Je, ni kweli mtu akijifungua kwa operation uzao wa kwanza hawezi tena kujifungua kawaida?

Asante kwa elimu Dr., mimi nina swali, je ambaye hutoa maamuzi kuwa nyonga ni ndogo hivyo ufanyike operation ni daktari au muuguzi?? Samahani, ila sinaga imani sana na wauguzi ktk baadhi ya maamuzi yao!!
Na je ni kweli kuwa nyonga kuwa ndogo yawezekana kuwa mtoto labda alikuwa mkubwa zaidi ya njia ya kutokea?? Kuna uwezekano raundi ya pili akawa mtoto ana saizi ndogo??
Nilikuwa nahitaji hii elimu, nimewahi uliza humu ila sikupewa maelezo ya kina hivyo niliingia mtandaoni na kujipatia election mu kidogo, hivyo kwa kuwa Dr. Upo naomba elimu ya ziada!
Nimeelimika pia kutokana na elimu uliotoa hapo juu, asante!!
 

Kawaida mshono hupona kabisa baada ya muda gani, maana mi mke wangu kabeba hii nyingine baada ya kupita mwaka na miezi 6 tangu apasuliwe, msaada kwa tena tafadhali.
 
Under ideal conditions, maamuzi kuwa nyonga ni ndogo hivyo afanyiwe operation hutolewa na daktari; Na daktari hutoa maamuzi hayo baada ya kuwa amepima njia ya mama mjamzito, na kuona kuwa size ya nyonga ya mama ni ndogo kuliko kawaida na haitaweza kupitisha mtoto kwa njia ya kawaida. Ideally, yote haya hufanyika wakati mama mjamzito anahudhuria kliniki, na ndipo sasa daktari baada ya kumpima huamua kama mtoto anawez kupita au laah. Ndio maana ni muhimu sana kwa mama mjamzito kuweza kuhudhuria kliniki zake kama anavyopangiwa; ili haya yote yafanyike. (Pamoja na vipimo vingine vingi pia kama wingi wa damu, grupu la damu la mama, ultra saundi ya kuangalia ukuaji wa mtoto na ukubwa wa mtoto, etc).
Na pia, ni kweli kuwa mtoto anaweza kuwa mkubwa kuliko kawaida, kiasi cha kusababisha kuwa vigumu/kutokuwezekana kwa mtoto kupita katika njia ya kawaida na hivyo mama kuhitaji oparesheni (kikawaida, mtoto kuanzia kilo 4.5 huwa inakuwa vigumu kuzaliwa njia ya kawaida). Lakini, pia wako ambao wanazaa watoto hata wa kilo 5 kwa njia ya kawaida (nimeshuhudia wengi tuu); Ndio maana ni muhimu kwa vipimo kuweza kufanyika mapema; ili sasa daktari aweze kuangalia kwa kadri ya makadirio ya uzito wa mtoto yalivyofanyika (huwa inakadiriwa kwa ultra saundi), na pia kwa ukubwa wa nyonga ya mama, je huyu mama ataweza kupitisha mtoto huyo kwa njia ya kawaida?? Au atahitaji oparesheni, na kama atahitaji oparesheni, aweze kupangiwa tarehe (elective cesarean section), ili asipate leba, apigwe kisu moja kwa moja. Kwa hiyo kwa ufupi, ndio inawezekana size ya mtoto ikasababisha mama ajifungue kwa oparesheni (hasa kama ni zaidi ya kilo 4.5), na inawezekana kama mimba inayofuatia mtoto kama akiwa ni mdogo (kwa mfano kilo 3), akapita vizuri tuu.
Tatizo kibongo bongo, wamama hawahudhurii kliniki kama inavyotakiwa, na pia hata wanaohudhuria, kliniki nyingi hazina huduma zile ambazo ni standard mjamzito anatakiwa apate (kama ultra saundi), na wanalipua lipua tuu. Matokeo yake, vitu ambavyo ilibidi vijulikane mapema kabisa wakati wa kliniki vinakuja kujulikana wakati wa leba, na kusababisha heka heka na matatizo lukuki. barafuyamoto
 
Asante sana Dr., nimejifunza kitu muhimu siku ya leo mpaka sasa toka kwako!!
 
Muda gani maalum
maana wangu mi kabeba ikiwa imepita mwaka na mi 6 tangu apasuliwe.
hiyo ni risk,inakuwa vigumu kufanya trial of scar sababu inatakiwa at least miaka 3 ndio abebe mimba
 
Ewe Mwenyezi wanusuru mama zetu na janga hili la operation,
manake mh! Omba yasikukute.
 
Ipo factor nyingi za mtu kuzaa kwa oparation , lkn akizaa yakwanza ya pili anaweza kuzaa kwa kawaida isipokuw tu kama amepata mimba mapema sana chini ya mwaka mmpja laima afanyiwe elective mana ili azae kawaida anatakiwa akae miaka 3 ndo abebe mimba tena
 
Asante

Maana watu wanadhani ni "kupenda" u "uvivu"
 
Asante dr....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…