Je, nani anastahili pongezi katika soka la Tanzania?

Watu wanashangaza sana ligi yetu imekuwa na ushindani sana.

Ukiona timu kama mtibwa na kagera Sugar zinapambana kutoshuka daraja ni picha tosha ushindani umeongezeka.

NB: Ningependa Mbeya City wasishuke daraja msimu huu aisee.
Waafrika kila kitu ni kulalamika tu hawaji na solution bali ni kulaumu laumu tu, hawapendi kupongeza kabisa ni chuki na wivu vinavyosababishwa na umaskini wetu ndiyo kitu kinatafuna bara hili.
 
Kwa hili la Azam nakubaliana na wewe. Eti kuna sehemu watu wanalipia ktk vibanda umiza kuangalia ligi ya ndani!! Hakika haya ni maajabu na usingeweza kuamini jambo hili linawezekana miaka michache iliyopita.

Ila mimi naongezea na TFF jamani, najua tumezoea kuwazodoa ila kuna mambo na mazingira wamefanya na kusimamia na matokeo ndio haya.
 
Watu wanashangaza sana ligi yetu imekuwa na ushindani sana.

Ukiona timu kama mtibwa na kagera Sugar zinapambana kutoshuka daraja ni picha tosha ushindani umeongezeka.

NB: Ningependa Mbeya City wasishuke daraja msimu huu aisee.
Upo sahihi chief.
 
Nakukatalia mpaka nakufa, bongo hakuna mchezaji anayecheza ili aonekane mahala kama yupo naomba unitajie ( labda kama una maanisha kwenda simba na yanga kwa uchache Azam).
Hongera kwa Azam kwa kutoongezea wafutiliaji,
Hongera kwa Kina MO kumwaga hela, wachezaji wazuri mataifa jirani wanazisaka hela za MO, GSM na Bakhressa.
Hongera kwa TFF kwa kuruhusu namba ya players wa kigeni.
Shukrani kwa Smartphones na mitandao ya kijamii.
 
Ushauri mzuri sana. Inapendeza na sisi Tanzania tukawa na jambo letu zuri.

Kwa maoni yangu, upo uwezekano wa Tanzania kuwa na ligi bora zaidi yenye kufuatiliwa Africa.

Ushauri kwa serikali, viwanja vyote vya ccm virudishwe serikalini viboreshwe au uwekezaji mkubwa ufanyike.
 
Naona umetoa bonge la summary.

Pamoja na uchumi kuwa mgumu lakini bado wafadhili wametoa pesa zao nyingi. Na hili la wachezaji wa kimataifa limeleta chachu sana.
 
Kwahiyo hizo Azam, Simba na Yanga co timu au sio? Umefikiria kabla ya kujibu?
 
Kaangalie Ligi ya South africa ina team ngapi urudi hapa
 
Mkuu nadhani hujanisoma vizuri,

Nimesema mpira wetu haujakua japo kuna hatua flani tofauti na mwanzo

Nimewasifia hao watu kwasababu ya kuifanya ligi yetu iwe na wafuatiliaji wengi, si kwa kukua kwa ligi

Ligi bado haijakua ukilinganisha na za wenzetu.
 
Waafrika kila kitu ni kulalamika tu hawaji na solution bali ni kulaumu laumu tu, hawapendi kupongeza kabisa ni chuki na wivu vinavyosababishwa na umaskini wetu ndiyo kitu kinatafuna bara hili.
Wewe jamaa embu pitia vizuri ni wapi nilipolalamika? Nimeuliza maswali kwasababu mleta mada katumia reference ya Simba vs Mbeya kutushawishi kuwa ligi imekwa na ushindani. Hivi timu kufungwa goli nne nako ni ushindani? Ingekuwa ni ushindani basi ingekuwa tough mechi kila upande na matokeo yasingepishana vile.
Unazungumzia kupongeza embu pitia post usome vizuri nimesema wazi kuwa Simba ndio imekuwa lakini ligi yetu bado haijakuwa. Mpaka hapo nimeipa sifa Simba japokuwa mimi ni mshabiki wa Yanga. Kuna gap kubwa sana kati ya Simba na timu zingine zote zilizopo kwenye ligi kuu wakati timu zilizobakia viwango vyao vinafanana fanana na ndio maana unaona timu za chini zinapishana point chache chache.
Na kinachoibeba ligi yetu ni Azam media kurusha live mechi kumeongeza wafuatiliaji
 
Kuna mke wa jamaa angu alikuja hajui lolote kuhusu mpira ila walivonunua azam tv saivi hadi line up ya Ihefu anakupangia[emoji3]
 
1.Uongozi Imara TFF ( hakuna migogoro)
2.Uongozi wa vilabu
3.Makocha
4.Simba s.c
 
Kwahiyo hizo Azam, Simba na Yanga co timu au sio? Umefikiria kabla ya kujibu?
Nachomaanisha mmi Bongo hakuna mchezaji anayecheza kusema aonekane aende nje.
Kama ni kwenda simba na yanga haihitaji Azam Tv maana hiyo movement ilikuwepo miaka yote.
Na simba na Yanga husajili yule anayewatesa wao tu.
 
Waafrika kila kitu ni kulalamika tu hawaji na solution bali ni kulaumu laumu tu, hawapendi kupongeza kabisa ni chuki na wivu vinavyosababishwa na umaskini wetu ndiyo kitu kinatafuna bara hili.
Mimi naona taasisi zilizofanya vizuri miaka mitano iliyopita ni TFF na Bodi ya ligi.
Tuna ligi ya wanawake, ligi ya under 17, ligi ya under 20, tumecheza AFCON under 17 mara mbili, tumecheza AFCON under 20 mara moja, tumetwaa vikombe under 17 vya East Africa mara mbili,
Timu yetu imeingia AFCON mara moja, Simba kaingia kwenye quarter final mara mbili, Namungo hatua ya makundi mara moja.
Mvuto wa ligi umeongezeka sana na udhamini kwenye ligi umeongezeka sana

TFF wamejitahidi sana kwa hii miaka mitano.
 
Mkuu baniani mbaya kiatu chake dawa. Hakika tusione mapungufu tu ya TFF ila wamefanya kazi kubwa sana....tuwapongeze.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…