Je, ni kwanini Millard Ayo na Mkurugenzi wa TANAPA wasishtakiwe kwa uhujumu uchumi?

Huna hoja kaka, wasinge post wao wangepost wageni, au familia ya mfiwa. Na hii si mara ya kwanza ajali kutokea.
Mamlaka imefanya sawa kabisa, punguza ushamba na mihemko
 
Lakini wasingejua kwa wingi wa kiasi hiki, kuna vitu vingi vyenye negative impact kwenye utalii ambapo huko kwa wenzetu huwa vinabaki minong’ono tu, lakini hawatangazi wala kudhibitisha…
Kwa wenzenu wapi wasitangaze umeenda Nchi gani ajali itokee wakae kimya wewe kila kukicha ni huyu akamatwe huyu ashtakiwe mnawaacha Majambazi wakubwa wakitafuna fedha za Serikali hivi kweli unafikiri kabisaa kwamba wazungu wasijue wewe msaga nyoka ujue?
Ajali ya Mv Bukoba tulikua tunadanganyana kuwa sijui meli ilijaza mzigo mkubwa wakaja USA wakasema Meli hii hapa imegonga mwamba ndio chanzo cha ajali..
Watengeneze hizo bara bara ndio chanzo kikubwa cha ajali huko na zinatokea mara kwa mara wasifikiri kukusanya dollar tu..
 
Hiyo habari ni kweli au siyo kweli? Kila siku tunasikia habari za ajali za ndege za Boeing na bado zinafanya kazi kama kawaida japokuwa wana historia mbaya katika safari zao.

Hii nchi ina watu wajinga-wajinga sana, kila kitu mnataka kuweka siasa.
Tena hayo mandege yalishafanyiwa na uchunguzi na kuna baadhi ya nchi yamepigwa marufuku. Mengine kurudishwa kiwandani.

Siasa kwenye kila kitu haifai. Na ajarizinatokea kila sehemu muhimu kufanya uchunguzi kama kuna uzembe alio husika achukuliwe hatua
 
Avatar yako inasema mengi kuhus ww, endelea kuamini katika kuficha taarifa
 
Kwamba Miladi ashitake kosa gani?
 
Kila mtu anaangalia maslahi yake, Millard kuitoa hiyo taarifa inazidi kumweka vizuri na anavuna mashabiki nje na ndani ya nchi.

Suala la kusema maslahi mapana ya nchi walitakiwa waanze wenyewe viongozi wa nchi na wakusanyaji kodi.
Kila mtu angekuwa anaangalia maslahi yake binafsi bila kujali madhara makubwa yanayoweza kutokea at large sidhani kama kuna nchi ingepiga hatua hapa duniani, lazima pawe na hisia za uchoyo wa maendeleo, kama ilivyo Kenya. Kama serikali imekosea sio lazima na wewe umalizie kabisa kuharibu.., ni akili ndogo tu ilihitajika..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…