Inashangaza sana kiukweli.katika pita,pita yangu mitaani nikiwa katika harakati zangu za kujikwamua kiuchumi.nilifika katika mgahawa na kupata chakula cha mchana.pembeni yangu kulikua na vijana wanne,nao wakipata vinywaji uku wakiongea kwa sauti kubwa tu, ambayo kira aliokua,mle mgawahani anasikia.NILISHANGAA SANA NILIPO SIKIA MMOJA WAO AKISEMA"yaani maisha haya bora kuzali mbwa ulaya kuliko,kua binadamu tanzania".mwisho wa kunukuu.Kiukweli kauli ile ilinishangaza sana na kuniachia maswali mengi sana kichwani mwangu.katka maswali ambayo najiuliza ni kama yafutayo-:
(1)je?nikweli mbwa ulaya ni bora kuliko binadamu aishio tanzani?
(2)uvivu uzoba wa kuto fikili nini cha kufanya ndio hali iliompelekea kuongea kauli ile?
(3)ukosefu wa ajira,na kutokua na njia m'badala ya kuongeza kipato ndo chanza cha hayo yote?WANA JF NIPENI UFAFANUZI JUU YA HII KAULI.