Je mlalamikaji yupo sahihi??

Je mlalamikaji yupo sahihi??

Hivi haiwezekani makanisa na misikiti kuweka ule mfumo sijui unaitwaje ambao sauti inaishia ndani kama vile clubs/disco zilivyo
 
Habari za muda huu wana JF??

Nimekutana na video moja mitandaoni iliyorekodiwa na muumini wa dini ya Kiislam akilalamikia Kanisa lililopo karibu na Msikiti alipokua anakwenda kufanya ibada na kukuta Redio ikiwa inaimba kwaya Kanisani hapo pasipo kuwa na mtu ndani.

Muumini huyo amelalamikia na kuziomba mamlaka kuingilia kati swala hilo kutokana na kile alichokua anakilalamikia.


Mimi sio muumini wa Imani hizo mbili tofuauti(Ukristo na Uslam)

Baada ya kufuatilia comments kwenye post hizi nimeona waumini wa Imani hizo tofauti kila mmoja akitetea upande wake.

Kwa upande wangu na kuheshimu Imani hizo nimeona wote kwa wakati huo walikua na makosa

1. Kanisa limefungulia kwaya kwa sauti kubwa inayoweza kuwafikia na kuwakwaza hata waumini wasiokua waumini wa Imani hiyo au waliopumzika jirani na maeneo hayo,

2. Msikiti umefungwa speakers nje na inasikika adhana kwa sauti kubwa kitu ambacho pia kinaweza kuwa kero kwa wasiokua waumini wa Imani hiyo.
Mambo mengine ni kukubaliana na diversity. Hatuwezi kufanana. Kwangu Mimi kwaya Wala adhana haziwezi kunisumbua. Tukibali tofauti zetu. Concentrate na Mambo yako. Kwaya Nini, wanaimba maneno ya Mungu, adhana hivyo hivyo.
 
Hivi haiwezekani makanisa na misikiti kuweka ule mfumo sijui unaitwaje ambao sauti inaishia ndani kama vile clubs/disco zilivyo
Adhana ni km wito na kuwakumbusha walio nje kwamba ni muda wa swala, haiwezi kuwekwa sound proof
 
Back
Top Bottom