Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sheria haipo ila kama ni mnufaika wa moja kwa moja atapata mgao kama mzazi wake hayupo. Kama mzazi yupo basi atapata kile atakachopewa mzazi wake.Niliyaka kujua kama kuna sheria ya moja kwa moja inayompa haki mjukuu kuwa na sehemuya urithi kupitia mama yake.
Mjukuu sio mnufaika wa moja kwa moja otherwise wosia useme hivyo,Niliyaka kujua kama kuna sheria ya moja kwa moja inayompa haki mjukuu kuwa na sehemuya urithi kupitia mama yake.
Mjukuu hana haki ya kumrithi babu..Baba yangu mdogo alikuwa na mke mmoja na watoto watatu na mjukuu mmoja baba na mke wake walitangulia kufariki, baada ya muda kidogo akafariki mtoto mmoja kwa sasa wamebaki watoto wawili na mjukuu.
Swali
Je, Huyu mjukuu ana haki gani katika urithi wa babu yake?
Makaburi hayarithi.Mimi sio mwana sheria, nachojua yeyote yule aliyemtegemea huyo babu na mali yake katika maisha yake anahaki ya kupata urithi (kupata mgao)
Lakini pia mjukuu atapata mgao wa urithi kupitia kwa baba yake hata kama hayuko hai, kwa maana hiyo watoto hao 3 watagawana urithi bila kujali uhai wao.
MWISHO: USHAURI WANGU:
1.URITHI sio TUKIO ni Process (Ni namna gani ya kuziendeleza rasilimali alizoziacha
marehemu kwetu sisi na vizazi vijavyo)
2.URITHI: SIO kwa mtu mmoja (yaani mm juma nimerithi nyumba ya baba yangu)
HAPANA KABISA Juma anarithi na kizazi chake kupitia kwake ni mbio za kijiti ni lazima na yeye amrithishe mwanae na kuendelea
3. URITHI: SIO mali ya BAHATI HAPANA KABISA, Ni mali ya JASHO inastahili kuheshimiwa sio kamwe kuharibu au kuuza hovyo kama umeiokota vinginevyo hilo jasho la baba yenu ataliokota mtu mwingine baki kwa bei ya bure na lengo la baba yako litapotea nyie mtabaki maskini kwa maana hiyo bora yeye angeiuza kabla hajafa kuliko wewe.