Je, ni kweli tozo wanazotozwa wananchi zinatumika kulipa mikopo wanayochukua Zanzibar?

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
38,920
Reaction score
44,970
Kumekuwa na hii tabia ya kuchukua mikopo kwa ajili ya shughuli mbali mbali zinazoitwa za kimaendeleo; ila kinachoshamgaza ni jinsi mikopo hiyo inavyogawanywa kwa usawa baina ya Watanzania wa Bara na Wazanzibari as kanakwamba idadi ya Zanzibar na Bara ni sawa.

Hivi uwe na maandazi 10, halafu watu 9 uwape maandazi ma 5 na mtu mmoja umpe maandazi ma 5, yaani nusu kwa nusu. Hapo kuna usawa katika ugawaji wa maandazi hayo?

Na linapokuja kwenye suala la kuyalipia hayo maandazi, wale tisa wanatoa 90% ya malipo na yule mmoja anatoa 10% ya malipo, je, mantiki ni ipi, kwahiyo watanzania tunakamuliwa tozo kulipa madeni na riba zisizotuhusu?
 
Kwani hao Wazanzibar hawakatwi tozo za miamala pamoja na kodi za TRA?

Kama jibu ni ndio wanakatwa ni haki yao kulipiwa.
 
Kichwa cha habari hakiendani na kilichoandikwa. Hata hivyo ingekuwa vyema kama ungetoa mfano wa mikopo iliyochukuliwa na kugawiwa nusu kwa nusu, haya madai yangekuwa na mashiko.
 
Je Kuna tozo Zanzibar?
 
Shida huna ushahidi wowote. Uzi wako unakuwa km porojo na hisia tu. Tafuta takwimu zinazoonesha ukweli vinginevyo itaonekana chuki na ubaguzi kwa ndugu zetu wa Zanzibar
 
Ni Kweli umeuliza SWALI bt swali lako linaleta NDITTA usoni, Si poa😠😠.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…