Je,matatizo ya la elimu nchini yatatatuliwa kwa kuchunguza tu matokeo ya kidato cha 4 ?

Mkulia

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2012
Posts
375
Reaction score
95

Binafsi huwa napata sana shida kubaini uwezo wa hawa watawala wetu kifikra katika kutatua matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii yetu. Kwa hivi sasa taifa letu limekumbwa na tatizo kubwa la anguko la elimu katika ngazi zote yaani elimu ya msingi,sekondari na hata elimu ya juu. Serikali kwa uzuzu au sijui kwasababu ipi inaamini kuwa kuchunguza tu ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha IV mwaka 2012 ndio mwarobaini wa tatizo hili. Hivi ni kweli kuwa tunaweza kutatua tatizo letu la elimu kwa njia hii pekee?
 

sasa,ndg,wakitoa elim nzuri,mazuzu siyata amka na kupata ufaam,kwamba nchi inaliwa,alafu elf 2000,2000, za magamba watampa nani,asiye na helim ukimwambia 2+2=10,watasema ndiooooo,kofia kanga na tisheti,sukari,na kubebwa kwenye malori,nani atakubali,,,,,,,,,,izi,,,,ndio,,,sera,,,,za,,,ccm,,,,wajinga,,,,ndio,,,waliwao,,,,,,umeni,,,,,,soma,,,,mkuu,,,,,,
 
Mh. Raisi anasubiri matokeo ya tume ili kuhakikisha kucfeli hakujirudii. Sitarajii mafanikio ya haraka katika ufaulu, labda wanafu nzi wapewe alama, ikiwa kama wanaokwenda sekondari tayari walikuwa wamafeli mtihani wa darasa la saba.
 
Binafsi huwa napata sana shida juu ya uwezo wa kifikra wa watawala wetu katika kutatua matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii yetu. Kwa miaka ya hivi karibuni kumekuwa na mdororo wa elimu katika nchi yetu ambao kwa hakika umeukumba ngazi zote za elimu yaani msingi,sekondari na hata elimu ya juu. Serikali yetu badala ya kuunda tume kuchunguza mdororo wa elimu nchini kwa ujumla wake wao wanachunguza matokeo mabaya ya kidato cha IV 2012 kana kwamba ndio tiba hasa ya anguko la elimu hapa Tanzania. Kwa mtazamo wangu naona wanakosea kuchunguza tu matokeo mabaya ya kidato cha IV badala ya kuchunguza anguko/mdororo wa elimu nchini kwa ujumla wake. SIJUI
 
Sinahakika kama majibu ya tume yatasaidia, kwasababu hao wanaotakiwa kutoa matokeo bora wengi wao wanafundisha kwa amri yamahakama. Nitashangaa kama CWT watajumuika katika tume ambayo imeundwa na chombo ambacho hawakua namuafaka nacho. Nadhani mdororo wa Elimu ndio kiini, je Serkali inataka kutuambia sera za PEDP na SEDP hawakujua zita adhiri kwa kiwango elimu yetu? Hawakujua kwamba sera hizo zilijali zaidi uingi(quantity) kuliko ubora(quality) ? Tume italeta maswali zaidi kuliko majibu. Tusubiri tuone.
 
Mwanzo nlimheshim sana huyu Wazir Mkubwa kwa kuona angeweza kuwa na busara na msaidizi wa Wananchi nilimdharau huyu Mzee kwenye Kampeni za mwaka 2010 siku mbili kabla ya uchaguzi alifanya Mkutano wa hadhara ktk Mji wa Makambako kumnadi Deo Sanga(Jah People) Mbunge wa Njombe Kaskazini sasa hivi kwa maneno yake mwenyewe alikiri kuwa Elimu si lolote kwani uongozi ni karama kwani Watu walikuwa wanadoubt kutokana na Elimu ya Deo ya darasa la pili kuwa kwa wakati huu walimleta lkn si muda sghihi wa kumsimamisha yeye na wakati kuna watu wenye uwezo mzuri wanaoweza kufukuzana na utandawazi binafsi naona Pinda nae anachangia ktk kudumaza Elimu ya Tanzania kwani kwa maneno yake ya kudharau elimu kuna baadhi ya watu huyachukua kama yalivyo na kuyafanyia kazi. Hivyo kamati hiyo hakuna jipya itakalokuja nalo kwani Msingi wa Elimu umeuliwa na Viongozi waliopo madarakan
 
tume ngapi zimeundwa na hakuna impact yoyote tuliyo iona,tusitegemee miujiza kutoka kwenye hii tume ya pinda,binafsi naona ni vituko vya serikali na viongozi uchwara wa ccm,sababu za matokeo mabovu iko wazi na haiitaji elimu ya shahada kujua hilo,hzi tume wanazounda n kutuziba macho watanzania,nan asie jua kua mtaala wa elimu n mbovu?,nan asie jua mazingira wanayofanyia kaz walimu ni hatarish?,nan asie jua kipato kidogo cha mwalimu?,nan asie jua kua serikal haijal walimu?,nan asie jua kua selikar haiwekez vya kutosha kwenye elimu? nan asie jua kua baadh ya walimu hawana weledi wa kutosha na kaz yao? nan asiejua kua walimu wengi hawaipend kaz ya ualimu na hvyo hawafany kaz kwa moyo? nani asie jua kua hata wazir wa elimu pia ni bogus? UKUBWA WA PUA SIO WING WA KAMASI,WING WA SHULE ZA KATA ..............!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…