Je? Mkojo Wa Ngamia Ni Dawa

Je? Mkojo Wa Ngamia Ni Dawa

Kennedy

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2011
Posts
54,894
Reaction score
64,043


Salaam Wa JF Wote

Nmekutana Na Mtu Mmoja Akiwa Anasumbuliwa Na Ugonjwa Wa UTI, Malaria, Kukosa Hamu Ya Chakula,Kwenye Maongezi Yetu Baada Ya Kumjulia Hali
Akaniambia Ana Miaka 10 Hajawahi Kuugua Magonjwa Kama Malaria, UTI, Minyoo, Vidonda Vya Tumbo Na Magonjwa Mengi Mengine


Akaniambia Mwaka 2013 Alikwenda Safari Mombasa, Siku Moja Jioni Akaenda Ufukweni Mwa Bahari Kupunga Upepo Mwanana
Mzee Mmoja Akapita Na Ngamia Wake, Sasa Huyu Jamaa Alistaajabu Kuona Wanyama Wale Wakiwa Warefu Sana,


Akamfuata Mzee Anayewamiliki Aongee Naye Mawili Matatu Angalau Ajue Umri Na Namna Anavyowatunza. Anasema Hao Ngamia Walikuwa Na Umri Wa Miaka 15,Na Wanakula Aina Mbalimbali Ya Majani

Mzee Mwenyewe Ngamia Akamwambia Mkojo Wa Ngamia Unatibu Magonjwa Mengi Ya Binadamu Tena Haraka Sana, Jamaa Akasema Sasa Naupataje Huo Mkojo, Yule Mfugaji Akasema Anaongea Na Hao Wanyama Wanapokea Amri Na Kutekeleza Muda Huo Huo.



Jamaa Akaambiwa Tafuta Kopo Lete, Kwakuwa Ni Ufukweni Akapata Haraka Yale Ya Maji. Mfugaji Akaongea Na Mnyama Akakaa Chini Akampa Amri Atoe Mkojo Akatoa Wakakinga Lita Moja, Pia Watu Wengine Wakakinga

Baada Ya Pale Jamaa Akanywa Kama Nusu Lita Ya Mkojo Wa Ngamia Ilikuwa Mwaka 2013 Hakuwahi Kuumwa Malaria, Tumbo,Minyoo Na Magonjwa Yoyote Hadi 2023


Yeye Anasema Mkojo Aliambiwa Ndiyo Ulimsaidia
Nimeleta Maelezo Marefu Kiasi Nia Yangu Ni Kutaka Kujua Iwapo Kuna Mtu Yoyote Amewahi Kutumia Ama Kusikia Hili, Kwakuwa Tuna Ndugu, Jamaa Na Marafiki Wengi Wana Changamoto Mbalimbali Za Afya Na Wanatumia Gharama Nyingi

Naomba Kuwasilisha!!
 
Huo mkojo utatetewa kama inavyotetewa strawberry, tende, tufaa, zaituni na zamzam
 
Back
Top Bottom