Je, kitambulisho cha taifa na cheti cha kuzaliwa havitoshi mpaka tena uwe na barua kutoka serikali za mitaa?

Je, kitambulisho cha taifa na cheti cha kuzaliwa havitoshi mpaka tena uwe na barua kutoka serikali za mitaa?

Mkoba wa Mama

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2021
Posts
208
Reaction score
91
Ni kawaida mtu anapotuma maombi ya kazi atatakiwa kuambatanisha baadhi ya nyaraka, lakini hizi nyaraka zote kwa wakati mmoja ni kwa ajili ya nini?

Mtu anatuma maombi anatakiwa aambatanishe kitambulisho cha taifa, cheti cha kuzaliwa na hapohapo tena barua kutoka serikali za mitaa. Ina maana kitambulisho cha taifa hakitoshi au hakijitoshelezi mpaka tena kuwepo na barua kutoka serikali za mitaa?

Mimi naona hizi barua kutoka serikali za mitaa zibaki kwenye maombi ya kazi ambazo zinahitaji mzaliwa wa eneo fulani (mwenyeji) na isitumike kwenye maombi ya kazi za kitaifa ambazo mtu yeyote anaweza kuajiliwa mahala popote pale.

Hali hii inaleta usumbufu na mlolongo mrefu kwa waombaji wa kazi husika na usumbufu pia kwa waombaji na hata kwa viongozi wa serikali za mitaa.
 
Wakati unazaliwa - vyeti vya utambulisho vya wazazi
Wakati unaandikishwa shule - cheti cha kuzaliwa
Chuo, mikopo - cheti cha kuzaliwa na kitambulisho cha taifa
Kuomba kazi - cheti cha kuzaliwa, kitambulisho cha taifa na barua ya mtendaji
Kwenda enterview Dodoma SGR - cheti cha uraia, barua ya utambulisho yenye picha
kuajiriwa - cheti cha kuzaliwa, kitambulisho cha taifa, barua ya mtendaji, fomu za daktari, cheti cha mpiga kura
Subiri kustaafu - vyote hapo juu uwe navyo na nyongeza juu
Total confussion
jumla mchanganyiko shagala bagala
 
Ni kawaida mtu anapotuma maombi ya kazi atatakiwa kuambatanisha baadhi ya nyaraka, lakini hizi nyaraka zote kwa wakati mmoja ni kwa ajili ya nini?

Mtu anatuma maombi anatakiwa aambatanishe kitambulisho cha taifa, cheti cha kuzaliwa na hapohapo tena barua kutoka serikali za mitaa. Ina maana kitambulisho cha taifa hakitoshi au hakijitoshelezi mpaka tena kuwepo na barua kutoka serikali za mitaa?

Mimi naona hizi barua kutoka serikali za mitaa zibaki kwenye maombi ya kazi ambazo zinahitaji mzaliwa wa eneo fulani (mwenyeji) na isitumike kwenye maombi ya kazi za kitaifa ambazo mtu yeyote anaweza kuajiliwa mahala popote pale.

Hali hii inaleta usumbufu na mlolongo mrefu kwa waombaji wa kazi husika na usumbufu pia kwa waombaji na hata kwa viongozi wa serikali za mitaa.
Zinatosha ila Wenyeviti wa serikali za mitaa hawana mishahara, mnapoambiwa mkachukue barua kuna ile nanii mnachaga pale , inasaidia kusukuma maisha yao.
 
Hivyo ni vitu vinavyorahisisha ukifanya uharifu ukamatwe kirahisi.
 
Nida umesajili kibamba kazi uombe dodoma unaishi dodoma. Ukipotea? Kama una kesi za jinai? Kama unatafutwa, unadhani wapi itakua chimbuko lako, na wapi utakua makazi yako itafahamika vipi.

It carries your history. Ni muhimu sana katika ajira. Maana mpaka upate hyo barua fahamu unakua umeheshimika sana.
Kuwa mwizi mtaani kwenu au fanya fujo mtaa husika kama utaipata hyo barua.
 
Barua kutoka serikali za mitaa inarahisisha nini? Una uhakika huyo mtu ataashi mtaa huo kwa mda gani?
barua ya serikali za mtaa ili upate lazima uwe mkaazi wa eneo hilo!hata ikitokea ukahama bado ni rahisi kukushika lazima kuna alama utaziacha sehemu uliyowahi kuishi.
 
Nida umesajili kibamba kazi uombe dodoma unaishi dodoma. Ukipotea? Kama una kesi za jinai? Kama unatafutwa, unadhani wapi itakua chimbuko lako, na wapi utakua makazi yako itafahamika vipi.

It carries your history. Ni muhimu sana katika ajira. Maana mpaka upate hyo barua fahamu unakua umeheshimika sana.
Kuwa mwizi mtaani kwenu au fanya fujo mtaa husika kama utaipata hyo barua.
Umefafanua vizuri sana
 
Nida umesajili kibamba kazi uombe dodoma unaishi dodoma. Ukipotea? Kama una kesi za jinai? Kama unatafutwa, unadhani wapi itakua chimbuko lako, na wapi utakua makazi yako itafahamika vipi.

It carries your history. Ni muhimu sana katika ajira. Maana mpaka upate hyo barua fahamu unakua umeheshimika sana.
Kuwa mwizi mtaani kwenu au fanya fujo mtaa husika kama utaipata hyo barua.
Wewe unahisi hizo barua watu wote wanazichukulia mahali walipozaliwa au kwenye makazi yao ya kudumu? Mtu anachukua barua mahali ambapo tangazo la kazi limemkuta anaishi kwa wakati huo
 
Wewe unahisi hizo barua watu wote wanazichukulia mahali walipozaliwa au kwenye makazi yao ya kudumu? Mtu anachukua barua mahali ambapo tangazo la kazi limemkuta anaishi kwa wakati huo
Kama kweli una akili timamu na unajua kusoma utaelewa maana yangu. Wengi wanachukulia popote, ila ulippchukulia inaonyesha kwamba umeaminika beyond doubt kupewa. Na ni rahisi kupatikana details zako, na kwamba anayetuma maombi ni mtu na si roboti. Chukua popote ila physically ulionekana. Jifunze kusoma.
 
Kama kweli una akili timamu na unajua kusoma utaelewa maana yangu. Wengi wanachukulia popote, ila ulippchukulia inaonyesha kwamba umeaminika beyond doubt kupewa. Na ni rahisi kupatikana details zako, na kwamba anayetuma maombi ni mtu na si roboti. Chukua popote ila physically ulionekana. Jifunze kusoma

Kama kweli una akili timamu na unajua kusoma utaelewa maana yangu. Wengi wanachukulia popote, ila ulippchukulia inaonyesha kwamba umeaminika beyond doubt kupewa. Na ni rahisi kupatikana details zako, na kwamba anayetuma maombi ni mtu na si roboti. Chukua popote ila physically ulionekana. Jifunze kusoma.
Kwa hiyo wakati unaandikishwa na kupewa kitambulisho cha taifa ulikua huaminiki? Hukuonekana physically? Wakitaka details zako hawawezi kuzipata kupitia NIDA?
 
Ni kawaida mtu anapotuma maombi ya kazi atatakiwa kuambatanisha baadhi ya nyaraka, lakini hizi nyaraka zote kwa wakati mmoja ni kwa ajili ya nini?

Mtu anatuma maombi anatakiwa aambatanishe kitambulisho cha taifa, cheti cha kuzaliwa na hapohapo tena barua kutoka serikali za mitaa. Ina maana kitambulisho cha taifa hakitoshi au hakijitoshelezi mpaka tena kuwepo na barua kutoka serikali za mitaa?

Mimi naona hizi barua kutoka serikali za mitaa zibaki kwenye maombi ya kazi ambazo zinahitaji mzaliwa wa eneo fulani (mwenyeji) na isitumike kwenye maombi ya kazi za kitaifa ambazo mtu yeyote anaweza kuajiliwa mahala popote pale.

Hali hii inaleta usumbufu na mlolongo mrefu kwa waombaji wa kazi husika na usumbufu pia kwa waombaji na hata kwa viongozi wa serikali za mitaa.
Barua ya serikali ya mtaa ni muhimu, ndio uthibitisho wa makazi yako
 
Hivyo ni vitu vinavyorahisisha ukifanya uharifu ukamatwe kirahisi.
Wengine hulipa posho za usafiri au usafiri au nyumba kujua unaishi wapi kwao muhimu
Pia ni njia ya kukujua kuwa unakoishi kuna watu wanakujua wasijeajiri mtu asiyejulikana akaleta shida mbele
 
Back
Top Bottom