Je kwa Uzembe huu wa madaktari ulivosabababisha kumpoteza mdogo wangu,nilikosea kuwaacha ningechukua hatua??,(ukweli)

Je kwa Uzembe huu wa madaktari ulivosabababisha kumpoteza mdogo wangu,nilikosea kuwaacha ningechukua hatua??,(ukweli)

EP3
NAENDELEA

Baada ya madaktari hao wa aic kukataa kumpokea sababu hawana mashine ya xray,nililazimika kuelekea hospitali kubwa,ya government,basi nilimfikisha mpaka mapokezi ,madaktari walimpokea niliwaeleza kuwa mtoto huyu ana matatizo ya sickle cell na uwa anapata upungufu wa damu mara kwa mara ,ambapo wagonjwa wa aina hii wao madaktari uwatambua kama sicle (sikla). ,lakin awakuanza kumpa huduma kwa kusema kuwa daktari anayesimamia maswala ya xray,nae anamuhuguza baba yake mzazi,kuwa nae yuko mahututi mpaka amalize ,kwaiyo awawezi kumuhudumia wakiwa awajui ukubwa wa tatizo lake,basi alifungwa boksi katika mguu wake hili kuuweka katika hali yake,
Tulikaa tukimsubiri daktari uyo wa xray mpka kama muda wa saa 3 usiku ndio alipomaliza kuhudumia baba yake ,alikuja tukamkalisha mdogo wangu katika kit cha wagonjwa,na kuelekea chumba cha xray,basi alipigwa xray na kukuta mifupa yake.yote miwili ya mguu imevunjika kilichoshikilia ni nyama na ngozi,basi daktari uyo aliandikisha ripoti hile na mimi na mdogo wangu tulielekea wodi ya wagonjwa mahututi,basi tulifika katika wodi hile na kumlaza katika kitanda kilichokuwa kalibu na dilisha la sehem ya kukaa,(kupumzika ) wanaouguza wagonjwa,basi baba alikuwa ameshaletwa taarifa na ilipofika muda wa saa 3 na ,mzee alifika hospitalin na kutujulia hali.
Nilimweleza hali yote uliompata mwanae ,alisikitika sana basi alituaga na kuniachia kiasi cha pesa kwa ajili ya dharula kama ikitokea yeye anaelekea nyumbn na kesho asubuhi atawah kuja
Tuliagana akaondoka ,nilibaki na mdogo wangu mle wodini uku kukiwa na wagonjwa wengine 4,mmoja wa ajali,na wawili wamevunjika ,mmoja amevunjika paja kwa kuangukiwa. Na jiwe na mwingn amevunjika kwa ajali na mmoja amevunjika mbavu,basi daktari alimpa sawa zingn tena na akasema kesho.atafungwa PoP(mhuogo) ,basi usiku hule sikulala nilikuwa nikimuuliza kama anajisikia chochote mguuni lakini jibu lake alisema hapana ,sissiikii chochote,ata ukiushika hakuna ninachosikia,basi nilijisikia vibaya na kupatwa na uzuni ,nilitoka pembeni kidogo nililia sana ,basi nilijokaza nikaludi ndani nikiwa najifanya nafuraha nikimchekesha na kumpa moyo kumwambia atakuwa sawa ata asijali atapona,
Basi usiku ule sikupata usingizi nilikesha namwangalia. Yeye alibaatika kupata usingizi alilala,
Nashukuru Mungu asubuh kukakucha na nilipoamka nilienda nikanunua kadishi madogo Tsh 500 hili awe anatumia kunawia ,nilinunua na chakula ,nakumbuka nilinunua wali na maharage,muhogo wa kupika,vitumbua 5,na chapati na chai ,kutoka canteen ya mle hospitali,nolimpelekea hili anyww

TUTAENDELEA
SOON..….….
 
EP 4
INAENDELEA
Basi nilinunua vyakula hivyo na kumpelekea,nilimhamsha nikampa alikula kidogo tu na kukataa akisema asikii hamu ya kula,
Basi nilitunza chakula kilichobaki tutakula baadae, basi ilipo fika saa 4 mzee wetu alikuja na kumjulia hali mwanae,
Alikaa kwa muda kabla ajatuaga na kuelekea nyumbn,basi siku hiyo madaktari wa zamu ya mchana uo walikuwa wengine tofauti na wale waliotupokea na kuandika ripoti ya mdogo wangu,
Walifika na kukagua wagonjwa wote, basi waliniambia wanajiandaa kuja kumfungia PoP mdogo wangu,
Basi tulikaa kuwasibil mpaka midaa ya saa 6, niliwafata tena na kuwaambia wakammalizie mdogo wangu kumfunga PoP (muhogo) ,maana madrip ya maji ya yaliochanganywa na dawa walikuwa wamemuongezea drip4,
Basi waliniambia wanakuja,baada ya dakika kama 15 walikuja na kumfungia muhogo na kukamilisha matibabu yake,nilielekea sehemu ya kupumzika kukaa,ilipokaribia saa 7 mchana basi nilielekea kwa mdogo wangu kwa ajili ya kumpa chakula ambacho mzee alikuwa ametuletea hile saa 4 ,nilipofika nilimkuta amelala usingizi mzito,nilimhamsha aliamka uku akiwa na usingizi mzito ,nilimwambia amka tule chakula , lakini alikataa akasema (akinitaja jina ) niache nilale kwanza na usingizi mzito nikiamka nitakula) basi nilimuacha akaendelea kulala mimi nilienda kukaa katika mabenchi ya kupumzika wahuguzaji,
Nilikaa mpaka saa 8 niliamka tena na kwenda kumhamsha hili Hale chakula, nilimkuta vilevile akiwa katika usingizi mkubwa,nilimhamsha tena, ahamke tule, lakini alipo amka jibu lake lilikuwa lile lile ,we niache nilale kwanza na usingizi mzito nikiamka nitakula, basi nilimuacha tena kwa mara ya pili, nilirudi kukaa palepale,nilikaa hilipofika saa 9 kwa vile nilipokuwa nimekaa kulikuwa kunapakana na dirisha ambapo kitanda chake kipo , nilianza kusikia kama sauti ya mtu akiguna,mh,mh,mh, (kukema, yaani mfano ukiwa kama umebanwa na kitu kwenye kifua na kupelekea kupumua kwa shida) mwanzo sikutilia maanani sauti hiyo ya kuguna na sikutambua ni nini,ziliendelea kwa muda mpaka akili yangu iliposhtuka kwamba sauti zile zinatoka wodini kwangu, basi nilitoka
Nikaenda moja kwa moja katika kitanda chake , kwakweli nilichokikuta kilinishangaza sana ,na nilijiuliza inawezekanaje,nilimkuta mdogo wangu kapiga magoti ,uku akiwa kama anasujudu,nilishangaa sababu mguu wake hule alikuwa awez ata kuunyanyua wala kusogeza,ukiachilia hilo pia alikuwa amelala chali sasa kitendo cha kujigeuza kilinishangaza kwa sekunde kadhaa, basi kengere ya hatari hilipiga akilini mwangu moja kwa moja nililudi kwa kasi katika chumba cha madaktari na kuwakuta wale madaktari waliomhudumia wakiendelea na shughuli nyingine,niliwaambia daktari twendeni haraka mdogo wangu amezidiwa,
NITAENDELEA
SOON...,.....
 
FINAL EP
INAENDELEA
Basi baada ya kuwaambia madaktari waje mdogo wangu nahisi kazidiwa kutokana na mabadiliko ya kutoka kulala chali adi kupiga magoti kitandani,basi nilitoka haraka kurudi wodini hile nafika tu daktari mmoja akawa ameshafika nae nyuma yangu,nakumbuka uyo daktari alikuwa anaitwa dr baraka, basi tulimrudisha kulala chali .
Lakini nilikumbuka kitu kimoja ambacho toka hile jana yake tumeingia mpaka leo hii saa 10 jion akupewa ,na uwaga akipata shida kidogo tu utokea ni damu,nilikumbuka damu huwa inamhishia mara kwa mara sasa nikahisi itakuwa damu imepungua ndio maana kwanza kupata hali tofauti,
Basi nilimwambia yule dr baraka kuwa mbona damu ajaongezwa na niliandikisha kwenye ripoti kuwa ana matatizo ya sickle cell,na upungufu wa damu,basi daktari alikimbilia kipimo cha damu na kupima
,Na kweli walikuta damu imepungua imebaki point 5na sehemu ambayo ilikuwa ndogo sana,
Basi nilimlalamikia yule daktari kwa kuchelewa kumpima damu wakati niliandikisha kwenye ripoti ya yule daktari alietupokea jana yake na nae alimpima na kuacha ripoti kuwa damu yake ni ndogo ,
Yule dr baraka aliniandikia haraka vifaa vya kwenda kuchukua kwenye duka la mle hosptal ambalo lilikuwa liko pembeni ya hospitali japo utoki kabisa nje Uzio wa hospitali hile,basi aliniandikia mipira ya kutundikia damu,na damu fulani hivi nomezisahau ,pamoja na gloves,nilitoka haraka kuelekea kufata vifaa hivo hili mdogo wangu awekewe damu,nyuma yangu dr nae alitoka kuelekea ofisini kwao,
Bado ilikuwa ni kama majira ya saa 10,jioni
nilitoka nje ya wodini na kwenda kuchukua hivo vifaa haraka ,nilipokuwa narudi nilipofika katika dirisha lile alipolala nilimhangalia kupitia hapo dilishani,
kiukweli nilishangaa tena kwa mara ya pili kwa halivokuwa amebadili tena staili ya kukaa ,nilimhshudia akiwa amelala chali kama tulivyokuwa tumemlaza ,cha ajabu miguu yote miwili kainyanyua juu,(yan ulale ukiangalia paa la nyumba afu miguu uinyanyue juu) nilipigwa na butwaa ,mapigo ya moyo yakienda kasi nilishindwa kuamini inawezekanaje tena kwa mara ya pili,akae mkao ambao kutokana na mguu ulivovunjika na pia hauna nguvu ,na ata kuusogeza popote wala yeye kujisogeza hilikuwa ngumu, sasa iwezekane kwa kunyanyua miguu yote juu ,wakati mmoja ni mbovu( ebu ww jifikilie kidogo ata kama ni wewe hauta shangaa??)basi nilivoona kitendo hicho sikutaka ata kuchelewaa nilipitiliza mpaka chumba cha madaktari na kumtahadharisha de baraka kwa hali niliomuona nayo mdogo wangu
baada ya kumwambia aje haraka nilitoka spidi mpaka wodini kwa mdogo wangu,nilimkuta akiwa vilevile basi nilimshusha hile miguu lakini nilipooshusha
alitaka kama kunyanyuka ,nilimshika kwenye kifua nikimuita jina lake nikimwambia lala usikae hivo lakini
mara niliona akitaka kunyanyuka tena nilipomwangalia usoni niliona ametoa macho kama analazimisha kutapika lakini sio kutapika ,uku macho akiyatoa akilazimisha kusimama
mara yule dr baraka alifika alimwekea kipimo cha mapigo ya moyo,lakini niliona kama uyu mtoto anapumua kwa shida ,nilianza kumpampu kifua kurudisha mapigo ya moyo,yule dr baraka nae akajiunga na mim tukawa tunampampu,basi aliingia harakatena de mwingn aliemuhudumia na dr baraka wakati wa kumfunga PoP ,akiwa na vifaa vya kusaidia kupumua,basi nilimhangalia kiukweli matumaini yalikataa nilianza kuliakulia, madaktari waliniambia nitoke njee basi nilitoka ,nikaenda kukaa kwenye benchi za kupumzikia,niliona wakisogeza yale mashuka kuzunguka kitanda na wakaendelea kumhudumia ,lakini kwa nilivomuacha nilikosa kabisa matumaini ya kumpata hai mdogo wangu,
Baada ya muda nilishuhudia wakimfunika hadi kichwa chote na mashuka meupe ,kumbe kaisha kata kauli ,nilianza kuisi uchungu mkubwa moyoni mwangu nilijikaza nisilie ,basi wale madaktari walitoka nje na kuelekea ofis nyingn,ndipo nilipata wasaa wa kuingia kuona nini kimeendelea,kiukweli nilimfunua na kukuta kaisha fariki,nalihinama nikalia sana ,basi nami nilimfunika na kutoka kukaa pale nje ya wodini watu wakiwa awaamin kama mtoto yule kafariki,nilipojipa moyo nilichukua CM yangu na mtu wa kwanza kumpigia halikuwa ni kaka yetu mkubwa aliekuwa Arusha kipindi hicho,nilipompogia nilisalimiqna nae tu afu nikamuuliza Upo kazin akasema hee nipo kazini basi sikutaka kumwambia akiwa kazini ,nilimwambia tu basi poa nitakupigia jioni ukitoka kazini,baada ya kama dk 5 ,nilimuona baba akiwa amekuja na chakula kwa ajili ya sisi kula usiku hule maana sahiyo hilikuwa inaelekea saa 11,alipofika alinikuta nimekaa nje ya wodi uku na majonzi ,kaniuliza mmnaendeleaje kuna nn,nilimwambia tu mdogo wangu (nikimtaja jina) amefariki ,kiukweli mzee alipigwa na butwaa maana akutegemea kuwa hivyo na ukijumlisha asubuh alimhacha marehemu akiwa sawa aoneshi dalili za kujakuzidiwa baadae.
Basi mtu wa mochwali alikuja na tukaupakia mwili kwenye kitanda cha kubebea maiti,nilitoka mpaka ofisini kwa wale madaktari nikiwa na uchungu,niliwakuta wakiwa wamekaa wanajadiliana kuhusu kifo cha mtoto huyu (mdogo wangu) nilipofika nikawakuta na nessi aliekuwa zamu ,nilianza kuoji inakuwaje daktari alietupokea tuliandikisha ripoti kwake na nikaandika kila kitu kuwa uyu mtoto anamatatizo ya sickle cell na upungufu wa damu,na alipopima alimkuta kweli ana upungufu wa damu hivo kumaanisha alitakiwa kuwekewa drip za damu usiku hule tumefika au asubuh sababu nyingi mliofata zamu lazima mpokee ripoti za wagonjwa wote,madaktari wale walianza kujitoa kila mmoja kivyake ,wakwanza alianza kusema hapana ripoti awakupewa hivyo walishindwa kujua ,nilikawauliza kama amkupewa hile saa 6wakati mnamfunga PoP niliwaambia ana matatizo aya na aya kwann msingepima tena hili kupata uhakika ,yule dr baraka alilukia et wao ni wageni pale hospitali kwaiyo vitu vingi vya pale hospitali awvijui vizuri,basi nilisema tambueni hapa tunaongea kuhusu kupoteza uhai wa mtu,mara yule nessi akanijibu"kwan uhai wa mtu ni nini?"jibu lile lilinivuluga kabisa ,nikamuuliza "uhai wa mtu ni nn,kwaiyo www haujali kuwa kilichotokea maana ni uzembe wenu uliosababisha kupoteza maisha ya mdogo wangu,ujui wajibu wako wew kama nesi kufariki kwa mtu mbele yenu unaona sawa ,ushtuki,nikamwambia sasa hivi ni kesi mimi na wewe kwa kusababisha kifo ,maana wew ndio ulikuw nesi unaudumia wodi yetu lilikuwa jukumu lako kutambua,basi yule nessi alikaa kimya , ndpo yule dr baraka aliposema ". Walipompima damu aliokutwa nayo hapo hospitalini ilikuwa imeisha kwaiyo walikuwa wameagiza inakuja kutoka hospitali nyingine ya mkoa jirani (kubwa sana ya serikali)" baada ya utetezi wa dr baraka,niliwauliza kama ni damu ilikuwa imeagizwa mbona mlisema amkupata ripoti kujua kama anaitajika kuongezwa damu,pia mkoa wangu na mkoa damu ilipoagizwa ni jirani ,kwa usafiri wa kawaida ni masaa 3-4 ,hila kutokana na kuwa ni ambulance.mngetumia masaa2-3 kwaiyo kama ni toka saa 4 mpk saa 6damu ingekuwa tayari hilishafika "niliwaambia kabisa hii naenda kuwafungulia kesi,
Baada ya kuona nimewabana na wanapishana pishana kujitetea,dr baraka alinikuta pembeni,akaanza kunibembeleza niachane tu na ayo maswala uku akiniomba msamaha kwa yote uku akikili ni uzembe basi kwa kumheshimu maana alituhudumia kwa kadiri ya uwezo wake nilimwambia sawa nimekueshim sana ,lakini isingekuwa wew pengine tungekutana mahakamani,basi nilitoka na kukuta baba na ndugu wakiwa wameshafika tulikabidhi mwili na kuondoka kwenda nyumbani kuanza msiba,

,NDUGU WANAJAMVI NIMESHEA STORY HII YA KWELI HILIONIPATA MIAKA MICHACHE ILIYOPITA, KUTOA USHAURI KWA WAZAZI NDUGU NA JAMAA,AMBAO PENGINE WANAO WATOTO WENYE SICLE (SICKLE CELL)WAWAANGALIE WASIPENDE KUWAFANYA WAPATE MAUMIVU AU SHIDA KAZIKA MIILI YAO,PILI TUNAPOPELEKA WAGONJWA WOWOTE HOSPITALINI TUJITAHIDI HUDUMA ZOTE STAHIKI ANAPEWA MGONJWA,,PIA KUWAEPUSHA WATOTO WETU NA HATARI ZA KIMWILI

ASANTENI SANA MLIOSHILIKI NAMI MPAKA MWISHO.
unaweza kuuliza chochote na kushauli kuhusiana na hi story yangu.

..................MWISHO.........................
 
FINAL EP
INAENDELEA
Basi baada ya kuwaambia madaktari waje mdogo wangu nahisi kazidiwa kutokana na mabadiliko ya kutoka kulala chali adi kupiga magoti kitandani,basi nilitoka haraka kurudi wodini hile nafika tu daktari mmoja akawa ameshafika nae nyuma yangu,nakumbuka uyo daktari alikuwa anaitwa dr baraka, basi tulimrudisha kulala chali .
Lakini nilikumbuka kitu kimoja ambacho toka hile jana yake tumeingia mpaka leo hii saa 10 jion akupewa ,na uwaga akipata shida kidogo tu utokea ni damu,nilikumbuka damu huwa inamhishia mara kwa mara sasa nikahisi itakuwa damu imepungua ndio maana kwanza kupata hali tofauti,
Basi nilimwambia yule dr baraka kuwa mbona damu ajaongezwa na niliandikisha kwenye ripoti kuwa ana matatizo ya sickle cell,na upungufu wa damu,basi daktari alikimbilia kipimo cha damu na kupima
,Na kweli walikuta damu imepungua imebaki point 5na sehemu ambayo ilikuwa ndogo sana,
Basi nilimlalamikia yule daktari kwa kuchelewa kumpima damu wakati niliandikisha kwenye ripoti ya yule daktari alietupokea jana yake na nae alimpima na kuacha ripoti kuwa damu yake ni ndogo ,
Yule dr baraka aliniandikia haraka vifaa vya kwenda kuchukua kwenye duka la mle hosptal ambalo lilikuwa liko pembeni ya hospitali japo utoki kabisa nje Uzio wa hospitali hile,basi aliniandikia mipira ya kutundikia damu,na damu fulani hivi nomezisahau ,pamoja na gloves,nilitoka haraka kuelekea kufata vifaa hivo hili mdogo wangu awekewe damu,nyuma yangu dr nae alitoka kuelekea ofisini kwao,
Bado ilikuwa ni kama majira ya saa 10,jioni
nilitoka nje ya wodini na kwenda kuchukua hivo vifaa haraka ,nilipokuwa narudi nilipofika katika dirisha lile alipolala nilimhangalia kupitia hapo dilishani,
kiukweli nilishangaa tena kwa mara ya pili kwa halivokuwa amebadili tena staili ya kukaa ,nilimhshudia akiwa amelala chali kama tulivyokuwa tumemlaza ,cha ajabu miguu yote miwili kainyanyua juu,(yan ulale ukiangalia paa la nyumba afu miguu uinyanyue juu) nilipigwa na butwaa ,mapigo ya moyo yakienda kasi nilishindwa kuamini inawezekanaje tena kwa mara ya pili,akae mkao ambao kutokana na mguu ulivovunjika na pia hauna nguvu ,na ata kuusogeza popote wala yeye kujisogeza hilikuwa ngumu, sasa iwezekane kwa kunyanyua miguu yote juu ,wakati mmoja ni mbovu( ebu ww jifikilie kidogo ata kama ni wewe hauta shangaa??)basi nilivoona kitendo hicho sikutaka ata kuchelewaa nilipitiliza mpaka chumba cha madaktari na kumtahadharisha de baraka kwa hali niliomuona nayo mdogo wangu
baada ya kumwambia aje haraka nilitoka spidi mpaka wodini kwa mdogo wangu,nilimkuta akiwa vilevile basi nilimshusha hile miguu lakini nilipooshusha
alitaka kama kunyanyuka ,nilimshika kwenye kifua nikimuita jina lake nikimwambia lala usikae hivo lakini
mara niliona akitaka kunyanyuka tena nilipomwangalia usoni niliona ametoa macho kama analazimisha kutapika lakini sio kutapika ,uku macho akiyatoa akilazimisha kusimama
mara yule dr baraka alifika alimwekea kipimo cha mapigo ya moyo,lakini niliona kama uyu mtoto anapumua kwa shida ,nilianza kumpampu kifua kurudisha mapigo ya moyo,yule dr baraka nae akajiunga na mim tukawa tunampampu,basi aliingia harakatena de mwingn aliemuhudumia na dr baraka wakati wa kumfunga PoP ,akiwa na vifaa vya kusaidia kupumua,basi nilimhangalia kiukweli matumaini yalikataa nilianza kuliakulia, madaktari waliniambia nitoke njee basi nilitoka ,nikaenda kukaa kwenye benchi za kupumzikia,niliona wakisogeza yale mashuka kuzunguka kitanda na wakaendelea kumhudumia ,lakini kwa nilivomuacha nilikosa kabisa matumaini ya kumpata hai mdogo wangu,
Baada ya muda nilishuhudia wakimfunika hadi kichwa chote na mashuka meupe ,kumbe kaisha kata kauli ,nilianza kuisi uchungu mkubwa moyoni mwangu nilijikaza nisilie ,basi wale madaktari walitoka nje na kuelekea ofis nyingn,ndipo nilipata wasaa wa kuingia kuona nini kimeendelea,kiukweli nilimfunua na kukuta kaisha fariki,nalihinama nikalia sana ,basi nami nilimfunika na kutoka kukaa pale nje ya wodini watu wakiwa awaamin kama mtoto yule kafariki,nilipojipa moyo nilichukua CM yangu na mtu wa kwanza kumpigia halikuwa ni kaka yetu mkubwa aliekuwa Arusha kipindi hicho,nilipompogia nilisalimiqna nae tu afu nikamuuliza Upo kazin akasema hee nipo kazini basi sikutaka kumwambia akiwa kazini ,nilimwambia tu basi poa nitakupigia jioni ukitoka kazini,baada ya kama dk 5 ,nilimuona baba akiwa amekuja na chakula kwa ajili ya sisi kula usiku hule maana sahiyo hilikuwa inaelekea saa 11,alipofika alinikuta nimekaa nje ya wodi uku na majonzi ,kaniuliza mmnaendeleaje kuna nn,nilimwambia tu mdogo wangu (nikimtaja jina) amefariki ,kiukweli mzee alipigwa na butwaa maana akutegemea kuwa hivyo na ukijumlisha asubuh alimhacha marehemu akiwa sawa aoneshi dalili za kujakuzidiwa baadae.
Basi mtu wa mochwali alikuja na tukaupakia mwili kwenye kitanda cha kubebea maiti,nilitoka mpaka ofisini kwa wale madaktari nikiwa na uchungu,niliwakuta wakiwa wamekaa wanajadiliana kuhusu kifo cha mtoto huyu (mdogo wangu) nilipofika nikawakuta na nessi aliekuwa zamu ,nilianza kuoji inakuwaje daktari alietupokea tuliandikisha ripoti kwake na nikaandika kila kitu kuwa uyu mtoto anamatatizo ya sickle cell na upungufu wa damu,na alipopima alimkuta kweli ana upungufu wa damu hivo kumaanisha alitakiwa kuwekewa drip za damu usiku hule tumefika au asubuh sababu nyingi mliofata zamu lazima mpokee ripoti za wagonjwa wote,madaktari wale walianza kujitoa kila mmoja kivyake ,wakwanza alianza kusema hapana ripoti awakupewa hivyo walishindwa kujua ,nilikawauliza kama amkupewa hile saa 6wakati mnamfunga PoP niliwaambia ana matatizo aya na aya kwann msingepima tena hili kupata uhakika ,yule dr baraka alilukia et wao ni wageni pale hospitali kwaiyo vitu vingi vya pale hospitali awvijui vizuri,basi nilisema tambueni hapa tunaongea kuhusu kupoteza uhai wa mtu,mara yule nessi akanijibu"kwan uhai wa mtu ni nini?"jibu lile lilinivuluga kabisa ,nikamuuliza "uhai wa mtu ni nn,kwaiyo www haujali kuwa kilichotokea maana ni uzembe wenu uliosababisha kupoteza maisha ya mdogo wangu,ujui wajibu wako wew kama nesi kufariki kwa mtu mbele yenu unaona sawa ,ushtuki,nikamwambia sasa hivi ni kesi mimi na wewe kwa kusababisha kifo ,maana wew ndio ulikuw nesi unaudumia wodi yetu lilikuwa jukumu lako kutambua,basi yule nessi alikaa kimya , ndpo yule dr baraka aliposema ". Walipompima damu aliokutwa nayo hapo hospitalini ilikuwa imeisha kwaiyo walikuwa wameagiza inakuja kutoka hospitali nyingine ya mkoa jirani (kubwa sana ya serikali)" baada ya utetezi wa dr baraka,niliwauliza kama ni damu ilikuwa imeagizwa mbona mlisema amkupata ripoti kujua kama anaitajika kuongezwa damu,pia mkoa wangu na mkoa damu ilipoagizwa ni jirani ,kwa usafiri wa kawaida ni masaa 3-4 ,hila kutokana na kuwa ni ambulance.mngetumia masaa2-3 kwaiyo kama ni toka saa 4 mpk saa 6damu ingekuwa tayari hilishafika "niliwaambia kabisa hii naenda kuwafungulia kesi,
Baada ya kuona nimewabana na wanapishana pishana kujitetea,dr baraka alinikuta pembeni,akaanza kunibembeleza niachane tu na ayo maswala uku akiniomba msamaha kwa yote uku akikili ni uzembe basi kwa kumheshimu maana alituhudumia kwa kadiri ya uwezo wake nilimwambia sawa nimekueshim sana ,lakini isingekuwa wew pengine tungekutana mahakamani,basi nilitoka na kukuta baba na ndugu wakiwa wameshafika tulikabidhi mwili na kuondoka kwenda nyumbani kuanza msiba,

,NDUGU WANAJAMVI NIMESHEA STORY HII YA KWELI HILIONIPATA MIAKA MICHACHE ILIYOPITA, KUTOA USHAURI KWA WAZAZI NDUGU NA JAMAA,AMBAO PENGINE WANAO WATOTO WENYE SICLE (SICKLE CELL)WAWAANGALIE WASIPENDE KUWAFANYA WAPATE MAUMIVU AU SHIDA KAZIKA MIILI YAO,PILI TUNAPOPELEKA WAGONJWA WOWOTE HOSPITALINI TUJITAHIDI HUDUMA ZOTE STAHIKI ANAPEWA MGONJWA,,PIA KUWAEPUSHA WATOTO WETU NA HATARI ZA KIMWILI

ASANTENI SANA MLIOSHILIKI NAMI MPAKA MWISHO.
unaweza kuuliza chochote na kushauli kuhusiana na hi story yangu.

..................MWISHO.........................
Pole sana
 
Back
Top Bottom