Kwa maisha ya sasa hivi kuishi mbali na mkeo/mume ni hatari sana. Tumekuwa hatuaminiki hata tukiwa pamoja je kama hupo? nafikiri ni wakati mzuri wa kuangalia wapi ubase. Kama hilo swali limeshakuja kichwani mwako basi uwe mwangalifu na mengine mengi yanawezekana. Tafuta kazi karibu na mkeo ili uwe na amani.
Kazi zisiitufanye watumwa, weka mazingira mazuri ya wake zenu kujiajiri wenyewe. usikubali baba na mama kuamaka asubuhi wote mnaenda kazini. Weka miradi ambayo mkeo atasimamia hata siku umeacha kazi ghafla una pa kuanzia. Utakuta mke/mume asubui wangu wangu wanawahi kaziini. Mimi ilinilazimu niache kazi. Nimejiajiri nashukuru mungu naendelea vizuri.
Wale amba bado, hakikisha mna miradi mingi ya kufanya mama kukaa karibu na miradi iwe rahisi kuangalia familia kwa ukaribu. Ni hayo tu.