Je, makampuni ya simu yamepunguza Mb/sec?

Je, makampuni ya simu yamepunguza Mb/sec?

Naomba anayefahamu atueleze, kuna kitu gani kinachoendelea katika hii mitandao ya simu kwa sababu inaonekana ni wizi wa dhahiri kabisa.

Kwa mfano, kwa sasa ukinunua GB moja ambayo ni sawa na MB 1,000 na kama hutumii kwa kupakua ila kwa ku-browse tu pale ambapo ulikuwa ukitumia kwa takriban siku 5 sasa utatumia kwa siku moja na nusu tu na sio zaidi ya hapo na huu mchezo umeanza kama siku mbili tu zilizopita..!!!!

Je haya makampuni hasa Airtel na Vodacom ambazo ndizo ninazitumia zaidi wanaweza wakatueleza kuna nini hapa kabla hatujafuatilia TCRA???? Maanake ni wazi kabisa kwamba huu ni wizi wa wazi kabisa.
Airtel wezi,sinunui Tena mb,yaani GB 1 kusoma jamiiforums kwa siku inaisha!?..nazima data nikiwa na mb 150,kesho asubuhi meseji inakuja mb zimeisha wakati sijawasha data
 
Sasa hivi tuko 4G na 5G, wewe bado uko 3G, spidi ni kubwa na bando inalika hivyohivyo.

Halafu, huku ndio kuna mapato ya kodi, si mmelimbia mashamba ya kahawa, pamba, na katani mmehamia kwenye mitandao, serikali ipo mlipo.

Ukitumia muda mwingi kumuangalia mwijaku, lazima tozo iwe kubwa, unaangalia wema sepetu anajibinua, tozo
Mkuu una shombo sAna
 
Nahisi wanatupa mfano 1GB kama kiini macho sahihi ni 250MB....

Bundle linakula hela zangu kuliko ngozi yangu.
Kinachotokea kwenye suala la bando ni wizi ulikubuhu na uliobarikiwa.
Viongozi wanafurahi kwasababu wanapunguza watu wanaokosoa serikali mtandaoni
 
Hapana na hakuna wizi wa aina yoyote ile. jaribu kufanya utafiti utagundua kuwa speed imeongezeka sana ya mtandao kwa sasa. Mfano mimi ambaye ni mtumiaji wa VODACOM kuna maeneo ambayo nilikuwa nahangaika sana juu ya kasi ndogo ya mtandao lakini siku hizi speed Ni kubwa nikiwa mahali popote pale hadi mashambani Vodacom inachapa kazi kwa kwenda mbele .hata kuwe na mvua au baridi au jua kali au vumbi Vodacom ni kazi kazi tu.hata uwe mlimani au mteremkoni au vichakani au mbugani Vodacom inakasi ileile kukupa raha ya kufurahi unachotaka kukipata mtandaoni
Jaza vocha ya 500 au 1000. Ukishaona salio, toa laini kwenye simu yako. Weka pembeni.
kaa siku 1 yaani masaa 24 kisha weka laini yako kwenye simu.
Angalia salio, ukikuta salio liko vile vile, kanunue soda unywe😁😁😁😁
Hayo makampuni ni wezi
 
MAKAMPUNI YA SIMU YANATUIBIA …SIMU ZIMEKUA NA NETOWORK MBOVU SANA NA PIA INTERNET IKO CHINI ……KUNA RADIO ILIKUA INASEMA ASUBUHI KUTOKANA NA KUKATIKA KATIKA UMEME MINARA MINGI HAIFANYI KAZI ….NA PIA KUNA CHANGAMOTO YA GENERETA ZA MINARA KUIBIWA MAFUTA NA BETRI PAMOJA NA BAJETI YA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU KUSHUKA KUTOKANA NA USHINDANI MKUBWA
 
Back
Top Bottom