Je ni lini Tanzania itaweza kurusha satellite angani?

Je ni lini Tanzania itaweza kurusha satellite angani?

siku ccm itakapo toka madarakani...

kama sivyo, basi KATIBA ya nchi hii, itakapo fanyiwa marekebisho....
 
Satellites sio mchezo mchezo, kama mnavyodhani huwezi miliki sate alafu silaha unanunua, huko juu watu wanavyogombania viwanja utadhani wapo ardhini.
 
Ni Tanzania hii hii mkuu, hao walioendelea kuna mahali walianzia na sisi ndiyo tumeshaanza hatua ya kwanza, badala ya kuwa negative, hebu tuunganishe mawazo, nguvu na rasilimali kwa pamoja na tusema sasa yatosha! hatutaki kununua, kuuza na kutumia (kwa mfano) Smart phone toka ughaibuni, tunataka kutengeneza zetu wenyewe na sisi ndiyo tuwauzie majirani zetu. ili kuwezesha hili kumeanzishwa klabu maalum kwa ajiri ya kuwaunganisha watanzania wa kada mbalilmbali ili waweze kushiriki kwa kutoa maoni ya kuboresha au hata kufanya kile ambachi wanadhani kitaipeleka tanzania kwenye level ya juu kabisa ya teknolojia. kwa habari zaidi tembelea hapa
ESTA -TANZANITE CITY OF TECHNOLOGY & INNOVATION: MBEYA: FRIENDS CLUB OF THE TANZANITE CITY
Kila kitu kinawezekana cha msingi ni mikakati ya kufanikisha hiyo nia.
 
Una mawazo mazuri ila viongozi hawawazi ivo na hawashauriki sibiri wapite uje tena na hoja kama hii,,
 
Kutengeneza calculator tu tumeshindwa sembuse satellite hyo

OvA
 
Mataifa mengi hususani Africa yameanza kwa kasi urushaji wa Satellite angani katika karne hii kwa kurusha wenyewe au kushirikiana na mataifa kama Japan, Russia, Marekani n.k. Dunia ya sasa matumizi ya satellite ni muhimu sana kwa maendeleo ya nchi husika asa kwenye sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Matumzi ya satellite yanasaidia kuchukua taarifa za Duniani kwenye maswala ya uboreshaji wa kilimo, kijeshi, uchaguzi, afya, hali ya hewa na pia kupata taarifa kwa haraka zinazohusu vimbunga na matetemeko ili mamlaka zilizopo nchi hizo kutoa tahadhari za majanga kabla ya kutokea au serikali kujipanga kwa ajili ya kuchukua tahadhari.

Nchi za Africa ambazo zimeweza kurusha Satelite angani na matumizi yake ni kama ifuatavyo;_


· Misri

Misri wana satellite kama EgyptSat 1 na EgyptSat 2 ambazo wanazitumia kwa matumizi mbalimbali kwa ajili ya kuleta tija kwenye shughuli zao za uchumi. Mwaka huu 2017 wanapanga kurusha Satelite ya DesertSat kwa ajili ya ulinzi na usiamimizi wa maliasili zao ambazo zipo maeneo ya jangwani ili ziweze kuleta tija katika nchi yao.



· Africa Kusini

Afrika kusini wana satellite nyingi ambazo wamerusha toka mwaka 1999-2015. Sateliete ya Kondor-E waliirusha mwaka 2015 huwa wanaitumia kwa ajili ya matumizi ya kijeshi na Satelite nyingne nyingi kama SUNSAT, SumbandilaSat kwa ajili ya matumizi mbalimbali yanayoleta tija kwenye taifa lao n.k


· Morocco

Morocco pia wana satellite mbalimbali pia ifikapo Novemba 2017 watarusha satellite yao nyingine ambayo itatumika kwa shughuli za kijamii na kijeshi ambapo wametumia takribani Euro 500 Million kutaka kufanikisha hilo .


· Algeria

Algeria nao walianza tafiti na hatua za urushaji wa satellite toka miaka ya 2002. Algeria wana satellite zao kama Alsat-1B ambayo inatuamika kwa ajili ya uchukuaji taarifa katika maswala ya kilimo na taarifa za majanga kama vimbunga na matetemeko.

Alsat-2A wanaitumia kwa ajili ya upigaji picha za anga ambazo zinazotumika kwenye taasisi zao kama za kilimo, upimaji ardhi na mamlaka ya hali ya hewa.


· Nijeria

Wanaijeria wanazitumia sana Satellite zao kama SatX na Sat 2 ambazo zipo angani kwa ajili ya kufanya uangalizi wa vyazo vya mafuta kule Niger Delta, chaguzi mbalimbali kwa ajili ya ubainishaji wapiga kura na shughuri za kiusalama na kijeshi wakati wa kutafuta maficho ya Boko Haram pamoja na utafutaji wa watoto 273 waliotekwa kule Chibok mwaka 2014 zilitumika sana.



· Ghana

Mwaka huu 2017 Ghana wamerusha ya kwao inaitwa GhanaSat-1, ni satellite ndogo kabisa na ni satellite ya kwanza kurushwa nchini Ghana wakishirikiana na Mamalaka ya anga ya Japani JAXA (Japanese Aerospace Exploration Agency) imewaghalimu takribani Dola 50,000/=, wanaitumia kwa ajili ya upigaji wa picha za anga nchini Ghana.

MASWALI YANGU

Je Tanzania ina mikakati gani kuhusu au wazo la kurusha satellite angani kwa ajili ya matumizi kijamii na kiuchumi ili kuliletea tija Taifa letu ?

Je maproffesa wetu wanajipanga vipi kufanikisha hili?

Je Serikali inaweza kuweka bajeti ya kusomesha wadogo zetu kwenye Sayansi ya anga ili kuleta tija ya kufanikisha ndoto yetu ya kurusha hata satellite moja ndogo kama waliorusha wenzetu wa Ghana mwaka huu 2017 yenye Launch mass ya 1 Kilogramu(Kg)?

Je kuna fungu lolote huwa linatengwa kwa ajili ya tafiti za sayansi asa za anga ?


Klementos- Jamii Forum
Tutaweza atakapokufa yohana mvinyo.
 
Sidhani kwamba Kurusha satellite ndio kigezo cha maendeleo, tuangalie priorities zetu zitakazotuwezesha kupiga hatua kimaendeleo. Maana najua wenzetu walipitia hatua kadhaa za maandalizi mpaka wakafika hapo walipo, tufanye kazi kwa bidii na tuwe tayari kuumia katika harakati za kufika huko.......sio lelemama.
 
Dawa mahospitalini ni shida, halafu mnakuwa na mawazo ya kurusha sattelait....

Ngoja trafic waendelee kukusanya hela zikifika tutairusha
 
Sidhani kwamba Kurusha satellite ndio kigezo cha maendeleo, tuangalie priorities zetu zitakazotuwezesha kupiga hatua kimaendeleo. Maana najua wenzetu walipitia hatua kadhaa za maandalizi mpaka wakafika hapo walipo, tufanye kazi kwa bidii na tuwe tayari kuumia katika harakati za kufika huko.......sio lelemama.
Umeongea kweli mkuu, lakini Tanzania ina watu milioni 50, hawa watu wote wote tukiamua kugawana majukumu, hatuna sababu ya kusubiri, wanasiasa wafanye kazi yao kuhakikisha kuna haki na uwajibikaji, wanasayansi wafanye kazi zao kwa weledi, kujituma na ubunifu wa hali ya juu, wanaotaka kuunda satelites waunde, wanaotaka kuunda magari, meli, matrekta wote wafanye hivyo, mwisho wa siku tutajikuta tumekuwa kama Wenzetu walioendelea. Tusiogope kuota ndoto za mafanikio kwa sababu tu kuna watu watatuona mahayawani! Bila hiyo tutajikuta kila mtu anawaza kubeti, na mambo mengine yasiyokuwa ya msingi kwa taifa letu.
 
Katika umiliki wa anga kuna mipaka na vibali, sasa kuvipata hivyo vibali peke yake ni mtihani mkubwa maana kuna vibali vya kimataifa na vya kitaifa kwamba unaweza kupewa kibali ndani ya anga lako tu basi na sio anga la kimataifa kama marekani, japani, urusi na china hayo mataifa yana satellite katika anga za kimataifa ndio maana unaona wanabishana kuhusu nyuklia maana wanajua zilipo

Sasa nchi ulizozitaja kaka ni anga la kitaifa tu sio kimataifa maana hawawezi kukubali kimataifa maana huenda ukawa unatumiwa na maadui zao kupata habari zao hivyo wanakuwa na vikwazo ili usiweze kufikia hapo.

Lakini kuna mataifa kama Canada, chile nk wamejiunga kwenye satellite ya marekani ambapo wako chini ya uongozi wa marekani kupata habari za nchi zao
Hivyo TZ kama ikitaka inaweza kurusha kwenye anga la kitaifa tu hiyo inawezekana kama ambayo iko ghana au la sivyo ikaomba kuungwa kwa marekani japo ni ngumu maana tunaukaribu na maadui wa marekani hivyo hatutaaminika

Pointi ya kuwasomesha watu wetu nje ya nchi ili kuwa na wataalamu n pointi kubwa sana yenye mashiko makubwa sana na hilo viongozi wetu hawajaligundua

Satellite ni kitu cha muhimu sana ingetrack hata mienendo ya waliomshambulia lissu
Ingesaidia kujua madini na mafuta yako wapi, miamba, baharini kama kuna nyambizi zinaingia kinyemela au meli, mawasiliano nk yaani inasaidia sana

Mwaka 2014 kulitokea wachimba madini kufa kwenye migodi yaani walifukiwa na kifusi
Lakini satellite iliwaonyesha walipo na kuwaokoa

Tanzania bado sana tuwaze tu maisha haya haya ya kuwafuatilia wenye malengo na nchi ili wauwawe

Kama wasomi wananyanyasika na wanafunzi wanaonewa ni lini tutakaa sawa? Mawazo ya wenye maono yanafukiwa, sauti ya mwenye maono inazimwa, jitihada za wazalendo zinabomolewa
Bora ulale tu ndugu waza kula na kuvaa tu
 
Dawa mahospitalini ni shida, halafu mnakuwa na mawazo ya kurusha sattelait....

Ngoja trafic waendelee kukusanya hela zikifika tutairusha
Kwa hapa tulipo fika teknolojia na uchumi ni kama kuku na yai, kipi kinaanza na kipi kinafuata, usipokuwa dawa hospitali, afya itakuwa mashakani na huwezi kuwa productive, lakini pia usipokuwa na hizo teknolojia huo ichumi wa kukuwezesha kununua dawa pia ni shida kuipata. Lakini kwa nini tusigawane majumu serikali ikusanye kodi na kutoa huduma, wananchi tufanye kazi ya kuibua na kubuni teknolojia na kuanzisha viwanda, hii siyo kazi ya serilkali, kwa kuwa serikali inaongozwa zaidi na mahitaji ya kisiasa, hata hivyo hao wanasiasa wanatoka miongoni mwetu sisi wenyewe, tunachowaza sisi ndivyo hivyohivyo na wao wanawaza. Teknolojia mbalimbali zinazotamba duniani ni kazi za watu binafsi na si serikali japo serikali huchangia kuziendeleza kwa manifaa ya watu wao. Watanzania tunaweza tukiamua.
 
Katika umiliki wa anga kuna mipaka na vibali, sasa kuvipata hivyo vibali peke yake ni mtihani mkubwa maana kuna vibali vya kimataifa na vya kitaifa kwamba unaweza kupewa kibali ndani ya anga lako tu basi na sio anga la kimataifa kama marekani, japani, urusi na china hayo mataifa yana satellite katika anga za kimataifa ndio maana unaona wanabishana kuhusu nyuklia maana wanajua zilipo

Sasa nchi ulizozitaja kaka ni anga la kitaifa tu sio kimataifa maana hawawezi kukubali kimataifa maana huenda ukawa unatumiwa na maadui zao kupata habari zao hivyo wanakuwa na vikwazo ili usiweze kufikia hapo.

Lakini kuna mataifa kama Canada, chile nk wamejiunga kwenye satellite ya marekani ambapo wako chini ya uongozi wa marekani kupata habari za nchi zao
Hivyo TZ kama ikitaka inaweza kurusha kwenye anga la kitaifa tu hiyo inawezekana kama ambayo iko ghana au la sivyo ikaomba kuungwa kwa marekani japo ni ngumu maana tunaukaribu na maadui wa marekani hivyo hatutaaminika

Pointi ya kuwasomesha watu wetu nje ya nchi ili kuwa na wataalamu n pointi kubwa sana yenye mashiko makubwa sana na hilo viongozi wetu hawajaligundua

Satellite ni kitu cha muhimu sana ingetrack hata mienendo ya waliomshambulia lissu
Ingesaidia kujua madini na mafuta yako wapi, miamba, baharini kama kuna nyambizi zinaingia kinyemela au meli, mawasiliano nk yaani inasaidia sana

Mwaka 2014 kulitokea wachimba madini kufa kwenye migodi yaani walifukiwa na kifusi
Lakini satellite iliwaonyesha walipo na kuwaokoa

Tanzania bado sana tuwaze tu maisha haya haya ya kuwafuatilia wenye malengo na nchi ili wauwawe

Kama wasomi wananyanyasika na wanafunzi wanaonewa ni lini tutakaa sawa? Mawazo ya wenye maono yanafukiwa, sauti ya mwenye maono inazimwa, jitihada za wazalendo zinabomolewa
Bora ulale tu ndugu waza kula na kuvaa tu
Umefafanua vizuri sana kiongozi. Mi nadhani kumiliki satelite au kuanza kusomesha watoto wetu nje au kuanza tafiti za maswala ya anga si anasa, kuna faida nyingi tunaweza kupata ili kutuletea maendeleo katika nchi yetu .
 
mkuu ngoja tuwe na Radar za kutosha kwa ajili ya usafiri wa anga na maswala ya kijeshi
 
Back
Top Bottom