Je, ni kwanini nchi ya Rwanda si tu 'inasifika' bali kwa sasa 'inaogopeka' pia kwa kuwa na 'Majasusi' mahiri kabisa kuliko nchi nyingine za EAC?

Je, ni kwanini nchi ya Rwanda si tu 'inasifika' bali kwa sasa 'inaogopeka' pia kwa kuwa na 'Majasusi' mahiri kabisa kuliko nchi nyingine za EAC?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Inasemekana huwezi kupanga Jambo baya la 'Kuidhuru' Rwanda ukiwa ndani au nje ya nchi hiyo na kama ukipanga kufanya hivyo usijulikane mapema kwani utadhibitiwa Kikamilifu kabisa.

Pia wanasema huwezi 'Kuvamia' Mkoa wowote ule wa Rwanda hata kama Wewe ni Gaidi na ukauwa Wanyarwanda au ukawashambulia Wanajeshi wake tena 'Makomandoo' kabisa na wengine wakakimbia na kukuachia 'Vifaru' vyao.

Nasikia 'Majasusi' wa Rwanda ni wazuri sana katika 'Kunusa' hatari na wala hawana mambo mengi, hawapendi 'Sifa', hawajihusishi mno na 'Siasa' za Rwanda bali Wao wanapambana tu Kuilinda Rwanda na Wanyarwanda wote.

Je, hii ina ukweli wowote labda? Na kama ni kweli ina maana 'Mafunzo' wanayopewa 'Majasusi' wa Rwanda ni tofauti na Nchi zingine zote za EAC?
 
Si kweli kwamba Rwanda wana intelejensia ya hivyo isipokuwa P. K Mbuli kumlomo kama ulivyosikia hizo tetesi. Watu wanawachukulia poa kutokana na maswaibu yaliyowakuta 1994. Lakini ukiangalia ukubwa wa nchi yao, kilometer za mraba ni bomu mbili tu zinatosha kuimaliza Rwanda.

Vile vile kwa nchi inayo pakana nazo hakuna cha maana hasa Rwanda kitakachopelekea kuwaanzishia gwamvu. Gwamvu pekee litakaloibuka Rwanda ni la wenyewe kwa wenyewe kama ilivyo ada yao. Kwa Sasa watu wanajipanga wanammezea mate ya akili P. K, ni suala la muda tu.
 
Hiyo ilikua zamani lakini sasa hivi wanajeshi wa Rwanda wameanza kutumikia siasa na kulega kwenye jukumu lao la msingi la ulinzi wa mipaka. Siku hizi kila mahali ni wao tu kuanzia kwenye uendeshaji wa mikoa ya Rwanda, ujenzi wa mabarabara, madaraja, majengo na kadhalika

Kwenye chaguzi wanatumika kukibeba chama kimoja katika vingi vinavyogombea. Athari zake ni kubwa kwenye hili
 
Hivi nani aangaike na mkoa ambao hauna hata rasilimali moja? Kamkoa magazine yenye risasi 30 inatosha kukasambaratisha. Hao ni intelijensia ya kagame sio Rwanda na wanafanya kazi ya kumlinda kagame na maslahi. Kagame Kama sio kuiba madini ya Kongo angeshindwa kukaendesha kale kamkoa.

Wanaoigopa intelijensia ya Rwanda ni maadui binafsi wa Kagame ambao NI wanyarwanda wenzao ikiwemo na wewe na wanawashughulikia kweli kweli. Nchi Kama Tanzania inaanzaje kuiogopa intelijensia ya Rwanda. Huyo Kagame si alijaribu kumshika sharubu Kikwete kilichomkuta hukumsikia Tena anaishobokea tz, au unajisahaulisha?
 
Rwanda ni Taifa dogo sana lisilo na lolote la maana zaidi ya wananchi wake kuishi kwa hofu kubwa sana kutokana historia mbaya ya vita ya wenyewe kwa wenyewe

Hivyo hakuna Taifa lolote linaweza kupanga kuvamia nchi hiyo.

Pia hiyo intelijensia yao unayosema ipo maalumu kwaajili ya kulinda utawala wa Kitutsi dhidi ya mahasimu wao wa Kihutu na si dhidi ya Taifa lao against Taifa jingine

Katika ukanda huu wa nchi za maziwa makuu Tanzania ndio baba lao, superior country katika ishu za majeshi na intelijensia kwa ujumla.

UN Security Council linai-label Tanzania kama a supervisor/watchdog katika ukanda wa nchi za maziwa makuu,,, ikitokea mtifuano kidogo tu Burundi/Rwanda/Congo DRC basi UN security Council wanapiga simu Tz kuomba taarifa kamili na kuhitaji Tz iunde na ipeleke delegates kushughulikia mtifuano huo.
Amani ya ukanda wa maziwa makuu ipo mikononi mwa Tz

Tunalinda Amani ya nchi yetu,Tunalinda Amani ya nchi nyingine.

Mungu Ibariki Tanzania
 
Hivi Nani aangaike na mkoa ambao hauna hata rasilimali moja? Kamkoa magazine yenye risasi 30 inatosha kukasambaratisha. Hao ni intelijensia ya kagame sio Rwanda na wanafanya kazi ya kumlinda kagame na maslahi. Kagame Kama sio kuiba madini ya Rwanda angeshindwa kukaendesha kale kamkoa. Wanaoigopa intelijensia ya Rwanda ni maadui binafsi wa kagame ambao NI wanyarwanda wenzao ikiwemo na wewe na wanawashughulikia kweli kweli. Nchi Kama Tanzania inaanzaje kuiogopa intelijensia ya Rwanda. Huyo kagame si alijaribu kumshika sharubu kikwete kilichomkuta hukumsikia Tena anaishobokea tz, au unajisahaulisha?
Mkuu umejibu vizuri sana ofcoz ni sifa za kijinga tu kuhusu Rwanda halafu kama mtu hajafika anaweza akaamini huu uzushi hamna kitu kule bora hata South Sudan
 
Nimesoma comments zote nahisi watu hawajelewa fasihi nzito iliyopo kwenye huu uzi. Nawashauri kwamba hebu muupitie tena kwa utulivu na umakini, msome kati ya mistari(between the lines) kisha tupate maoni ya kifasihi.

Fasihi ni pana na inategemea kila mmoja kaichambua vipi kazi husika na hiyo inaonyesha ubora wa "Fanani", ila kwa maoni yangu Rwanda kama Rwanda imetumika kuwakilisha hoja ya mahala fulani.
 
Nimesoma comments zote nahisi watu hawajelewa fasihi nzito iliyopo kwenye huu uzi. Nawashauri kwamba hebu muupitie tena kwa utulivu na umakini, msome kati ya mistari(between the lines) kisha tupate maoni ya kifasihi.

Fasihi ni pana na inategemea kila mmoja kaichambua vipi kazi husika na hiyo inaonyesha ubora wa "Fanani", ila kwa maoni yangu Rwanda kama Rwanda imetumika kuwakilisha hoja ya mahala fulani
Kwani humjuagi huyo? Hana fasihi yoyote hapo. Hii Wala Haina uhalisia na yanayotokea huko kusini
 
Nimesoma comments zote nahisi watu hawajelewa fasihi nzito iliyopo kwenye huu uzi. Nawashauri kwamba hebu muupitie tena kwa utulivu na umakini, msome kati ya mistari(between the lines) kisha tupate maoni ya kifasihi.

Fasihi ni pana na inategemea kila mmoja kaichambua vipi kazi husika na hiyo inaonyesha ubora wa "Fanani", ila kwa maoni yangu Rwanda kama Rwanda imetumika kuwakilisha hoja ya mahala fulani
Kuwakilisha kichapo kilichotokea kule Ntwara?
 
Ni swala la mda tu

Nina uhakika kuna watanzania wanashirikiana na hawa washenzi kuua ndugu zetu ili kumtia kiwewe raisi

Watashindwa, na wakishughurikiwa tusisikie kelele.
 
Tulikua vizuri sana, sijajua majukumu ya majasusi wetu yamekuaje.

Kuna watu wa military intelligence wamejaa kwenye taasisi za kiraia na wanafanya majukumu ya civilian intelligence agencies.

Tukiendelea hivi Rwanda itaendelea kuwa juu kijasusi, sisi tutaendelea kupokwa vifaru na kubughudhiwa na vile vigaidi uchwara kule kusini.
 
Kosa litakalo mgharimu huyu..tall ni kufeli kuweka suluhu..baina yake na wahutu...! angeliomba hata saidizi kwa magwiji wa diplomasia! ila kiburi kinavyo mtembea sasa...

Kuishi kwa visasi na kuviziana ni zaidi ya mtihani ... ..
 
Kwani waliwaachia kifaru big no nafikr ni jeshi la msumbiji, wale walifanya ambush kweli wameua watu ila hawawezi tia watu kidole namna ya kuteka kifaru na wakipeleke wapi,na wamekitekea wapi ilihali wamevamia kijijini.
 
Hakuna ujasusi usiohusisha siasa, unafikiri kwanini hali ya upinzani Rwanda ipo ilivyo? Alafu pia Rwanda ni nchi ndogo sana na rahisi sana kulinda mipaka yake kulinganisha na nchi kama Tanzania, Tumezungukwa na nchi nyingi zenye matatizo ya kiusalama lakini bado vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vimefanikiwa tusipatwe na madhara.

Kutokea ambush za kihalifu inaweza kutokea popote, lakini hakuna anayeweza kuingia nchi hii na kumwaga damu za Watanzania akabaki salama. Hao waliotenda huo unyama tunaousikia WATALIPA! Africa na dunia inajua, ni ukichaa kuigusa Tanzania.
 
Back
Top Bottom