika kwa kuwa makato ni makubwa sana na kudai makato hayo yaweze kupunguzwa jambo ambalo limekuwa kama kelele zisizokuwa na faida kwani japokuwa kuna madai na malalamiko mengi kuhusiana na kupandishwa kwa kodi na tozo lakini bado watumiaji wengi wamezidi kutumia huduma hizo huku takwimu zikioneshwa kwamba matumizi hayo yanazidi kupanda kama BoT

View attachment 2333398

Na hat idadi ya mawakala imeongezeka jambo linaloonesha kuwa watumiaji wanazidi kutumia kwa kasi na wamekubaliana na tozo hizo.
View attachment 2333401
Hata hivyo, hivi karibuni tozo za miamala ya kibenki nayo imeanzishwa huku watu wengi wakilalamikia madai hayo na wakati huo huo takwimu zilizotolewa na BoT zinaonesha kuwa watumiaji wa miamala ya kibenki ni wachache kuliko watumiaji wa miamala ya Makampuni ya simu.
View attachment 2333405
Swali linabaki Je, kelele hizi zitakuwa ni za bure kama za tozo za miamala ya simu au zitafanyiwa kazi na watumiaji kwa ujumla na wakati bado watu wanatumia kwa kasi huku takwimu zinaonesha kuwa kila siku inazidi tu kupanda?
Ili kupinga hili kunaitishwa na waungwana: "kila mtu atokee nyumbani kwake kivyake vyake apinge kwa nguvu zake." Kwamba litaondoka.

Hiyo ndiyo Tanzania ya wajinga kwenye ubora wake.

Cc: mwanawao, Kalunya, antimatter
Mabadiliko hayaji kirahisi..

Ngoja kwanza raia wakamuliwe sanaa, ili kufikia 2025 majority wawe tayari kwa mabadiliko.

Ndo sababu baadhi ya watu wanamuona Mwigulu kama mkombozi, maana anatekeleza jukumu muhimu la kuamsha watu kutoka Kwa usingizi wa pono!
 
Mabadiliko hayaji kirahisi..

Ngoja kwanza raia wakamuliwe sanaa, ili kufikia 2025 majority wawe tayari kwa mabadiliko.

Ndo sababu baadhi ya watu wanamuona Mwigulu kama mkombozi, maana anatekeleza jukumu muhimu la kuamsha watu kutoka Kwa usingizi wa pono!

Kwani raia ni nani mkuu? Inafahamika kuwa aliyekuwa exempted hapa ni mlamba asali pekee.

Au ninyi wenzetu mko kwenye hiyo timu pendwa ya walamba asali?
 
Lawama na kelele zinazoendelea kuhusiana na uanzishwaji wa tozo za miamala na za kifedha sasa zimekuwa kama kelele za chura akiwa kwenye maji kwani hayamzuii tembo kuyanywa maji apatapo kiu.

Lawama na malalamiko mengi yameanza mwaka 2021 baada ya serikali kuanzishwa kwa tozo mbalimbali kwa lengo la kuinua uchumi wa Taifa kwa kasi jambo lililopelekea kupandishwa kwa tozo katika makampuni ya simu na hata taasisi za kifedha kama vile benki.

Lakini mwanzoni watumiaji wakubwa wa huduma hizi walilalamika kwa kuwa makato ni makubwa sana na kudai makato hayo yaweze kupunguzwa jambo ambalo limekuwa kama kelele zisizokuwa na faida kwani japokuwa kuna madai na malalamiko mengi kuhusiana na kupandishwa kwa kodi na tozo lakini bado watumiaji wengi wamezidi kutumia huduma hizo huku takwimu zikioneshwa kwamba matumizi hayo yanazidi kupanda kama BoT

View attachment 2333398

Na hat idadi ya mawakala imeongezeka jambo linaloonesha kuwa watumiaji wanazidi kutumia kwa kasi na wamekubaliana na tozo hizo.
View attachment 2333401
Hata hivyo, hivi karibuni tozo za miamala ya kibenki nayo imeanzishwa huku watu wengi wakilalamikia madai hayo na wakati huo huo takwimu zilizotolewa na BoT zinaonesha kuwa watumiaji wa miamala ya kibenki ni wachache kuliko watumiaji wa miamala ya Makampuni ya simu.
View attachment 2333405
Swali linabaki Je, kelele hizi zitakuwa ni za bure kama za tozo za miamala ya simu au zitafanyiwa kazi na watumiaji kwa ujumla na wakati bado watu wanatumia kwa kasi huku takwimu zinaonesha kuwa kila siku inazidi tu kupanda?
Watu watakubali tu. Baada ya wiki moja, utaona kimya.
 
Watu tunapiga kelele wao wapo busy kupiga picha na watu wa Sensa...kama vile hawajui kitu chochote
 
Back
Top Bottom