Je, ni busara kujenga nyumba kwa milioni 150 kisha kukusanya kodi laki 6 kwa mwezi?

Je, ni busara kujenga nyumba kwa milioni 150 kisha kukusanya kodi laki 6 kwa mwezi?

Mbona mnatupigia hesabu za UPE(Ualimu pasipo Elimu)? Yaan kwa miaka 29, kodi itakuwa hiyohiyo laki 6? Haiongezeki? Ni nani hapa amewahi kupanga nyumba na kulipa kiasi kile kile kwa miaka hata 5?

Inawezekana hii biashara ya nyumba za kupanga haina faida kivile. Basi tuipinge kwa hoja za kweli, sio za kuungaunga.
Unachosahau ni kuwa baada ya miaka 29 lazima uwe umefanya ukarabati mara kadhaa (ikiwemo kubadilisha paa, nyaya za umeme na design kadhaa za nyumba. Pia, design za miaka hiyo usidhanie utampangisha mpangaji wa maana zaidi ya wanachuo na mateja
 
Mi nishapanga kujenga lodge yangu mahali, vyumba kumi tu kwa siku vinaweza kunipa sh. 150,000 per day! Real estate is my dream
 
... kwa mtaji huo jenga g/house/lodge unapata 30k daily per room; ukiwa na vyumba 20 unapiga 600k daily kwa mwezi almost 18m/- kabla ya kutoa gharama za uendeshaji (mishahara, utilities, etc.). Lakini it is far better.
Hizi ndio akili za motivational speaker 😂😂😂😂😂😂 si mpaka vijae sasa kila siku.
 
Uwekezaji kwenye real estate, shares au Treasury bill una faida mbili (1) Ni return on investment (2) Appreciation in value of investment. Nyumba kama nyumba utaona hiyo kodi ya TZS 600,000 ni ndogo sana lakini ukiuza hiyo nyumba utapata zaidi mfano hiyo nyumba ya TZS 150,000,000 unaweza ukauza TZS 300,000,000.

Kwa wale tunaowekeza kwa ajili ya elimu ya watoto wetu; bado kuwekeza kwenye nyumba ni bora zaidi kuliko "Fixed deposit" kwani wakati nyumba ikiongezeka thamani kuendana na wakati, Principal amount kwenye Fixed Deposit haiongezeki thamani kinyume chake inapungua thamani (inflation).

Ushauri wangu wekeza kwenye nyumba pesa ambayo huna matumizi nayo yaani mtaji uliozidiki kwenye biashara yako na usiwekeze kwa matazamio ya kuvuna faida
Mistari ya mwisho.!
 
Umepata hiyo pesa, yote Ukaizike!? Huo ni wendawazimu wa hali ya kutosha. Kama unawashwa na kujenga, toa hats mil 30 ukajenge nyumba iishe kabisa uhamie hiyo nyingine iweke kwenye mzunguko wa biashara ya kuaminika na uifanye wewe mwenyewe.

Nilishasema sitokaa niyaogope maisha nikimbilie kuizika pesa(kujenga) niache kuiweka kwenye biashara kwa kuogopa kupanga.

Chukulia mfano, umeenda kujenga Mbande au Kisewe huko Mbagala, shughuli zako ziko Tegeta na huko ndiko ulikokuwa umepanga mwanzoni.
Kama shuguli ni Tegeta bas jenga huko kwann uende mbali
 
Thread nzuri sana hapa ndio utagundua tofauti ya:
1. KUSOMA na KUELIMIKA
2. Dhana Thoughts tofauti tofauti kwa kila taaluma yaani dhana ya
accountants, Finance Managers, Economists, Entrepreneurs
3. Lugha tofauti tofaut kulingana na taaluma

Mfano mzuri accountant anakuambia Nyumba ni asset nzuri sana maana siku zote value yake ina appreciate inapanda thamani eti kunakuwa na capital gain

Finance manager , Investment analysis anasema kwenye asset kama nyumba compare capital gain na Inflation then return yake ndio utajua kama una gain or lose

Economist ataangalia Feasibility study atakuambia nyumba haina hasara.

Entreprenuer ataangalia kwanza Cashflow then Return On Investment ndio ita determine either ni Asset or Liability

Sorry sijaiweka vizuri sana lakini najaribu tu kuonyesha changamoto tullizonazo kwa wasomi wetu hawa na kila mmoja anajiona yuko sahihi sana na anadiliki kuwashauri wateja/ jamii/ kwa hizo fikra zake

Ebu kwa mfano huo hapo accountant anaamini siku zote duniani land or House inapanda thamani yaan kuna capital gain je anasahau pia kuna Inflation ?
 
Point nzuri sana

Mashirka makubwa yenye uwezo kama Tigo na Voda, NMB nk hawajengi nyumba za kuishi maxpatriates - wanapanga. Lazima kuna maana kubwa katika hii strategic decision
Hata Minara wanakodi
Wafanyakazi wameoutsource kwa watu.
Wanafanya hivyo kuepuka mambo mengi.
Hawajengi sababu assets zao zaweza dakwa na serikali
 
Na hii ndio hofu yetu watanzania wengi.
Huwa hatujiamini kwenye biashara,lakini sababu inatokana na lack of business knowledge.
Ndio maana wote tumekuwa na utamaduni wa kujenga tu au kuziacha hela benki kwenye saving account.
Ila wahindi huwa hawana hobby ya kujenga majumba wapatapo pesa Wana njia zingine za investment Kama kununua bonds/shares au other liquid assets Kama golds na kuzihifadhi ndani.
Siku akifirisika anauza kwa Bei ya juu na kuibuka tena.
Wahindi wanajenga nenda upanga uone mijengo, ukiona muhindi kapanga jua Hana pesa ya kununua plot sehemu wanazopenda mfano upanga, kariakoo, na muhindi hawez kuja nunua kiwanja uswazi. Ila zikimtembelea wanajenga.
 
Nyumba inaleta security kwa familia
Mnakua huru hata kama hamna kipato
Sio kwa sababu ya wazazi

Mwanamke unakua free nyumbani kwako
Unapendezesha hata weeekend jumuiya na nini au shoga zako waje kikao cha kikoba ujinafasi

Kwenu mnaweza kupaendeleza kupakarabati nk...si kwenu bwana

Kwa hio mmezaa watoto bado hamjipangi hata kununua kiwanja muwe na kwenu?..

Jmn heshimuni nyumba ya familia usiolipia hata 100...ni kwakoo...hata watoto wakikua hawajakaa sawa wana pa kuanzia maisha

Mkiwa watu wazima vipato vikayumba mna pa kukaa
Mtu hadi miaka 60 upange we muhindi?..
Unajenga nyumba kwa ajili ya vikao vya VICOBA?? Hv Watanzania mtaacha lini ushamba? Mimi kwangu hakanyagi mtu mambo yote tunamalizana huko huko kwenye restaurant/hotel
 
Mi naona kupanga saa zingine ni vizuri kuliko kwenda jenga mbali unatumia gharama kusafiri na muda unapoteza mwingi.
Mtu anaishi Bunju anafanya kazi Posta huyu alitakiwa apange kkoo ili apunguze muda unaopotea na fedha anazotumia kwenye usafiri
 
Mi naona kupanga saa zingine ni vizuri kuliko kwenda jenga mbali unatumia gharama kusafiri na muda unapoteza mwingi.
Mtu anaishi Bunju anafanya kazi Posta huyu alitakiwa apange kkoo ili apunguze muda unaopotea na fedha anazotumia kwenye usafiri
La ajabu zaidi huko alipojenga hana hata bustani wala kiduka. Ananunua mpaka mchicha.
 
Na hizi ndizo akili za mwafrica per se.
Nimesoma comments za huyo laki si pesa kwenye uzi huu mojawapo ni comment inayosema "wahindi wana hela za majini" nimechoka alafu ni gamba mwenzio. Zero brain
 
Ukijenga nyumba kwa million 150 na kuanza kukusanya kodi ya 600,00. Itakupa rental yield ya 4.8%, siyo nzuri saana, lakini haijambo.
Rental yield ya kuanzia 7% kwenda juu ni nzuri zaidi. Nyumba ni long-term investment. Wanaweza kuja kufaidi matunda watoto wako/wajukuu/vitukuu. Kila kitu ni timing. Hali ya real estate Tanzania kwa sasa ni tete sana.
Kwenye thread hii wewe ndio wa kwanza kwa jibu sahihi asante sana bila shaka umesoma Finance or Investments
 
Uwekezaji kwenye real estate, shares au Treasury bill una faida mbili (1) Ni return on investment (2) Appreciation in value of investment. Nyumba kama nyumba utaona hiyo kodi ya TZS 600,000 ni ndogo sana lakini ukiuza hiyo nyumba utapata zaidi mfano hiyo nyumba ya TZS 150,000,000 unaweza ukauza TZS 300,000,000.

Kwa wale tunaowekeza kwa ajili ya elimu ya watoto wetu; bado kuwekeza kwenye nyumba ni bora zaidi kuliko "Fixed deposit" kwani wakati nyumba ikiongezeka thamani kuendana na wakati, Principal amount kwenye Fixed Deposit haiongezeki thamani kinyume chake inapungua thamani (inflation).

Ushauri wangu wekeza kwenye nyumba pesa ambayo huna matumizi nayo yaani mtaji uliozidiki kwenye biashara yako na usiwekeze kwa matazamio ya kuvuna faida
Akili kubwa
 
Kwa DSM maeneo hot 150M unaweza kutoa Chumba na Sebule + jiko lake zikawa 8 na pesa ya Fensi pembeni Market value ya chumba +Sebule+jiko classic ni 250,000-----350,000 at lowest 250*8= 2M kwa mwezi.

Nyumba ni Longterm investment itakuchukua kama miaka 6-8 kurudisha pesa yako kwa hapa Dar maeneo ambayo yamechangamka.
 
Xxxx
Kwa DSM maeneo hot 150M unaweza kutoa Chumba na Sebule + jiko lake zikawa 8 na pesa ya Fensi pembeni Market value ya chumba +Sebule+jiko classic ni 250,000-----350,000 at lowest 250*8= 2M kwa mwezi.

Nyumba ni Longterm investment itakuchukua kama miaka 6-8 kurudisha pesa yako kwa hapa Dar maeneo ambayo yamechangamka.
Mkuu elimu yako umefika hata darasa la Saba kweli?
 
waswahili tuna usemi wetu ya kuwa hakuna baba mwenye gari bali kuna baba mwenye nyumba,hiyo nyumba ya 150m kodisha kwahiyo 600000na baada ya miaka miwili iuze utapata faida.
Nalog off
 
Back
Top Bottom