Je, ni kweli TRA wameshaita watu kwenye ORAL INTERVIEW?

Mkuu sisi watu wa pembeni ambao hatuku fanya huo usahili huo tuna shukuru kwanza kwa kutuletea taarifa ya kile ulicho kiona kwenye usahili huo, sababu hao upande wa pili walio chaguliwa kuendelea na usahili hawawezi ongea chochote hapa kuhusu kilicho tokea sababu tayar wao wamesha nufaika pakubwa na matokeo yao, kwa maoni ya upande wako unadhani nini kifanyike baada ya yote hayo ili kuleta imani kwa watu wengine baada ya kuona andiko lako hili..? ,maana tunapo elekea ni jamii kukosa imani na serikali yao kwenye kukosa haki zao za msingi kama hizo na mambo mengine mengi tu sasa.
 
hii ngoma haijasahihishwa,walichofanya wamechukua sample ya watu wachache kwenda oral ili kujidai kuwa walifanyisha watu usahili,majibu ya oral hawatayapublish wataitana kwa vimemo tu,wakiulizwa watasema waliwapigia wahusika simu na kuwatumia e-mail.hii ndio bongoland.mtihani ulikua mrahisa sana ule hasa kwa upande wa tax management officer ii
 
Mtihani mrahisi na wakati kuna wenzio wamepata zero?
 
Bongo yoso mjomba,Binafsi nipo tayar kupita mbele uletwe ule mtihan niliojibu mm tusahihishe kw majibu yao tuone km hiyo 33 waliitoa wapi,actually nimeona vijana weng mtaani hawajaridhishwa na outcome hii ila hakuna cha kufanya kw Tz hii.
 
Jibu la nini kifanyike!?
1.Taasisi zinazopewa mamlaka ya kuajiri yenyewe inabidi zijitathimini kama zinapaswa kuendelea kuendesha mchakato wa usahili pasipo upendeleo.
2.Taasisi kama takukuru na usalama ni lazima wawe wanapenyenza watu wao katika mchakato hii.
3.Mchakato wa usahili uhusishe taasisi nyingi Kila moja ipewe jukumu lake mfano shortlist awe mwingine, kutunga mtiani mwingine na matokeo yathibitishwe na jopo la wataalamu katika sector iyo hii itaondoa loop hole ya kuvujisha mtiani na upendeleo.
4.Usahihisaji uwe na time limits ili kutokuleta wasiwasi miongoni mwa wasahiliwa
5.Kuwe na manpower zaidi ya kusimamia mtiani.
 
Wahusika watazame hili
 
USHENZIII MTUPU!...nilikaa na mdada alikuwa hajui kitu kenye written, alikopy kila kitu kwangu lakini kapata 58 mimi 31...siombi tena kazi serikalini
Hii kali sana, pengine dada lao alichukua baadhi ya vitu kwako vingine kwa mwenzako, ila Dah [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] hii kali sana
 
Kwenu Passmark ni ngapi ?.

Kama wote na huyo mdada hamjachaguliwa basi kuna namna hizi marks itakuwa ni za kutengenezwa tu
Yeye kachaguliwa mimi nimekosa wakati aliangalizia kwangu alikuwa hajui kitu ...passmark ni 50 ...kapata 58 mimi 31 daaah akiananii......nimeumia kichiziii atleast ningemfata kwa maks basi...
 
Ili uajiriwe TRA Inatakiwa uwe umesoma course gani na gani chuo maana nimesoma ifm lakini sikuchukua taxation nilisoma course nyingine
 
tafuteni connection acheni kulia lia hum
Sasa kila mtu akisha kuwa na hiyo connection, hiyo nchi si itakuwa ina kwenda kimichongo michongo tu mkuu kila sector hapa mm nadhani Lengo la mleta mada hii ni kuieleza jamii kupitia serikali wasikie malalamiko haya then waya tatue na kuyafanyia kazi ila kuendelea kutafuta connection sio muarobaini wa kutatua jambo hili tukumbuke kuwa kuna vizazi na vizazi vina kuja hapo baadae sasa wakija katika mfumo wa connection na wao hali ndio itakuwa mbaya zaid tunapo elekea mambo haya lazima sisi tuliopo wakati huu tupaze sauti zetu kama hivi ni moja ya njia sahihi ipo siku ujumbe uta fanyiwa kazi.
 
Umeongea vyema..
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…