Je, kuna penzi la milele?

Je, kuna penzi la milele?

Tausi Mzalendo

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2010
Posts
1,470
Reaction score
722
Kuanza penzi ni raha, kwisha kwa penzi nako raha?
Wengi watasema ni machungu, kilio na simanzi
hasa kwa yule ambaye bado anapenda.

Wengi hutamani penzi liwe la milele.....
wengi hutamani kama ni ndoto basi wasiamke ili iendelee.

Wengine huona kama penzi lao ni njama kutoka juu!
Wengine , wenye kupenda kuangalia mambo kwa jicho la tatu watakuambia
Penzi lenye mwanzo, halina budi kuisha!
Kwanini basi wengi hufikiria kuwa penzi lao litakuwa la milele?


Je, ni vibaya uwapo mapenzini kuwazia kuwa kila chenye mwanzo hakikosi mwisho ?
Je ni vibaya kujiandaa kwa mwisho wa penzi?
Hebu tupe uzoefu wako ewe mwenzetu.
 
wajua ukiwa waanza mapenzi hisia hujaa mwili kiasi cha kwamba tunatarajia mema tuu na hta chembe chembe za kuwa mahusiano yanaweza isha hayapo kabisa....mwili unafuraha sasa wewe kweli utakuwa na akili ya kuwaza mabaya...ebo!!!
sasa kaa unajiaanda kwa mwisho wa mapenzi uju kweli hapo hujapenda...ni kwamba wewe upo kistarehe zaidi...kuchachuana tuu
 
wajua ukiwa waanza mapenzi hisia hujaa mwili kiasi cha kwamba tunatarajia mema tuu na hta chembe chembe za kuwa mahusiano yanaweza isha hayapo kabisa....mwili unafuraha sasa wewe kweli utakuwa na akili ya kuwaza mabaya...ebo!!!
sasa kaa unajiaanda kwa mwisho wa mapenzi uju kweli hapo hujapenda...ni kwamba wewe upo kistarehe zaidi...kuchachuana tuu

KIPI BORA...kujidanganya kuwa hayawezi fikia ukingoni au kukubali kuwa kuna uwezekano huo?
 
kipi boro inategemea na madhumuni yako ya kuingia katika mapenzi na mpendwa wako....wewe kama unaingia kabisa ukiwa na nia ya kujuakuw mke au mume basi mwanzani kabisa utakuwa makini na uchaguzi wa huyo mpenzi.....mara nyingi mapenzi yanaisha kwa sababu watu wanakuwa wapo hapo kimwili zaidi na ulimwengu wa sasa tunaoishi unalifanya jambo la kuchachuana kitu cha kawaida na perhaps jabo ambalo lazima ujiingize kama wewe ni kijana .....hapo basi ndipo tatizo lilipokuwepo...so kuanzia mwanzoni msingi imara wakwamba haya mapenzi yaishie kudumu hajajengwa.
 
Mapenzi ni taamuli * Si kila mtu hujua
Mpendanapo kwa kweli * Bila ya kusuasua
Penzi hua la ukweli * Mkaishi kwa murua
Bali kwa ndumakuwili * Hufa likishachanua
Mapenzi ni pande mbili!

Sumu ya pendo maudhi * Iwapo yatatokea
Au kama halikidhi * Lile ulotarajia
Na mwengine kutoridhi * Maovu kumtendea
Ingawa kuna baadhi * Waweza kuvumilia
Mapenzi ni pande mbili!

Mpende akupendae * Shauri langu natoa
Yule akudanganyae * Huyo hapendi tambua
Ya nini kukaa nae * Akutese ukijua
Tafuta akufaae * Kupanga ni kuchagua
Mapenzi ni pande mbili!
 
kipi boro inategemea na madhumuni yako ya kuingia katika mapenzi na mpendwa wako....wewe kama unaingia kabisa ukiwa na nia ya kujuakuw mke au mume basi mwanzani kabisa utakuwa makini na uchaguzi wa huyo mpenzi.....mara nyingi mapenzi yanaisha kwa sababu watu wanakuwa wapo hapo kimwili zaidi na ulimwengu wa sasa tunaoishi unalifanya jambo la kuchachuana kitu cha kawaida na perhaps jabo ambalo lazima ujiingize kama wewe ni kijana .....hapo basi ndipo tatizo lilipokuwepo...so kuanzia mwanzoni msingi imara wakwamba haya mapenzi yaishie kudumu hajajengwa.

Mzabzab na wewe!!
Hebu edit kidogo basi ili tukuelewe.....nashindwa hata kukuuliza maswali
 
Nimekumbuka wimbo wa afande Sele, wanaimba mambo yasiyo na maana, na yenye maana hayana vina.........lol! Ila jitahidi unaweza ukafanikiwa, haya mambo yana wenyewe mkuu
 
Penzi la dhati km lipo lipo kwa upande 1,kwa maana kuwa unaweza ww ukawa unampenda m2 kwa dhati lakn yy hakupend hvyo na kinyume chake.
penzi la dhat kwa wote wawili camin uwepo wake.
 
hakuna penzi la milele bibie,sometime kuvunjika kwa penzi ni raha ili kujiepusha na mibalaa ambayo ungekumbana nayo kwake. Nalog off
 
Back
Top Bottom