Je, kuna uhusiano ule mgomo wa wafanyabiashara wa Kariakoo na hiki kinachoendelea sasa hivi?

Je, kuna uhusiano ule mgomo wa wafanyabiashara wa Kariakoo na hiki kinachoendelea sasa hivi?

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Sabato NJEMA Wakuu!

Ufanisi ni mdogo, faida ni hafifu. Mtaji ni Duni, Muda unaopotezwa ni mwingi Hali inayozorotesha uchumi wa wafanyabiashara na serikali Kwa ujumla. Hicho ndicho kinafanya kuwe na haja ya kuleta Wawekezaji katika Bandari yetu.

Uwezo wetu ni mdogo, uwezo wa kinidhamu na uadilifu WA Watu wetu bado unatia mashaka. Wizi na ufisadi umekuwa ugonjwa miongoni mwetu Kwa kipindi kirefu. Taarifa za CAG kila Mwaka zinathibitisha tunahitaji msaada sio tuu wa kimtaji Bali pia wa kiuongozi kwani uadilifu na Uzalendo kwetu imekuwa kama Bikra kwenye Wodi ya Wazazi.

Ninaweza kuungana na yeyote mwenye uadilifu na ufanisi katika kuleta Maendeleo. Watanzania badala ya kusikitika na kulalamika Kwa nini Waarabu au mataifa mengine wanapewa fursa ya kuwekeza katika Nchi yetu, tunatakiwa tuwe waadilifu na wazalendo.

Kimsingi watanzania wengi wetu sio waaminifu, sio waadilifu, wengi ni majizi. Kama huamini au utaniona ninatukana basi unaweza kuchukua Nguo yako na kumpelekea fundi nguo alafu uone nini kitatokea. Au mpe kijana Bodaboda akuletee hesabu uone kama hamtasumbuana. Au mpe fundi mwashi kazi ya ujenzi alafu usimsimamie uone nini kitatokea.
Au kwenye Msiba au harusi uone Watu wakiiba chakula, mafuta na vinywaji.

Hivyo ndivyo wengi wetu tulivyo. Tufanye namna tukoke kwenye huo mkwamo.

Haya mpe mtanzania uongozi badala ya kusaidia Ndugu zake, ataanza kujiwekea Ulinzi ili aibe vizuri. Na ukisema ukweli utaishia Kufungwa, kuingia kwenye Matatizo ikiwezekana kuuawa. Hivyo ndivyo watanzania wengi wetu tulivyo.

Kwa upande wangu sio tatizo ikiwa tutakodisha baadhi ya miradi au taasisi au mashirika ikiwa Sisi wenyewe tunashindwa kujisimamia. Lengo likiwa ni kupata faida na Kupata tija iliyokusudiwa.

Muhimu ni mikataba iwe mizuri yenye kulinda maslahi ya taifa na sio kikundi cha watu

Mgomo wa wafanyabiashara wa Kariakoo unauhusiano wowote na hiki kinachoendelea?

Sabato njema tena!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Sabato NJEMA Wakuu!

Ufanisi ni mdogo, faida ni hafifu. Mtaji ni Duni, Muda unaopotezwa ni mwingi Hali inayozorotesha uchumi wa wafanyabiashara na serikali Kwa ujumla. Hicho ndicho kinafanya kuwe na haja ya kuleta Wawekezaji katika Bandari yetu.
Uhusiano upo lakini hii agenda sio ya juzi ni jambo la muda ambalo limeletwa hadharani siku sio nyingi.

Mgomo wa wafanya biashara labda imekuwa kama backing ya agenda husika.
 
Uhusiano upo lakini hii agenda sio ya juzi ni jambo la muda ambalo limeletwa hadharani siku sio nyingi.

Mgomo wa wafanya biashara labda imekuwa kama backing ya agenda husika.

Na hicho ndicho ninachokiongelea kuwa Ile mgomo huenda ilikuwa na Starter ya kinachoendelea?
 
Na hicho ndicho ninachokiongelea kuwa Ile mgomo huenda ilikuwa na Starter ya kinachoendelea?
Labda serikali iliona sasa kama imepata mahali pakuanzia baada ya mgomo. Kwamba wangepata support kubwa kutoka kwa wafanyabiashara hivyo wange push agenda faster.
 
Acha wale coz wameruhusiwa kula!!

Sema hawajaweka wazi kama nchi tutakua tunaingiza sh.ngapi KWA mwaka yaani kimapato!!

Mkataba mkataba kelele tu SASA tutaingiza sh ngapi KWA mwaka!!?
 
Waweke wazi basi hayo makubaliano wanayotaka kuingia na hao wadubai wananchi wote tuyapitie, na mchakato uendelee kuwa wa uwazi kwa kila hatua
 
Labda serikali iliona sasa kama imepata mahali pakuanzia baada ya mgomo. Kwamba wangepata support kubwa kutoka kwa wafanyabiashara hivyo wange push agenda faster.

Tatizo la Sisi wabongo kila kitu tunakitazama katika namna ya kutafuta mwanya wa kupiga Pesa. Hapo ndipo tunapokwama
 
Waweke wazi basi hayo makubaliano wanayotaka kuingia na hao wadubai wananchi wote tuyapitie, na mchakato uendelee kuwa wa uwazi kwa kila hatua

Uwazi ndio kinachoendelea Huko bungeni. Ukiona Jambo lolote bungeni linajadiliwa ujue tayari mwananchi upo pale na unajadili Jambo hilo kupitia mbunge wako.

Kuhusu kila hatua upo Sahihi
 
Acha wale coz wameruhusiwa kula!!

Sema hawajaweka wazi kama nchi tutakua tunaingiza sh.ngapi KWA mwaka yaani kimapato!!

Mkataba mkataba kelele tu SASA tutaingiza sh ngapi KWA mwaka!!?

Mbona wameeleza makadirio wanaoyategemea,
Ifikapo 2031 nchi itanufaika Kwa mapato yanayotokana na Bandari zaidi ya Trillion 27 Kutoka Trillion 7 ya hivi leo.
 
Ni kweli, lakini naamini sifa ulizotaja si za kuzaliwa nazo, ni sifa unazozipata baada ya kujifunza (kuona, kusikia, kusoma, kugusa etc). Je sisi 'Wabongo' tunaweza jifunza wapi, nini?

Uadilifu Watu wanajifunza Kwa wazazi na Walezi wao. Zaidi ya hapo hakuna pengine labda uzaliwe nao
 
Back
Top Bottom