Uchaguzi 2020 Je, kuna uwezekano kutangaza nia kugombea Urais kupitia CHADEMA kwa baadhi, kunatumika kama kichaka cha kujifichia aibu ya kushindwa ubunge?.

Hivi wana CCM kwani ni lazima kila kitu kinachofanywa na Chadema lazima muumie roho? Swala la watu wengi kujitokeza kuwania urais Chadema ni la kimkakati. Nyie tulieni huko huko gizani.
 
Uwanja uwe sawa kwa vyama vya siasa na tume ya uchaguzi itende haki katika uchaguzi kwa vyama vyote. Bila shaka Mayalla unafahamu pasi na hali kipindi cha uchaguzi kuna kuwa na figisufigisu nyingi sana kwa vyama mbadala
 
Shida Paskal umeanza mwenyewe kujadili watu badala ya vitu ...umeanza kuponda wagombea kuwa hawana ubavu wa kushindana na Magufuli kwa aliyoyafanya...
Mfano Mh Rungwe kila mwaka wa uchaguz anagombea uraisi,Dovutwa,je walikuwa na uwezo wa ku-compite na akina Mh Kikwete,wale watia nia 40 ikiwemo darasa la saba hukuwaona...
Mtu kutia nia n haki yake kidemokrasia, Pascall utaramba tu uteuzi muda sio muda kila kitu na wakat wake,tumia akili yako nguvu zako zote Yesu wa Chato amekuona kuna Yuda na Petro hawajafa...wakifa utaonekana kwenye maziko na ndo siku utapewa urithi wa nguo ..
 
Katika mijitu ya hovyo Pascal Mayalla ni moja ya majitu ya hovyo yanayoibukia kutafuta kuteuliwa. Kinachomuhangaisha ni ukabila na mwendendo wa magufuli kuchagua watu kwa ukanda/ukabila. He thinks he might be next in that ctegory!
 
Pamoja na kusema upinzani legelege nimefurahi kuona umesema Tundu Na Zitto wakisimama watamtia jambajamba JPM.
Hakuna upinzani legelege maana kama ungelikuwa legelege, kwa nguvu ya polisi, CCM, mahakama, bunge, upinzani ungelikuwa umeshatoweka. Kitu legelege unatumia nguvu zote hizo? yeye ndiye legelege maana kama una nguvu ya hoja huna sababu ya kutumia jeshi, polisi, ccm, mahakama, bunge, kugawa hela barabarani, kununu wapinzani etc!
 
Kuchukua fomu za urais hakuwazui wao kugombea ubunge baadae ikiwa hawatopata ridhaa ya kuwania urais.
 
Watu badala ya kujadili mada wanamshambilia mwandishi, ukweli uchaguzi huu kile "chama kikuu cha upinzani kitapoteza majimbo yote". Je ni kweli wanaohama wamenunuliwa? Wanaficha ukweli wa mambo lakini oktoba itakuwa fedheha kubwa. Mkuu Pasikali nafikiri watakuwa wanapitia mada zako na kutafakari kwa kina lakini wameshachelewa sana
 
Huyo mwandishi ni ndugu yangu lakini kwa akili zake hizi za sasa hivi wacha wamshambulie tu! Amezidi kujikomba kwa jiwe kwa ajili ya uteyuzi!!
 
Watawala wanalazisha kukubalika kwa kutumia nyenzo za watanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…