Je, ni kweli kuna genge linataka kukwamisha juhudi za Rais?

Au wazee wa legacy wanaendelea kufanya yao 🤣🤣🤣🤣🤣
 
Hakuna uhalisia wowote ni kujaribu kukwepa majukumu yako. Wewe kama ndo kiongozi mkuu wa serikali, Rais, amri jeshi mkuu, mwenyekiti wa CCM taifa unashindwa je kusambaratisha hayo makundi kama unayafaham yapo?
Maybe ndo kastukia huo mchongo!
 
Paruwaneni tu, weita tatutatu Kasumbalesa aijawahi lala.
 
Mimi namshauri mheshimiwa raisi avunje baraza la mawaziri!

Hii itamsaidia kujenga himaya yake na lawama zitaisha.
Avunje baraza la mawaziri halafu ataliunda kutokea wapi ambapo wabunge wote wako bungeni kwa nguvu ya mtu mwingine ambaye hayupo kwa sasa?

Kilichoanza kumkera kwa sasa ni ukungu bado mvua ya theluji kuna hatari dereva akakimbia usukani asifikiri nguvu iliyo kimya na ameibagaza ataishinda ni ngumu sana.

Kiongozi wanchi anawajibika kubeba lawama zote zinazojitokeza sio kusukumia awamu iliyopita kwani yeye alikuwa wapi si alikuwa sehemu ya mamlaka?

Watanzania hawayumbishwi kwa sasa kwa matamko na kujitetea kisiasa
 
ukiona mtu ameanza kulaumu ujue ameishashindwa successful people never blame, yeye kama anaweza aoneshe show sio kutupia lawama serikali iliyopita wakati alikua sehemu ya hiyo serikali
 
Mama sio mbaya tukianza upyaa, punguza masalia yote haujachelewa.
 
Chama kimerudi kwa wenyewe
 
Hizi ni porojo kama porojo zingine za kuuza umeme nje ya nchi. CCM wanajitekenya wao na kucheka
 
Gari bovu linaangushiwa AWAMU YA 6.

Makundi hayo OVYO, YASIYO NA UZALENDO ni kuyaondoa mamlakani mara moja.

Mh.Rais wetu asiyavumilie hata mara moja.

SIEMPRE CHIFU HANGAYA 🙏
 
Tangu amechukua nafasi ya uongozi baadhi ya Watanzania tuliona mbali tukamshauri kuondoa wale watendaji waliokuwa karibu zaidi na serikali ya mwendazake na kuchagua watu wengine ambao watakuwa wanamtii hasa pale anapotoa maelekezo fulani yafanyike ila mh. Raisi hakuzingatia ushauri huo leo amekuja kujua .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…