Je ni kweli Mahakama ni mhimili huru au ni taasisi ya Serikali?

Je ni kweli Mahakama ni mhimili huru au ni taasisi ya Serikali?

tz2015

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2014
Posts
982
Reaction score
447
Habari zenu wanajamvi wote katika jukwaa hili.

Ni muda mrefu nimekuwa nikijiuliza kuhusiana na uhuru wa mhimili huu unaoitwa mahakama bila kupata ufumbuzi.

Swali langu linakuja pale ninapokuta mihimili mingine kama vile bunge, na serikali wanachagua viongozi wao wenyewe, mfano, wabunge ndio wanaomchagua spika wa bunge kwa utaratibu waliojiwekea na wanashiriki kugombea na kupiga kura.

Serikali nayo tunaamini wananchi ndio wadau wakuu wa serikali au kwa maneno mengine ndio waajiri wa viongozi wa umma,na wanashiriki kuiweka serikali madarakani.

Sasa najiuliza kwa upande wa mahakama ni nani kiongozi mkuu wa mahakama? kama ni jaji mkuu,mbona anateuliwa na rais na kwa mawazo yangu ni rahisi huyu mteule wa rais kuendeshwa na aliyemteua na hivyo kuufanya mhimili huu usiwe huru tena bali kuwa taasisi ya serikali.

Nimeleta kwenu wanajamvi kwa anayejua aniondolee ujinga huu.

Naomba kuwasilisha kwa majadilianao.
 
Hoja yako inamashiko ndugu. Japokuwa katiba inasema kuwa Mara tu jaji ateuliwapo na raisi, raisi mwenyewe tu hawezi kutengua tena uteuzi huo km anavyofanya kwa mawaziri.

Pili unaposema bunge spika wanamteua wenyewe, lakini ukirudi nyuma pia spika lazima awe mbunge, na mbunge huwa anateuliwa na wananchi, na umesema wananchi ni sehemu ya serikali, KWA maana hiyo hata muhimili huu haupo huru.

Ukija KWA serikali, waziri mkuu nisehemu ya serikali na anateuliwa na raisi, lakini bunge linaweza kumuwajibisha WAZIRI mkuu na hata kusababisha atolewe. Mfano Edward low as a. Hii nayo inaonesha hata serikali haipo huru.

Kiufupi kuna kitu kinaitwa check anda balance. Hivyo hali hiyo haikwepeki ila inamipaka yake
 
Back
Top Bottom