Je kuna kitu choche cha maana au kizuri watanzania wanaweza kujifunza au kujivunia toka CCM ya sasa na uchawa wake?

Father of All

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
7,672
Reaction score
9,039
Huwa siachi kujiuliza. Tangu CCM itekwe na mafisadi, kuna kitu cha maana au kizuri tunaweza kujivunia kama watanzania?

Kila uchao, kuna matukio ya utekaji, tunapotezwa, tunatishwa, na watu wasiojulikana tunayonywa, tunadharauliwa, tunauzwa na kubinafsishwa, tunanyamazishwa, tunachanganywa na kuchanganyikiwa bila kusahau wanaotuchanganya nao wakajichanganya.

Tumegeuka kituko bila sababu japo wahusika wanaendelea kufanya vituko na kutaka wasifiwe kwa hilo.

Leo ukiulizwa wazi wazi au sirini, kipo kweli cha kujifunza au kujivunia toka kwa CCM ya sasa?
 
Nimejifunza kutumia Miguvu na kufurahia uongo bila aibu Wala kujali umri niilionao.
 
Hakuna
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…