Je, Kuna uwezekano wa Kesi ya Mbowe kuoneshwa Mubashara kwenye runinga?

Je, Kuna uwezekano wa Kesi ya Mbowe kuoneshwa Mubashara kwenye runinga?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kufuatia mahojiano ya Mtukufu Rais Samia na BBC, ameweka wazi kuwa vyombo vya habari viko na uhuru wao kamili.

Mtukufu Rais amekwenda mbele zaidi akisema kesi ya Mh. Mbowe ni nafasi nzuri kwa mahakama zetu, kuionyesha dunia kuwa haki inatendeka.

Kwa rejea mbili hizi ni wazi kuwa Mtukufu Rais na wasaidizi wake hawana tatizo na mashuhuda kufika mahakamani, ikiwamo kuonyeshwa mubashara kwenye Runinga kwa yanayojiri.

Vyombo vya habari fursa hiyo kwenye shauri hili lenye maslahi makubwa na wengi.

Kwa hakika inapendeza sana maneno yanapoambatana na vitendo ili kuweza kuivunja mifupa iliyomshinda mzee fisi hapo awali.

Wito:

IMG_20210811_155142_046.jpg

Vyombo vya habari ni huru, tulitumie dirisha hili kikamilifu.
 
... itakuwa jambo bora kabisa kuwahi kutokea katika medani za kimahakama nchini! Jaji Mkuu na timu yake (mhimili unaojitegemea) wafanyie kazi hili suala ili kesi ya Mbowe irushwe mubashara ugaidi wake uwekwe hadharani!

Hii ni fursa kwa pande zote:

1. Kuonyesha wanahabari wako huru
2. Kuweka uhalali kwenye kauli zote za Mtukufu Rais kuwa hakuwa mwongo
3. Kuondoa tashwishi za kubambikiziana kesi kwenye shauri hili.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Kwanini kuwajibia?

Mwenyekiti wao kathibitisha uhuru kamili kwa wanahabari.

Mungu atupe nini?
... Salim Kikeke angekuwa makini, hii ilitakiwa iwe follow-up question kwa Rais! "Vyombo vya habari sasa viko huru kurusha kesi za namna hii live kama ambavyo imekuwa ikifanyika nchi nyingine kwa kesi zenye maslahi na mvuto mkubwa kwa jamii"? Another golden chance was lost!
 
Sidhani kama ni ruksa kama anavyoongea. Ila sijui labda online tv's
 
Bado nina deni na wale wa ANAUPIGA MWINGI ndipo mambo mengine yatafuata.
 
... Salim Kikeke angekuwa makini, hii ilitakiwa iwe follow-up question kwa Rais! "Vyombo vya habari sasa viko huru kurusha kesi za namna hii live kama ambavyo imekuwa ikifanyika nchi nyingine kwa kesi zenye maslahi na mvuto mkubwa kwa jamii"? Another golden chance was lost!

No chance lost. Kauli za Mtukufu Rais dunia imezisikia.

Let's not lose this opportunity to put all her commitments to test. One after the other.
 
Sidhani kama ni ruksa kama anavyoongea. Ila sijui labda online tv's

Kwanini kujifungia milango wakuu?

Uhuru kamili wa vyombo vya habari maana yake inajulikana.

Pia kasema ana ngozi ngumu akimaanisha ni mvumilivu mno.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Hata shetani huogopa kuaibika, yale mazungumzo yalikuwa ya kufurahisha genge tu.
 
Kwanini kujifungia milango wakuu?

Uhuru kamili wa vyombo vya habari maana yake inajulikana.

Pia kasema ana ngozi ngumu akimaanisha ni mvumilivu mno.

Au nasema uongo ndugu zangu?
Tusiandikie mate ingali wino upo, huyu mama anaongea vile tu kuridhisha wafadhili. Hamaanishi wala nini.....

Kwani vingapi huwa anabwabwaja na havina uhalisia/ havitendewi kazi??
 
Samia -ruksa
Sirro- sogeeni kisutu mpigwe
Wanajuana.

Hawa ni wa kuwapa notice kama yeyote tu kuwa kuanzia sasa shauri la kesi hii kuanzia na lijalo litakuwa live.

Suala la kuwa live ni suala la mahakama na wana habari. Halina cha kufanya na Sirro wala Mtukufu Rais.

Shida gani wakuu?
 
Back
Top Bottom