Je, kuna uhusiano ule mgomo wa wafanyabiashara wa Kariakoo na hiki kinachoendelea sasa hivi?

Je, kuna uhusiano ule mgomo wa wafanyabiashara wa Kariakoo na hiki kinachoendelea sasa hivi?

Uadilifu Watu wanajifunza Kwa wazazi na Walezi wao. Zaidi ya hapo hakuna pengine labda uzaliwe nao
Okay, hii ni mada ndefu kidogo, maana wazazi nao inabidi wawe wamejifunza sehemu n.k

Nionavyo mimi ni kuwa, tunatakiwa kuanza sehemu (Tanganyika/Tanzania - haijawahi kufanya hichi)

Tunaanza kwa kujiwekea (sisi WANANCHI) muongozo/sheria/katiba yenye;
- kuhaikisha kuwa Tanganyika ni Republic ( hakuna mfalme/malkia )
- msingi wa HAKI SAWA Kwa Wananchi wote.
- kuhakikisha kuwa Uongozi ni UWAKILISHI (representation not a rulership), na kuwapa WAWAKILISHWA nguvu zaidi ya pamoja kuliko MWAKILISHI.
  • kuhakikisha MALI asili au man-made ya Taifa, inalinufaisha Taifa kwa asilimia zisizopungua 80 (80%)
  • e.t.c

Tumechelewa sana, lakini tukianza hapa, tutaweza;
  • Kuanza kuchuja wasiofaa kutoka kwenye uongozi.
  • wananchi watakua na pakujifunza e.g hata ukiwa raisi, ukipatikana na hatia ya jinai, unaadhibiwa kama mwananchi yeyote.
  • e.t.c

Hii ni kwa kifupi sana, lakni naamini umeelewa ninachomaanisha.
 
Okay, hii ni mada ndefu kidogo, maana wazazi nao inabidi wawe wamejifunza sehemu n.k

Nionavyo mimi ni kuwa, tunatakiwa kuanza sehemu (Tanganyika/Tanzania - haijawahi kufanya hichi)

Tunaanza kwa kujiwekea (sisi WANANCHI) muongozo/sheria/katiba yenye;
- kuhaikisha kuwa Tanganyika ni Republic ( hakuna mfalme/malkia )
- msingi wa HAKI SAWA Kwa Wananchi wote.
- kuhakikisha kuwa Uongozi ni UWAKILISHI (representation not a rulership), na kuwapa WAWAKILISHWA nguvu zaidi ya pamoja kuliko MWAKILISHI.
  • kuhakikisha MALI asili au man-made ya Taifa, inalinufaisha Taifa kwa asilimia zisizopungua 80 (80%)
  • e.t.c

Tumechelewa sana, lakini tukianza hapa, tutaweza;
  • Kuanza kuchuja wasiofaa kutoka kwenye uongozi.
  • wananchi watakua na pakujifunza e.g hata ukiwa raisi, ukipatikana na hatia ya jinai, unaadhibiwa kama mwananchi yeyote.
  • e.t.c

Hii ni kwa kifupi sana, lakni naamini umeelewa ninachomaanisha.

Nani atachuja hao wasiofaa na vigezo gani vitatumika kama viashiria kwamba huyu anafaa au hafai?
Maana binadamu hasa wabongo kuigiza kwao ni Jambo la kawaida hasa akiwa na shida au nje ya uongozi

Kwa kweli ni Jambo gumu na zito
 
Sabato NJEMA Wakuu!

Ufanisi ni mdogo, faida ni hafifu. Mtaji ni Duni, Muda unaopotezwa ni mwingi Hali inayozorotesha uchumi wa wafanyabiashara na serikali Kwa ujumla. Hicho ndicho kinafanya kuwe na haja ya kuleta Wawekezaji katika Bandari yetu.

Uwezo wetu ni mdogo, uwezo wa kinidhamu na uadilifu WA Watu wetu bado unatia mashaka. Wizi na ufisadi umekuwa ugonjwa miongoni mwetu Kwa kipindi kirefu. Taarifa za CAG kila Mwaka zinathibitisha tunahitaji msaada sio tuu wa kimtaji Bali pia wa kiuongozi kwani uadilifu na Uzalendo kwetu imekuwa kama Bikra kwenye Wodi ya Wazazi.

Ninaweza kuungana na yeyote mwenye uadilifu na ufanisi katika kuleta Maendeleo. Watanzania badala ya kusikitika na kulalamika Kwa nini Waarabu au mataifa mengine wanapewa fursa ya kuwekeza katika Nchi yetu, tunatakiwa tuwe waadilifu na wazalendo.

Kimsingi watanzania wengi wetu sio waaminifu, sio waadilifu, wengi ni majizi. Kama huamini au utaniona ninatukana basi unaweza kuchukua Nguo yako na kumpelekea fundi nguo alafu uone nini kitatokea. Au mpe kijana Bodaboda akuletee hesabu uone kama hamtasumbuana. Au mpe fundi mwashi kazi ya ujenzi alafu usimsimamie uone nini kitatokea.
Au kwenye Msiba au harusi uone Watu wakiiba chakula, mafuta na vinywaji.

Hivyo ndivyo wengi wetu tulivyo. Tufanye namna tukoke kwenye huo mkwamo.

Haya mpe mtanzania uongozi badala ya kusaidia Ndugu zake, ataanza kujiwekea Ulinzi ili aibe vizuri. Na ukisema ukweli utaishia Kufungwa, kuingia kwenye Matatizo ikiwezekana kuuawa. Hivyo ndivyo watanzania wengi wetu tulivyo.

Kwa upande wangu sio tatizo ikiwa tutakodisha baadhi ya miradi au taasisi au mashirika ikiwa Sisi wenyewe tunashindwa kujisimamia. Lengo likiwa ni kupata faida na Kupata tija iliyokusudiwa.

Muhimu ni mikataba iwe mizuri yenye kulinda maslahi ya taifa na sio kikundi cha watu

Mgomo wa wafanyabiashara wa Kariakoo unauhusiano wowote na hiki kinachoendelea?

Sabato njema tena!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Sidhani kama kuna ambaye anakataa uwekezaji haijalishi anapewa nani ila ni vile tu wahusika wanajaribu kubadili hoja iwe anayekataliwa ni mwarabu. Hoja hapa ni vipengele vya mkataba. Mbona suala la bandari kupewa DP world linajulikana toka mwaka jana na hakukuwa na kelele mpaka sasa?
 
Sidhani kama kuna ambaye anakataa uwekezaji haijalishi anapewa nani ila ni vile tu wahusika wanajaribu kubadili hoja iwe anayekataliwa ni mwarabu. Hoja hapa ni vipengele vya mkataba. Mbona suala la bandari kupewa DP world linajulikana toka mwaka jana na hakukuwa na kelele mpaka sasa?

Kipengele gani kinautata?
Tunaweza kujadili hata hapa.
 
Kipengele gani kinautata?
Tunaweza kujadili hata hapa.
Kwanza mpaka sasa wabunge wenyewe wameniacha na maswali zaidi ya kile walichokuwa wakikijadili. Mfano Kitila mkumbo kasema ile ni MoU baina ya serikali yetu na Dubai hapa hawajadili mkataba kwa sababu hata haupo bado. Mollel yeye katoka huko anadai hakuna anayepunga mkataba wa bandari na DP isipokuwa ni mbowe tu. Na wabunge wengi wana refer kama mkataba sasa najiuliza je, hao wabunge wenyewe walikuwa wanaelewa kweli walichokuwa wanakijadili?
 
Kwanza mpaka sasa wabunge wenyewe wameniacha na maswali zaidi ya kile walichokuwa wakikijadili. Mfano Kitila mkumbo kasema ile ni MoU baina ya serikali yetu na Dubai hapa hawajadili mkataba kwa sababu hata haupo bado. Mollel yeye katoka huko anadai hakuna anayepunga mkataba wa bandari na DP isipokuwa ni mbowe tu. Na wabunge wengi wana refer kama mkataba sasa najiuliza je, hao wabunge wenyewe walikuwa wanaelewa kweli walichokuwa wanakijadili?

Wabunge wengi waliochangia ni kama walikuwa hawaelewi kama Sisi wananchi wao.

Hata Mimi bado wameniongezea utata.
Mara mkataba, mara makubaliano.
Mara kilichopelekwa bungeni ni makubaliano ambayo ni msingi WA mikataba itakayoingiwa.
Mara
Mara
Mara
Yaani maneno yanachanganyana hata haijulikani kipi ni kipi.
 
Nani atachuja hao wasiofaa na vigezo gani vitatumika kama viashiria kwamba huyu anafaa au hafai?
Maana binadamu hasa wabongo kuigiza kwao ni Jambo la kawaida hasa akiwa na shida au nje ya uongozi

Kwa kweli ni Jambo gumu na zito
Ni swali zuri sana ndugu, Na mimi kusema ninaweza kulijibu kwa mapana yote nitakuwa mu-ongo. Lakini naweza kutoa mawazo ya juu juu tu.

Usaili wa kazi
  • kuwe na Bodi za usajili sehemu usika ambazo zitapokea maombi ya kazi kwa mtandao.
  • kila ombi la kazi, litarekebishwa na mfumo wa mtandao kabla halijakia bodi husika, ili kusiwe na jina, dini, jinsia, na kabila la muombaji.
  • Washiriki wa bodi, wawe wanachaguliwa na mfumo wa mtandao kwa ajili ya usaili fulani.
  • etc
Lengo ni kuondoa upendeleo na kusisitiza ubora.

Utendaji.
  • Utendaji wa kazi uwe wa ma-lengo (targets), za siku, wiki, mwezi, mwaka
  • Ufanisi wa mfanyakazi upimwe kutokana na kiwango cha kutimiza malengo
  • mshahara wa mfanyakazi uwe ( basic + perfamance allowance)
  • upandishwaji vyeo utengemee na kiwango cha kutumiza malengo
  • etc
Matumizi
- Kuwe na viwango vya matumizi, na uidhinishwaji na wasimamizi. E.g Milioni 10 haziwezi kutumia bila idhini ya waziri, milioni 100 haziwezi kutumika bila idhini ya bodi ya wasimamizi wa fedha, bilioni 1 haiwezi kutumika bila idhini ya raisi. Hivyo, e.g, TTCL ikitumia vibaya zaidi ya Bilioni 1, Raisi, bodi, waziri -> wanapoteza sifa za kuwa na nafasi zao. Zikitumika vibaya milioni 200, Raisi atangaze kuwawajibisha bodi, waziri, na wasimamamizi. etc

Kwa Viongozi
  • Kuwe na Tume HURU na ya HAKI itakayo simamia uchaguzi
  • Kura zipigwe kwa kutumia kitambulisha cha Taifa
  • Uhesabuji wa kura uwe live, ukiwakilishwa na makaratasi

Utendaji
  • Mipango ya kitaifa ipangwe na "Tume/Wakala/etc wa Maendeleo ya Taifa",
  • Viongozi, wapime katika kutekeleza mipango hii katika muda uliowekwa
  • Viongozi watapoteza sifa ya kugombea tena uongozi iwapo watashindwa kutumiza malengo ya mipango ya kitaifa, kikanda, etc.
  • etc
 
Ni swali zuri sana ndugu, Na mimi kusema ninaweza kulijibu kwa mapana yote nitakuwa mu-ongo. Lakini naweza kutoa mawazo ya juu juu tu.

Usaili wa kazi
  • kuwe na Bodi za usajili sehemu usika ambazo zitapokea maombi ya kazi kwa mtandao.
  • kila ombi la kazi, litarekebishwa na mfumo wa mtandao kabla halijakia bodi husika, ili kusiwe na jina, dini, jinsia, na kabila la muombaji.
  • Washiriki wa bodi, wawe wanachaguliwa na mfumo wa mtandao kwa ajili ya usaili fulani.
  • etc
Lengo ni kuondoa upendeleo na kusisitiza ubora.

Utendaji.
  • Utendaji wa kazi uwe wa ma-lengo (targets), za siku, wiki, mwezi, mwaka
  • Ufanisi wa mfanyakazi upimwe kutokana na kiwango cha kutimiza malengo
  • mshahara wa mfanyakazi uwe ( basic + perfamance allowance)
  • upandishwaji vyeo utengemee na kiwango cha kutumiza malengo
  • etc
Matumizi
- Kuwe na viwango vya matumizi, na uidhinishwaji na wasimamizi. E.g Milioni 10 haziwezi kutumia bila idhini ya waziri, milioni 100 haziwezi kutumika bila idhini ya bodi ya wasimamizi wa fedha, bilioni 1 haiwezi kutumika bila idhini ya raisi. Hivyo, e.g, TTCL ikitumia vibaya zaidi ya Bilioni 1, Raisi, bodi, waziri -> wanapoteza sifa za kuwa na nafasi zao. Zikitumika vibaya milioni 200, Raisi atangaze kuwawajibisha bodi, waziri, na wasimamamizi. etc

Kwa Viongozi
  • Kuwe na Tume HURU na ya HAKI itakayo simamia uchaguzi
  • Kura zipigwe kwa kutumia kitambulisha cha Taifa
  • Uhesabuji wa kura uwe live, ukiwakilishwa na makaratasi

Utendaji
  • Mipango ya kitaifa ipangwe na "Tume/Wakala/etc wa Maendeleo ya Taifa",
  • Viongozi, wapime katika kutekeleza mipango hii katika muda uliowekwa
  • Viongozi watapoteza sifa ya kugombea tena uongozi iwapo watashindwa kutumiza malengo ya mipango ya kitaifa, kikanda, etc.
  • etc

Mawazo yako yanaweza kuwa mazuri Ila vipi waendesha hiyo mifumo wasipokuwa waadilifu?
 
Mawazo yako yanaweza kuwa mazuri Ila vipi waendesha hiyo mifumo wasipokuwa waadilifu?
Uwezekano wa kukusa uwadilifu unapungua sana iwapo, Mfumo umetengezwa kuweka mihimili inayojitegemea lakini yenye nguvu sawa na yenye wajibu wa kahakikisha mihimili mingine inaenda sawa, e.g. Kukiwa kuna mihimili miwili A na B, A inanguvu sawa na B, A wajibu wake ni kuhahikisha B inatekeleza majukumu yake, B wajibu wake ni kuhakikisha A inatekeleza wajibu wake.

Hata hivyo iwapo mihimili hiyo itashirikiana kuharibu Taifa, mfumo unatakiwa kuwapa wenye Taifa (wananchi) jukumu la mwisho la kulinda taifa lao.
 
Uwezekano wa kukusa uwadilifu unapungua sana iwapo, Mfumo umetengezwa kuweka mihimili inayojitegemea lakini yenye nguvu sawa na yenye wajibu wa kahakikisha mihimili mingine inaenda sawa, e.g. Kukiwa kuna mihimili miwili A na B, A inanguvu sawa na B, A wajibu wake ni kuhahikisha B inatekeleza majukumu yake, B wajibu wake ni kuhakikisha A inatekeleza wajibu wake.

Hata hivyo iwapo mihimili hiyo itashirikiana kuharibu Taifa, mfumo unatakiwa kuwapa wenye Taifa (wananchi) jukumu la mwisho la kulinda taifa lao.
Mihimili inaongozwa na watu. Sasa ndio swali hao Watu waongoza hiyo mihimili vipi kama Hawana maadili na uadilifu?
 
Mihimili inaongozwa na watu. Sasa ndio swali hao Watu waongoza hiyo mihimili vipi kama Hawana maadili na uadilifu?
ndio hapo inatakiwa mfumo uweze kuwachuja. Chukua mfano niliotoa wa kuhudhinisha matumizi ya pesa, ule wa mil 10, 100 etc.. Nipe mfano wa viongozi wasio waadalifu wanavyoweza kuiba pesa au kuzitumia kwa uzembe bila kushikwa na huo mfumo..
 
Back
Top Bottom