Nikupateje
JF-Expert Member
- Dec 22, 2009
- 1,334
- 989
Wakati bunge likiendelea kujadili bajeti ya Wizara ya habari, vijana, jana jioni wabunge wawili Ester Bulaya na Vicky Kamata walichangia mzozo kati ya Lady JD na Ruge.
Wote wametoa maoni umalizwe nje ya mahakama.
Maana yake nini? Maana yake yule aliyetumia uhuru usioingiliwa kikatiba wa kufungua kesi, aliona amefanya uamuzi sahihi.
Anayajua yote hayo ya kufamaliza nje ya mahakama. Lakini akili yake imechagua uamuzi wa mahakamani kwa sababu ambazo sisi hatuwezi kumpangia.
Sasa, tunapotoa maoni tena public kwamba aangalie uamuzi mwingine. Binafsi nilidhani ilikuwa ni sahihi kama angekuwa yuko katika hatua ya kutafakari options nyingi za suluhu.
Kwamba kama katika options hizo za mawazo, tungekuwa na haki ya kusema, Bwana, tumia option fulani achana na option ya mahakamani.
Sasa, mwenzetu ambaye hatuwezi kumfundisha options zinazomfurahisha, kaamua kwenda mahakamani. Sasa, baadhi yetu, tunasema option aliyochagua aachane nayo, achukue tunayoitaka.
Tuliona hansard, ilivyotumika kama ushahidi kwenye kesi ya Prof. Costa Mahalu. Hansard ya jana inaonyesha majadiliano na mapendekezo hayo kwa suala la JD na Ruge.
Je, mle bungeni, hili si jambo ambalo linajadiliwa mahakamani na haliruhusiwi kama yalivyowahi kugomewa mengi mle bungeni kwa sababu yana kesi Mahakamani?
Huu ndiyo wasiwasi wangu.
SAIDIA KUONDOA WASIWASI HUO
Wote wametoa maoni umalizwe nje ya mahakama.
Maana yake nini? Maana yake yule aliyetumia uhuru usioingiliwa kikatiba wa kufungua kesi, aliona amefanya uamuzi sahihi.
Anayajua yote hayo ya kufamaliza nje ya mahakama. Lakini akili yake imechagua uamuzi wa mahakamani kwa sababu ambazo sisi hatuwezi kumpangia.
Sasa, tunapotoa maoni tena public kwamba aangalie uamuzi mwingine. Binafsi nilidhani ilikuwa ni sahihi kama angekuwa yuko katika hatua ya kutafakari options nyingi za suluhu.
Kwamba kama katika options hizo za mawazo, tungekuwa na haki ya kusema, Bwana, tumia option fulani achana na option ya mahakamani.
Sasa, mwenzetu ambaye hatuwezi kumfundisha options zinazomfurahisha, kaamua kwenda mahakamani. Sasa, baadhi yetu, tunasema option aliyochagua aachane nayo, achukue tunayoitaka.
Tuliona hansard, ilivyotumika kama ushahidi kwenye kesi ya Prof. Costa Mahalu. Hansard ya jana inaonyesha majadiliano na mapendekezo hayo kwa suala la JD na Ruge.
Je, mle bungeni, hili si jambo ambalo linajadiliwa mahakamani na haliruhusiwi kama yalivyowahi kugomewa mengi mle bungeni kwa sababu yana kesi Mahakamani?
Huu ndiyo wasiwasi wangu.
SAIDIA KUONDOA WASIWASI HUO