Nadhani tunapokosea sana ni kutojua faida inakuja baada ya muda gani? Eneo ninalojenga je linalipa? Mfano jirani yangu mjeda kachukua mkopo sijui ni kiasi gani kanunua viwanja vitatu mtaani. Kajenga nyumba tatu, mbili hazijamalizika. Alipopata mkopo kwanza kamnunulia wife Ist ya kuwapeleka watoto shule.nyumba ya kwanza imeisha ni two in one kuna mpangaji mmoja tu. Hizo mbili keshapaua lkn finishing bado naona pesa zimekata, naona wife hatumii tena IST, watoto wanasimamishwa shule pesa hakuna. Imefikia wife wake anauza mpaka bites na mboga mboga mtaani. Huyu kafanya bad investment, kwanza maeneo aliyojenga kodi haizidi laki 3. Pili katumia pesa yote kujengea bila kuwa na savings huku marejesho yanamsubiri. Hapa utaona mkopo mbaya wala haufai. Lazima kuwe na projections ya mradi mzima. Nachukua pesa kiasi gani, mradi wangu una cost kiasi gani, mida wa mradi mpaka kukamilika, eneo husika la mradi lina thamani gani, mvuto wa eneo kwa wateja, umbali na barabara kuu, pia urahisi wa kufikika, uwepo wa maji, umeme. Baada ya mradi kukamilika tozo kwa chumba itakuwa kiasi gani? Je ntaweza pata rejesho kupitia tozo hizi? Atleast sasa waweza kopa mamilioni ukijua fika mradi utalipa