Je, ni kweli Moshi na Arusha ndo inaongoza kwa kuwa na mafundi rangi wazuri wa magari?

Je, ni kweli Moshi na Arusha ndo inaongoza kwa kuwa na mafundi rangi wazuri wa magari?

Habari wadau,

Ninahitaji Fundi rangi mzuri, nimefanya research kati ya watu 8 katika 10 wanasema nipeleke gari Moshi au Arusha sababu wanajua vizuri kupiga rangi.

Je, ni kweli wanapatikana huko tu?
Wewe ungeuliza tu ni garage gani Arusha au moshi naweza kupaka rangi gari?
Ukweli ni kuwa unaweza kutengenezewa gari lolote likatoka kama vile ndio limetoka japani/ulaya ILA na bei zake zimechangamka
hivyo kama ni gari la kawaida, huna haja ya kupeleka huko kwani bei itakuwa juu; ila kama ni gari la kisasa la bei ya juu songa mbele; ulizia Garage tu
 
Moshi na Arusha kumebahatika kuwa na ufundi mkubwa wa magari na kampuni kubwa za kukata Cruiser zipo huko kwa mfano Moshi kuna Rajinder na Arusha kuna Hans hao jamaa wamekuwa na mafundi kibao wa kanda hiyo na kama unavyojua jamaa walitrain mafundi kufanya kazi kidunia ya sasa na ndo sababu kubwa mafundi wa mtaani wengi unakuta walipita kweny hiz kampuni kubwa au wamefundishwa na jamaa walopita huko. hii ndo sababu kuna mafundi watundu sana kaskazini sio tu kweny rangi ila hata kuchonga body na upande wa ufundi. kama bado hujapata fundi nijuze nikupe mpare flani yupo arusha huyu anakufata ulipo.. na kazi zake ni kiwango anachukuliwaga hadi nchi jirani.
 
Kwa mafundi ambao sio wababaishaji Moshi ni hakika, gari ikiwa ina tatizo unaelezwa straight na anachosema ndicho hasa na gharama zao ndio zitakuacha taya wazi.

Huku Dar mtu kufunga wishbone bush tu anataka umpe 20K wakati moshi kazi hio hio mtu anaifanya hata kwa buku 5!

Overhaul mtu anakufanyia kwa laki 1 Moshi. Ila hapa Daslam mtu wa overhaul lazma umuandalie hela ya tofali za nyumba nzima. Ndio akufanyie hio kazi na pengine hata asiweze akamtafute mtu mwengine ndio amfanyie hio kazi.

Body works ukiwa na 30K gari wana clear dents zote na kurudishia rangi. Hapa Dar hio 30K ni labour charge tu 😂😂😂
Dar inabaki kuwa juu
 
Hivi kweli Cfao wanakuwa na mafundi bora sana? Maana kuna mmoja namfahamu na mwingine keshastaafu huko, lakini kuna gari uwa wanalikimbia.
CFAO wana mafundi wazuri katika level. Nakumbuka zamani sana nilisha enda pale kufanya kama mafunzo flani ya ufundi kutumia cheti changu. Wale tunao ingia na mavyeti makubwa wengi wetu ni vimeo ila pia wenye mavyeti makubwa ukiwakuta deep wapo deep kweli na wengi walipitia. Ila pia pale kuna katabia ka ku specialize maeneo flani, ukimpeleke nje ya eneo lake anakimbia
 
Moshi na Arusha kumebahatika kuwa na ufundi mkubwa wa magari na kampuni kubwa za kukata Cruiser zipo huko kwa mfano Moshi kuna Rajinder na Arusha kuna Hans hao jamaa wamekuwa na mafundi kibao wa kanda hiyo na kama unavyojua jamaa walitrain mafundi kufanya kazi kidunia ya sasa na ndo sababu kubwa mafundi wa mtaani wengi unakuta walipita kweny hiz kampuni kubwa au wamefundishwa na jamaa walopita huko. hii ndo sababu kuna mafundi watundu sana kaskazini sio tu kweny rangi ila hata kuchonga body na upande wa ufundi. kama bado hujapata fundi nijuze nikupe mpare flani yupo arusha huyu anakufata ulipo.. na kazi zake ni kiwango anachukuliwaga hadi nchi jirani.
Samahani Naomba mawasiliano yake
 
Back
Top Bottom