Habari,wadau Mimi nina mdogo wangu aliteguka begi wakati anadaka mpira na kupelekea bega kushuka na kushindwa kubeba vitu swali langu amefanya vipimo cha MRI ya UTI wa mgongo kilingana na utaalamu wa daktari akijua maumivu yake yameanzia kwenye mgongo kusambaa kwenye mabega kwa madaktara wanafaham ilo lakini majibu ya MRI yakaja normal je?wadau ni kilimo gani nitaonesha tatizo la kuteguka kwa misuli?
Sent from my Infinix X650 using
JamiiForums mobile app
Habari!
Uombwaji wa kipimo hutegemea na kile ambacho mtaalamu wa afya hupata baada ya kusikiliza historia ya mgonjwa pamoja na ukaguzi wa mwili.
Kulingana na hayo hapo juu, unapoomba kipimo lazima uwe unahitaji taarifa ya kuthibitisha au kukanusha baadhi ya mambo unayofikiria kama ni tatizo au sehemu ya tatizo.
Ni kweli MRI ni kipimo cha juu kuweza kuelezea viungo vya mwili na tishu pia utendaji wake. Lakini mtaalamu anaweza kuongeza aina ya upigaji ili kupata picha mwafaka hii huusisha vitu kama upigaji mwafaka wa eneo husika na contrast. Hapa ndo huitaji mawasiliano mazuri kati ya mchukuaji wa kipimo na muombaji wa kipimo. Umuhimu wa uandishi wa historia kwenda kwa mchukua kipimo huonekana hapa kama sehemu muhimu ya mawasiliano.
Baada ya hapo ni usomaji wa majibu.
Kwa mtiroriko huu:
Mgonjwa=> Daktari => Mchukua kipimo=> Msomaji
Kutokutimiza wajibu kwa mmojawapo kwenye mnyororo huu, inaweza kusababisha kutokupata majibu sahihi.
Pia, kuruka hatua kwenye mnyororo huu huweza kuchangia kutokupata mwafaka.
Uhuru wa mtu kuomba vipimo na kwenda kufanya bila kufuata mnyororo husika pia ni sehemu ya tatizo kwa kuhisi au kuamini kipimo kikubwa kitaonyesha tatizo.
Kuna wakati kipimo kidogo kama Xray kinaweza kuwa suluhisho kwa matatizo mengine kabla hata ya CT scan, MRI vs PET scan. Suala kubwa ni kufahamu kipi kifanyike wakati gani na kwa kufuata utaratibu.
Lawama zitapungua sana kila mtu akitimiza wajibu wake sawasawa.
NB: Kutokana na mambo mengi kutokukamilika hapa, ni vigumu kujua tatizo linaanzia wapi kikamilifu.
Ushauri ni: Umuhimu wa mgonjwa kupitia vyema kwenye mnyororo husika ili kuona kama kipimo kinaendana na hali yake pia majibu kutizamwa tena kulingana na yatakayopatikana.