KING MIDAS
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 8,589
- 16,936
Nimekulia kwenye familia ya KKIKRISTO made hebu ya Kilutheli, na Sunday School na Kipaimara nilikuwa mwanafunzi bora kabisa nikiwa nimekariri vifungu vingi sana vya Biblia.
Baada ya kuhitimu kidato cha sita, nilipata daraja la tatu, nikaona niingie mazima kwenye biashara maana hamna tena namna nyingine.
Kwa miaka mingi nilikuwa busy na kutafuta maisha na kanisani sikukanyaga kwa muda mrefu hadi pale nilipotaka kufunga ndoa.
Baada ya ndoa ndipo nikaanza kwenda kanisani, kulikuwa na ujenzi wa kanisa kubwa , nikaahidi mabati ya kutosha kuezeka kanisa zima.
Baadae nilikuwa kusakafia kwa malumalu kanisa zima. Sasa baada ya hapo nikajitolea kufunga vyoo vya kisasa kanisani.
Kumbe nimekaribisha tatizo, nimekuwa nikipigwa sana mizinga na wazee na viongozi wa kanisa. Huyu anataka ada, yule anataka kile, hadi sasa naona hata kero kwenda kanisani.
Leo mchungaji alinitembelea ofisini kwangu, tumeongea mengi sana. Mchungaji wetu ni mjanja na bado janki, hivyo tuna uwanja mpana sana wa kuongea.
Pia akaniuliza mbona mahudhurio yangu yametetereka Church, sikuona ubaya wa kumpa ukweli. Nikampa ukweli wangu kwamba mizinga na vibomu vimekuwa vingi.
Akaniambia nitoe tu kwa imani, Mungu atanibariki. Jamani kweli?
Baada ya kuhitimu kidato cha sita, nilipata daraja la tatu, nikaona niingie mazima kwenye biashara maana hamna tena namna nyingine.
Kwa miaka mingi nilikuwa busy na kutafuta maisha na kanisani sikukanyaga kwa muda mrefu hadi pale nilipotaka kufunga ndoa.
Baada ya ndoa ndipo nikaanza kwenda kanisani, kulikuwa na ujenzi wa kanisa kubwa , nikaahidi mabati ya kutosha kuezeka kanisa zima.
Baadae nilikuwa kusakafia kwa malumalu kanisa zima. Sasa baada ya hapo nikajitolea kufunga vyoo vya kisasa kanisani.
Kumbe nimekaribisha tatizo, nimekuwa nikipigwa sana mizinga na wazee na viongozi wa kanisa. Huyu anataka ada, yule anataka kile, hadi sasa naona hata kero kwenda kanisani.
Leo mchungaji alinitembelea ofisini kwangu, tumeongea mengi sana. Mchungaji wetu ni mjanja na bado janki, hivyo tuna uwanja mpana sana wa kuongea.
Pia akaniuliza mbona mahudhurio yangu yametetereka Church, sikuona ubaya wa kumpa ukweli. Nikampa ukweli wangu kwamba mizinga na vibomu vimekuwa vingi.
Akaniambia nitoe tu kwa imani, Mungu atanibariki. Jamani kweli?