Je, Kisukari kina tiba? Fahamu tafiti zilipofikia mpaka sasa

Je, Kisukari kina tiba? Fahamu tafiti zilipofikia mpaka sasa

Dr Adinan

Member
Joined
Jul 11, 2021
Posts
14
Reaction score
22
Kama una miaka 30+ uko katika hatari ya kupata kisukari. ๐—๐—ฒ, ๐—ธ๐—ถ๐˜€๐˜‚๐—ธ๐—ฎ๐—ฟ๐—ถ ๐—ธ๐—ถ๐—ป๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ฏ๐—ถ๐—ธ๐—ฎ? ๐— ๐—ฝ๐—ฎ๐—ธ๐—ฎ ๐˜€๐—ฎ๐˜€๐—ฎ ๐—ต๐—ฎ๐—ถ๐—ท๐—ฎ๐—ณ๐—ฎ๐—ต๐—ฎ๐—บ๐—ถ๐—ธ๐—ฎ ๐—ฑ๐—ฎ๐˜„๐—ฎ ๐—ถ๐—ป๐—ฎ๐˜†๐—ผ ๐˜๐—ถ๐—ฏ๐˜‚ ๐—ธ๐—ถ๐˜€๐˜‚๐—ธ๐—ฎ๐—ฟ๐—ถ

Wengine wakiwa na imani kwamba kila ugonjwa una tiba yake, kwasasa dunia bado haijapata dawa ya kutibu ugonjwa huu mbaya na hatari. Kisukari inaongoza kwa kusababisha ulemavu kwasababu ya kukatwa miguu. Ya pili nyuma ya ajali.

Dawa zilizopo, nyingi zikiwa ziko kwenye majaribio, hupunguza kiwango cha sukari kwenye damu. Hivyo mtu hutakiwa kunywa dawa hizi kulingana na ufanyaji kazi wa dawa anazotumia na muda dawa inapoisha nguvu.

Ndiyo maana utakuta wengine hunywa/ kujichoma mara mbili kwa siku au mara moja.

Kwakuwa lengo ni kushusha sukari na kuwa katika kiwango kinachokubailka kwamba hakina madhara, njia mbalimbali zinatumika kukamilisha lengo hili.

Ikumbukwe kwamba tiba ya kisukari ina malengo matatu:

1. kushusha sukari kwenye damu mpaka kiwango kinachokubalika ki afya;
2. Kudhibiti madhara ya kisukari, na
3. Kukinga madhara ya kisukari.

Tiba ya kisukari kwahiyo nayo imegawanyika katika mafungu hayo matatu.

Yafaa kukumbuka pia, kitabibu, tiba hujumuisha ugunduzi wa tatizo la kiafya, tiba yenyewe/dawa, kisha ufuatiliaji / tathmini ya tiba

1. Tumeshafahamu namna ambavyo mtu huweza kufahamu kama ana kisukari na vipimo vinavyotumika. Glucose (Glucometer), HbA1C.

2. Pia tukasoma vifaa ambavyo mtu huweza kutumia kubaini kama ana madhara ya kisukari au yuko katika hatari ya kupata madhara ya kisukari, mizani ya uzito, kipimo cha hisia miguuni, BMI, kipimo cha presha, vipimo vya moyo na figo, na macho, vinavyofanyika hospitali.

Ya kuzingatia katika tiba ya kisukari ni kwamba tiba hii ni jumuishi: dawa + mabadiliko ya mfumo wa maisha - Mfumo wa maisha nikimaanisha kuacha yale ambayo hukuwekea kwenye hatari zaidi na kufanya yale ambayo yanaboresha afya yako na, + kufanya vipimo muhimu kufuatilia hali yako kwa ukaribu. Mfano kuacha sigara, kuacha kutumia sukari kwa wingi, kufahnya shughuli zinazochangamsha mwili/mazoezi na kupanga mlo wako.

Kuhahikikisha kwamba kila wakati unafanya tathmini ya tiba yako. Je, umeweza kudhibiti sukari? Je, umeweza kudhibiti vihatarishi vyote vya kupata madhara ya kisukari? Je, dawa inafanya kazi kama ilivyokusudiwa?

Hapa namaanisha kupima hali yako na kuhudhuria kliniki kwa tarehe zilie mlizokubaliana na tabibu wako.

Kuhakikisha unatumia dawa kama ulivyoelekezwa na tabibu wako .

Na kuhakikisha uko makini kutambua vihatarishi vyote vya madhara ya kisukari kama vile kucha kubwa miguuni au kutokuvaa viatu vinavyo kubana sana miguu ambavyo vyote vinaweza kusababisha kupata vidonda miguuni.

Umuhimu wa kuweza kujipima ukiwa nyumbani unajitokeza hapa, Kwasababu kikawaida huwa mgonjwa anahudhuria kliniki angalau kila baada ya mwezi. Kwa mtu anayejali afya yake angependa kufahamu hali yake inavyoendelea kabla ya kuenda kliniki.

Rafiki yako,
Dr. Adinan J.
 
Kama una miaka 30+ uko katika hatari ya kupata kisukari. ๐—๐—ฒ, ๐—ธ๐—ถ๐˜€๐˜‚๐—ธ๐—ฎ๐—ฟ๐—ถ ๐—ธ๐—ถ๐—ป๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ฏ๐—ถ๐—ธ๐—ฎ? ๐— ๐—ฝ๐—ฎ๐—ธ๐—ฎ ๐˜€๐—ฎ๐˜€๐—ฎ ๐—ต๐—ฎ๐—ถ๐—ท๐—ฎ๐—ณ๐—ฎ๐—ต๐—ฎ๐—บ๐—ถ๐—ธ๐—ฎ ๐—ฑ๐—ฎ๐˜„๐—ฎ ๐—ถ๐—ป๐—ฎ๐˜†๐—ผ ๐˜๐—ถ๐—ฏ๐˜‚ ๐—ธ๐—ถ๐˜€๐˜‚๐—ธ๐—ฎ๐—ฟ๐—ถ

Wengine wakiwa na imani kwamba kila ugonjwa una tiba yake, kwasasa dunia bado haijapata dawa ya kutibu ugonjwa huu mbaya na hatari. Kisukari inaongoza kwa kusababisha ulemavu kwasababu ya kukatwa miguu. Ya pili nyuma ya ajali.

Dawa zilizopo, nyingi zikiwa ziko kwenye majaribio, hupunguza kiwango cha sukari kwenye damu. Hivyo mtu hutakiwa kunywa dawa hizi kulingana na ufanyaji kazi wa dawa anazotumia na muda dawa inapoisha nguvu.

Ndiyo maana utakuta wengine hunywa/ kujichoma mara mbili kwa siku au mara moja.

Kwakuwa lengo ni kushusha sukari na kuwa katika kiwango kinachokubailka kwamba hakina madhara, njia mbalimbali zinatumika kukamilisha lengo hili.

Ikumbukwe kwamba tiba ya kisukari ina malengo matatu:

1. kushusha sukari kwenye damu mpaka kiwango kinachokubalika ki afya;
2. Kudhibiti madhara ya kisukari, na
3. Kukinga madhara ya kisukari.

Tiba ya kisukari kwahiyo nayo imegawanyika katika mafungu hayo matatu.

Yafaa kukumbuka pia, kitabibu, tiba hujumuisha ugunduzi wa tatizo la kiafya, tiba yenyewe/dawa, kisha ufuatiliaji / tathmini ya tiba

1. Tumeshafahamu namna ambavyo mtu huweza kufahamu kama ana kisukari na vipimo vinavyotumika. Glucose (Glucometer), HbA1C.

2. Pia tukasoma vifaa ambavyo mtu huweza kutumia kubaini kama ana madhara ya kisukari au yuko katika hatari ya kupata madhara ya kisukari, mizani ya uzito, kipimo cha hisia miguuni, BMI, kipimo cha presha, vipimo vya moyo na figo, na macho, vinavyofanyika hospitali.

Ya kuzingatia katika tiba ya kisukari ni kwamba tiba hii ni jumuishi: dawa + mabadiliko ya mfumo wa maisha - Mfumo wa maisha nikimaanisha kuacha yale ambayo hukuwekea kwenye hatari zaidi na kufanya yale ambayo yanaboresha afya yako na, + kufanya vipimo muhimu kufuatilia hali yako kwa ukaribu. Mfano kuacha sigara, kuacha kutumia sukari kwa wingi, kufahnya shughuli zinazochangamsha mwili/mazoezi na kupanga mlo wako.

Kuhahikikisha kwamba kila wakati unafanya tathmini ya tiba yako. Je, umeweza kudhibiti sukari? Je, umeweza kudhibiti vihatarishi vyote vya kupata madhara ya kisukari? Je, dawa inafanya kazi kama ilivyokusudiwa?

Hapa namaanisha kupima hali yako na kuhudhuria kliniki kwa tarehe zilie mlizokubaliana na tabibu wako.

Kuhakikisha unatumia dawa kama ulivyoelekezwa na tabibu wako .

Na kuhakikisha uko makini kutambua vihatarishi vyote vya madhara ya kisukari kama vile kucha kubwa miguuni au kutokuvaa viatu vinavyo kubana sana miguu ambavyo vyote vinaweza kusababisha kupata vidonda miguuni.

Umuhimu wa kuweza kujipima ukiwa nyumbani unajitokeza hapa, Kwasababu kikawaida huwa mgonjwa anahudhuria kliniki angalau kila baada ya mwezi. Kwa mtu anayejali afya yake angependa kufahamu hali yake inavyoendelea kabla ya kuenda kliniki.

Rafiki yako,
Dr. Adinan J.
Mkuu ninakubaliana na wewe kuwa maradhi ya kisukari hayana dawa za kutibu kutoka Mahospitalini. Lakini sikubaliani na wewe kuwa ugonjwa wa kisukari kuwa hauna dawa. Ugonjwa wa kisukari unao dawa yake mimi ninayo dawa ya kutibu huo ugonjwa wa kisukari na mgonjwa akitumia dawa zangu kwa muda wa miezi 3 atakuwa ameshapona ugonjwa wa kisukari. Sio tu Ugonjwa wa Kisukari hauna dawa hospitalini peke yake kuna maradhi ya kiharusi aka Stroke na maradhi ya Ukimwi na maradhi ya saratani za aina zote na maradhi figo kufeli na maradhi ya homa ya ini na maradhi ya wenda wazimu na maradhi ya kifafa na Maradhi ya masiko kupiga makelele aka Tinnitus na maradhi yote yanayotokana na virus hakuna tiba hospitalini lakini kwa dawa zetu za asili mtu akitumia anapona kabisa maradhi yote hayo.
 
Mkuu ninakubaliana na wewe kuwa maradhi ya kisukari hayana dawa za kutibu kutoka Mahospitalini. Lakini sikubaliani na wewe kuwa ugonjwa wa kisukari kuwa hauna dawa. Ugonjwa wa kisukari unao dawa yake mimi ninayo dawa ya kutibu huo ugonjwa wa kisukari na mgonjwa akitumia dawa zangu kwa muda wa miezi 3 atakuwa ameshapona ugonjwa wa kisukari. Sio tu Ugonjwa wa Kisukari hauna dawa hospitalini peke yake kuna maradhi ya kiharusi aka Stroke na maradhi ya Ukimwi na maradhi ya saratani za aina zote na maradhi figo kufeli na maradhi ya homa ya ini na maradhi ya wenda wazimu na maradhi ya kifafa na Maradhi ya masiko kupiga makelele aka Tinnitus na maradhi yote yanayotokana na virus hakuna tiba hospitalini lakini kwa dawa zetu za asili mtu akitumia anapona kabisa maradhi yote hayo.
Nashukuru mkuu. Hapo utakuwa umekalia utajiri Dr. Mzizi Mkavu. Leta hiyo dawa tusaidie watu huku nasi tukineemeka.
 
Nashukuru mkuu. Hapo utakuwa umekalia utajiri Dr. Mzizi Mkavu. Leta hiyo dawa tusaidie watu huku nasi tukineemeka.
Haya asante wanaotaka dawa ya kutibu maradhi ya kisukari ninayo wanitafute kwa wakati wao ili nipate kuwatibia maradhi yao.
 
Dawa ya sukari unayo au sijaelewa sukari huu huu ugonjwa au unamaana gani
 
Mkuu ninakubaliana na wewe kuwa maradhi ya kisukari hayana dawa za kutibu kutoka Mahospitalini. Lakini sikubaliani na wewe kuwa ugonjwa wa kisukari kuwa hauna dawa. Ugonjwa wa kisukari unao dawa yake mimi ninayo dawa ya kutibu huo ugonjwa wa kisukari na mgonjwa akitumia dawa zangu kwa muda wa miezi 3 atakuwa ameshapona ugonjwa wa kisukari. Sio tu Ugonjwa wa Kisukari hauna dawa hospitalini peke yake kuna maradhi ya kiharusi aka Stroke na maradhi ya Ukimwi na maradhi ya saratani za aina zote na maradhi figo kufeli na maradhi ya homa ya ini na maradhi ya wenda wazimu na maradhi ya kifafa na Maradhi ya masiko kupiga makelele aka Tinnitus na maradhi yote yanayotokana na virus hakuna tiba hospitalini lakini kwa dawa zetu za asili mtu akitumia anapona kabisa maradhi yote hayo.
Acha huu uongo wako na utapeli
 
Back
Top Bottom