Je, Nabi ataweza kuumaliza utawala wa Mamelodi kule Afrika Kusini?

Je, Nabi ataweza kuumaliza utawala wa Mamelodi kule Afrika Kusini?

vibertz

JF-Expert Member
Joined
Mar 15, 2022
Posts
2,474
Reaction score
4,726
Kuna tetesi kuwa Nabi ameamua kwenda kufundisha klabu ya Kaizer chief baada ya kufikiana makubaliano ya pande zote mbili.

Baada ya kuifundisha Yanga kwa misimu miwili yenye mafanikio kwa ngazi ya mashindano ya ndani na ya kimataifa, Nabi aliamua kutafuta changamoto nyingine huko Morocco na kushindwa kuifanya Far Rabat icheze hatua ya makundi klabu bingwa kwa kutolewa na Etoile du Sahel.

Nabi katika ligi kuu ya Morocco ameiongoza Far Rabat kwa michezo 29 na kushinda michezo 21, sare michezo 5 na kufungwa michezo 3 akiwa na point 68 nyuma ya Raja kwa point moja ikibakia mchezo mmoja kwenye ligi kuu.
Kama ligi ikiisha hivi, Nabi atakuwa ameshindwa kuifanya Rabati kutetea ubingwa wake aliopata msimu uliopata je ataweza kushindana na Mamelodi waliojitawalia ligi ya Afrika kusini au ndio anaenda kuua zaidi CV yake na kupotea kabisa?
 
Kwani lengo ni kushindana na Mamelodi? Halafu si kila mtu anafuata CV, wapo wengine wengi tu wanafuata hela
Lengo ni kutwaa mataji na kwenye moja la taji ka dominate Mamelodi hivyo ni lazima awe na timu bora kuliko Mamelodi ndio abebe ubingwa wa ligi kuu. Kocha sio sawa na mchezaji, kocha ili uendelee kudumu kupata ajira ni lazima uwe na mafanikio. Ukiwa na CV mbovu hizo ela utazipatia wapi? Ni timu ipi itatoa pesa nyingi kwa kocha aliyekuwa na CV za kufeli feli tu kila mahali?
 
Kaizer chiefs imeshajifia kabisa asiende

Huko atakutana na kocha msaidizi kirusi Arthur zwane
 
Lengo ni kutwaa mataji na kwenye moja la taji ka dominate Mamelodi hivyo ni lazima awe na timu bora kuliko Mamelodi ndio abebe ubingwa wa ligi kuu. Kocha sio sawa na mchezaji, kocha ili uendelee kudumu kupata ajira ni lazima uwe na mafanikio. Ukiwa na CV mbovu hizo ela utazipatia wapi? Ni timu ipi itatoa pesa nyingi kwa kocha aliyekuwa na CV za kufeli feli tu kila mahali?
Kwani huko alipo kabeba mataji mangapi?!
 
... kocha ili uendelee kudumu kupata ajira ni lazima uwe na mafanikio. Ukiwa na CV mbovu hizo ela utazipatia wapi? Ni timu ipi itatoa pesa nyingi kwa kocha aliyekuwa na CV za kufeli feli tu kila mahali?
Unadhani mshahara wa kocha aliyeipa ubingwa Yanga na FAR Rabat mfululizo ni mkubwa kuliko kocha wa sasa wa Kaizer Chiefs ambayo mara ya mwisho ilichukua ubingwa mwaka 2014/2015, miaka tisa iliyopita?
 
Unadhani mshahara wa kocha aliyeipa ubingwa Yanga na FAR Rabat mfululizo ni mkubwa kuliko kocha wa sasa wa Kaizer Chiefs ambayo mara ya mwisho ilichukua ubingwa mwaka 2014/2015, miaka tisa iliyopita?
Ni mkubwa ndio, na huo ukubwa umetokana na Nabi mwenyewe kujipandisha thamani kwa kuifanya Yanga kubeba ubingwa na pia kucheza fainali ya CAFCC. Jambo lipo wazi, kuwa baada ya mafanikio hayo Kaizer chief na Far Rabat walikuwa wanamgombania na walitoa ofa kubwa kuliko waliyoitoa Yanga. Je Nabi bila hayo mafanikio ni timu ipi ingeangaika kumuhitaji?
 
Mkuu embu tusubiri kwanza asign kisha ndo tuzungumze.
 
Haya jibu swali la msingi...huko aliko amemaliza utawala gani?!
Mashindano bado hayajatamatika nchi Morocco. Ligi kuu inaisha tarehe 24 mwezi huu, kama akishinda huku Raja akitoa sare au akifungwa basi anabeba kombe. Na pia ukiachana na kubeba kombe, kaendeleza ushiriki wa Far Rabat klabu bingwa msimu ujao.
Pia kombe la FA yupo nusu fainali hivyo mpaka sasa bado yupo kwenye kinyang'anyiro cha kugombea mataji mawili.
 
Msimu ujao ligi ya Afrika kusini itachimbika haswa, Pirates ni wa moto, Kaizer nao wameanza project yao chini ya Nabi, Mamelodi wajipange kwa kuwa na benchi la ufundi ya kiwango cha juu.
 
Back
Top Bottom