mwanakaya
Member
- Mar 17, 2012
- 56
- 183
Wanaspoti nawasalimu!
Jana nimeangalia kwa makini mechi ya pili ya Ligi kuu nchini Uingereza kati ya BHA na Manchester United ambapo Manchester ilipoteza mchezo kwa magoli mawili kwa matatu.
Pamoja na kwamba ndio kwanza msimu unaanza na inaweza kuwa sio sahihi sana kuhitimisha kwamba Manchester United Itafanya vibaya lakini pia kwamba mbinu za Mourinyo kwa misimu yake mitatu zimeendelea kuwa zile zile.
Msimu uliopita BHA waliifunga Man Utd mchezo mmoja na kutoa sare mchezo wa pili. Nilitegemea kwamba Mou angekuja mbinu bora za kuikabili timu hii kwa kuwa tena alifungwa mchezo wa mwisho wa msimu uliopita lkn inaonekana hakujifunza.
Msimu huu Jose anaonekana kulalamikia sana Bodi ya timu japo kila msimu amekuwa akipewa fungu la kufanya usajili. Kwa mfano msimu huu amepewa hela akasajili mabeki wawili (Eric Baily & Victor Lindelof) ambao katika mchezo wa jana walifanya makosa yaliyopelekea kupoteza mchezo.
Tujadili hapa, shida ya Man U ni nini? Mou mbinu zake zimekuwa outdated au makocha wengine wamezijua mbinu zake?
Sent using Jamii Forums mobile app
Jana nimeangalia kwa makini mechi ya pili ya Ligi kuu nchini Uingereza kati ya BHA na Manchester United ambapo Manchester ilipoteza mchezo kwa magoli mawili kwa matatu.
Pamoja na kwamba ndio kwanza msimu unaanza na inaweza kuwa sio sahihi sana kuhitimisha kwamba Manchester United Itafanya vibaya lakini pia kwamba mbinu za Mourinyo kwa misimu yake mitatu zimeendelea kuwa zile zile.
Msimu uliopita BHA waliifunga Man Utd mchezo mmoja na kutoa sare mchezo wa pili. Nilitegemea kwamba Mou angekuja mbinu bora za kuikabili timu hii kwa kuwa tena alifungwa mchezo wa mwisho wa msimu uliopita lkn inaonekana hakujifunza.
Msimu huu Jose anaonekana kulalamikia sana Bodi ya timu japo kila msimu amekuwa akipewa fungu la kufanya usajili. Kwa mfano msimu huu amepewa hela akasajili mabeki wawili (Eric Baily & Victor Lindelof) ambao katika mchezo wa jana walifanya makosa yaliyopelekea kupoteza mchezo.
Tujadili hapa, shida ya Man U ni nini? Mou mbinu zake zimekuwa outdated au makocha wengine wamezijua mbinu zake?
Sent using Jamii Forums mobile app