je ni madhara gani anaweza kupata mtoto anayenyonya maziwa ya mama ambaye ni mjamzito?

je ni madhara gani anaweza kupata mtoto anayenyonya maziwa ya mama ambaye ni mjamzito?

tafakari kali

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2012
Posts
211
Reaction score
39
Habari wana jamii f.

Naomba msaada wa swala hili, mimi na mke wangu tuna mtoto wa miezi 8,na kwa bahati mbaya mke wangu ameshika ujauzito mwingine, sasa sipo tayari kumwachisha mwanangu ziwa la mama yake kama hakuna madhara.

Sasa naomba kujuzwa endapo kuna madhara yoyote kwa mtoto kama ataendelea kunyonya maziwa ya mama yake na kama yapo basi naomba japo kinagaubaga nidadafuliwe nipate kujua ili niweze kufanya mahamuzi sahihi. natanguliza shukrani zangu.

NB; napenda maoni yatoke kwa watu wenye uhakika na wanachoniambia kwa sababu ni jambo muhimu sana kwangu.asante.
 
Wataalamu wanasema hakuna madhara yeyote yale, lakini nakushauri nenda hospital ukaonane na daktari mtaalamu na sio hawa madaktari wa kutibu malaria au hawa manesi wa kwenye dispensary..hao hawatkusaidia. Mwambie shem asitoehiyo mimba lakini next time awe makini asiwe anapenda tu utamu..ajue pia kuna kipindi cha kulea.
 
habari wana jamii f.

naomba msaada wa swala hili ,mimi na mke wangu tuna mtoto wa miezi 8,na kwa bahati mbaya mke wangu ameshika ujauzito mwingine,sasa sipo tayari kumwachisha mwanangu ziwa la mama yake kama hakuna madhara.sasa naomba kujuzwa endapo kuna madhara yoyote kwa mtoto kama ataendelea kunyonya maziwa ya mama yake na kama yapo basi naomba japo kinagaubaga nidadafuliwe nipate kujua ili niweze kufanya mahamuzi sahihi. natanguliza shukrani zangu.


NB; napenda maoni yatoke kwa watu wenye uhakika na wanachoniambia kwa sababu ni jambo muhimu sana kwangu.asante.

madhara yapo ila sijui ni yapi ila kwa uhakika zaidi nenda hospitali kaonane na daktari atakufafanulia vizuri
 
Pole sana kwa KUMBEMENDA MTOTO. Watoto wako wote 2 wa tumboni na kichanga lazma watakuwa na afya migogoro. Muone Dk yoyote au Mama wa makamu mwambie nifanye nini mke wangu KAMBEMENDA MTOTO. Pole sana na mue makini na tarehe. BILA SHAKA NYOTA KIJANI HAMUIJUI.
 
mkuu tafakari kali kitaalamu hakuna madhara ya kuendelea kumnyonyesha mtoto mkeo huko akiwa na mimba,ila tu unachotakiwa awe anakula balanced diet sababu mtoto wa ndani ya mfuko wa uzazi na huyu aliyezaliwa wote wanategemea lishe toka kwa mama.Hivyo akila vyakula vizuri itamsaidia kumudu mahitaji yao bila yeye mwenyewe afya yake kodhoofika.
.........Kwa vile kadri mimba inavyokuwa kubwa uzalishwaji wa maziwa unapungua ni vema ukaanza kumzoesha mtoto wako vyakula vingine,kwa umri huo anawezakuanza kula vyakula badala ya kutegemea maziwa ya mama.

.........Kwa ushauri mwingine mimba ikiwa imefika miezi mingi zaidi kuelekea kujifungua ni bora akamuachisha kunyonya kwa sababu maziwa yanabadilika kwa ajili ya mtoto atakayezaliwa haya yanaitwa colostrum ndiyo yale maziwa ya njano ya mwanzo mama hutoa.
 
hakuna madhara yoyote nakuhakikishia. mi nilipata ujauzito mwanangu akiwa na mwaka mmoja kamili. na nilimuona Dr. akaniambia nisimuachishe mtoto ghafla kunyonya sbb itamuathiri mtoto. cha msingi ni kula vzr tu. nilimnyonyesha mwanangu mpk mimba ilipofika 5 months. na nilikuwa nalala naye na namkumbatia km kawaida. hakuna cha kubemenda wala nini.


watoto wanaoathirika ni wale ambao mama akishajua kuwa ni mjamzito anamuachisha kunyonya na anakuwa hana ukaribu nae kwa kisingizio kwamba joto la mama litamuathiri mtoto. nilijifungua mwanangu akiwa na fya tele na huyu pia aliendelea vzr. cha msingi zidisha mapenz kwa mtoto kuna maudhi yale ya mimba jitahidi yasimdhuru mtoto. hongereni kwa kuto abort.
 
Wataalamu wanasema hakuna madhara yeyote yale, lakini nakushauri nenda hospital ukaonane na daktari mtaalamu na sio hawa madaktari wa kutibu malaria au hawa manesi wa kwenye dispensary..hao hawatkusaidia. Mwambie shem asitoehiyo mimba lakini next time awe makini asiwe anapenda tu utamu..ajue pia kuna kipindi cha kulea.

Acha dharau kijana..kwani manesi wa dispensary wanasomea wapi na hao madaktari wa kutibu malaria wanasomea wapi? Msaada unaweza kupata mahali popote bila kujali location na vile vile unaweza usipate msaada hata kwa hao unaowaamini sana.
 
mkuu tafakari kali kitaalamu hakuna madhara ya kuendelea kumnyonyesha mtoto mkeo huko akiwa na mimba,ila tu unachotakiwa awe anakula balanced diet sababu mtoto wa ndani ya mfuko wa uzazi na huyu aliyezaliwa wote wanategemea lishe toka kwa mama.Hivyo akila vyakula vizuri itamsaidia kumudu mahitaji yao bila yeye mwenyewe afya yake kodhoofika.
.........Kwa vile kadri mimba inavyokuwa kubwa uzalishwaji wa maziwa unapungua ni vema ukaanza kumzoesha mtoto wako vyakula vingine,kwa umri huo anawezakuanza kula vyakula badala ya kutegemea maziwa ya mama.

.........Kwa ushauri mwingine mimba ikiwa imefika miezi mingi zaidi kuelekea kujifungua ni bora akamuachisha kunyonya kwa sababu maziwa yanabadilika kwa ajili ya mtoto atakayezaliwa haya yanaitwa colostrum ndiyo yale maziwa ya njano ya mwanzo mama hutoa.

asante sana mkuu ,nimekuelewa sana . nimejaribu ku-google nimepata majibu yanayokaribiana na yako . thanks a lot man.
 
hakuna madhara yoyote nakuhakikishia. mi nilipata ujauzito mwanangu akiwa na mwaka mmoja kamili. na nilimuona Dr. akaniambia nisimuachishe mtoto ghafla kunyonya sbb itamuathiri mtoto. cha msingi ni kula vzr tu. nilimnyonyesha mwanangu mpk mimba ilipofika 5 months. na nilikuwa nalala naye na namkumbatia km kawaida. hakuna cha kubemenda wala nini.

watoto wanaoathirika ni wale ambao mama akishajua kuwa ni mjamzito anamuachisha kunyonya na anakuwa hana ukaribu nae kwa kisingizio kwamba joto la mama litamuathiri mtoto. nilijifungua mwanangu akiwa na fya tele na huyu pia aliendelea vzr. cha msingi zidisha mapenz kwa mtoto kuna maudhi yale ya mimba jitahidi yasimdhuru mtoto. hongereni kwa kuto abort.

asante sana kwa mchango wako ,nimepata nafuu sana maana ilishaanza kunichanganya. nimejaribu pia ku-goole nikapata majibu kuwa hakuna madhara jambo la msingi ni kuzingatia lishe ya mama kwan anakuwa anategemewa na viumbe wawili.
 
Pole sana kwa KUMBEMENDA MTOTO. Watoto wako wote 2 wa tumboni na kichanga lazma watakuwa na afya migogoro. Muone Dk yoyote au Mama wa makamu mwambie nifanye nini mke wangu KAMBEMENDA MTOTO. Pole sana na mue makini na tarehe. BILA SHAKA NYOTA KIJANI HAMUIJUI.

unaposema mke wangu kambemenda motto una maana gani, waone wataalam wa uzazi watakushauri vizuri ila sie kiukunga hutakiwa kuenelea kunyonyesha ukiwa mjamzito, mtotto anakua tu nt necessary anyonye maziwa ya mama
 
Kuna madhara gani kwa mtoto kunyonyeshwa hali yakuwa mama yake ni mja mzito?

Uswahilini nasikia mengi, naomba kupata uhakika katika hili!
 
Re: Swali kuhusu madhara ya mtoto kunyonya wakati mama akiwa mjamzito
Kuna siku nilikuwa namsikiliza mtaalamu akasema wakati wa ujauzito mtoto anaweza kuendelea kunyonya hadi miezi sita au saba. Ila kipindi ambacho mama amebeba ujauzitomwingine kunakuwa na mabadiliko ya homoni ambayo husababisha maziwa kuwa na virutubisho vingi na hivyo kusababisha mtoto anayenyonya kuweza kupatwa na tatizo la kuharisha, lakini ni kwa kipindi cha mpito tu yaani kipindi cha kushika mimba na baadae mtoto anaendelea kunyonya bila tatizo (kuna kasumba ya kusema mtoto amenyonya maziwa machafu ndo hicho kipindi cha mpito)
 
Hapa unaweza usipate majibu ndugu yangu mzaa mwingi,hayo maelezo nimeyatoa kwenye post moja ya siku nyingi humuhumu ila kwa sasa ingia google andika ujauzito au mimba na kunyonyesha utakutana na majibu mengi ya swali lako!
 
nguzi wa kitaalamu
unaonyesha kwamba hakuna madhara kwa
mwanamke kuendelea kumnyonyesha mtoto
mchanga iwapo atajikuta amepata ujauzito.
Hayo yamebainika wakati uchunguzi mwingine
unaonyesha kwamba asilimia 86 ya vifo vya watoto,
vikiwamo vya utoaji mimba, vinasababishwa na
wanawake wanaokwepa kulea ujauzito au
kuendelea kunyonyesha kwa fikra potofu kuwa
maziwa yamechafuka.
Hayo yamesemwa na Daktari Bingwa wa Magonjwa
ya Wanawake wa Chama cha Madaktari Wanawake
Tanzania (Mewata), Dk Caroline Mayengo kwenye
mahojiano na gazeti hili.
“Hakuna madhara yoyote kwa mama mjamzito
kuendelea kunyonyesha. Mtoto aliyeko tumboni na
mtoto mwingine ambaye bado ananyonya
wataendelea kukua vizuri,” alisema.
Alifafanua kuwa, iwapo mwanamke yeyote atabaini
amepata ujauzito wakati akiwa bado ana mtoto
mchanga ataendelea kumnyonyesha hadi mimba
itakapofikia umri wa miezi saba.
Ila ameonya kuwa mwanamke anayenyonyesha
huku akiwa ni mjamzito anapaswa kutunzwa vizuri
zaidi kwa kupatiwa vyakula bora vya kutosha ili
kujitunza binafsi na watoto anaowalea.
“Mtoto asiachishwe kunyonyeshwa kwa sababu
mama ni mjamzito… Hali ya utapiamlo ya mama
ndiyo inaweza kumwathiri mtoto lakini kama
anapata chakula cha kutosha hakuna madhara,”
alisema Dk Mayengo.
Kuhusu vyakula, alisema mama mjamzito anapaswa
kula vyakula vyote muhimu vikiwamo vya vitamini,
madini na vya protini kwa ajili ya kujenga mwili na
madini mbalimbali mwilini.
Alisema kitaalamu inashauriwa mtoto mmoja
anapozaliwa hadi kupata mimba ya mtoto wa pili
angalau wapishane kwa miaka miwili.
“Kama mama akibeba mimba nyingine chini ya
miaka miaka miwili(care)utunzaji wa mtoto
mwingine unakuwa si kubwa sana na ukiangalia
watoto wanaokufa utakuta mama zao wana watoto
wengine wachanga,”alisema.
Alisema kumekuwa na kupishana kwa watoto
ambako hakuendani na taratibu za kiafya hivyo
alishauri watu kutumia huduma za uzazi wa mpango
ili kutoa nafasi kati ya mtoto mmoja hadi mwingine.
Hata hivyo alisema baadhi ya watu wamekuwa
wakieneza mitazamo hasi juu ya uzazi wa mpango
wakati ukweli ni kwamba manufaa ni mengi.
1 | 2 Next Page»
Je, sababu hizi zinatosha kuiangusha
Ukawa 2015?
1 comment • 3 days ago
Avat revocatus — Jibu ya swali hili ni
HAPANA kwa sababu Viongozi wa
vyama vya siasa wamethubutu na
wameunganishwa kwa jambo …
MAONI: Mradi ‘Vitambulisho vya Kura’
unatia shaka - Maoni - …
4 comments • 3 days ago
Avat Mzalendo — Hongera mwariri kwa
kuthubutu. Ila Mwariri hakutupa
mifano wa nchi ambazo zilitumbukia
katika matatizo kwa kutumia BVR …
BRAZIL 2014: Mambo sita
yatakayokushangaza - Michezo - …
2 comments • 3 days ago
Avat Dennis Ogutu — Hii ni hali ambayo
Watanzania waige.
Bajeti Kuu yapita gizani, Mkuya atema
cheche
4 comments • 3 days ago
Avat Dennis Ogutu — Sawa kabisa Waziri
waFedha inabidi watu watozwe kodi
ALSO ON MWANANCHI SITE
0 Comments Mwananchi Site Login d
Sort by Best Share ⤤
Be the first to comment.
WHAT'S THIS?
Subscribe ✉ Add Disqus to your site d
Favorite ★
Kp Mei Kipanya
April Kp Machi
powered by Visit worldcup
site
BRAZIL 2014: Algeria yapania kulipa
kisasi 1982
Wanachama Simba chali
Maximo amleta Coutinho Yanga
MAONI: Tusipokuwa makini utamaduni
utapotea
UKATILI: Baba abaka bintiye,
amwambukiza Ukimwi
Waziri wa Fedha Zanzibar amshikia Raza
bango la kodi
Dar hatarini kwa unga wa lishe, visima vya
maji
Watumiaji wa huduma za kibenki
waonywa
USAFIRI: Sumatra yaiamuru Uda
kushusha nauli
Dk Salim apongezwa
Vita ya Werema, Kafulila yakolea
Dk Salim: Sina mpango na urais 2015
Werema nusura ampige Kafulila
Mtawa aagwa, dereva asimulia
Msekwa atoboa siri ya CCM
kung’ang’ania serikali mbili
Ada vyuo vya ualimu juu
Katibu: Bila Ukawa hakuna Katiba Mpya
Mabilioni yapelekwa nchini India
Wanachama 34 CUF wawakataa Seif,
Lipumba
Kisumo: Baraza la Mapinduzi Z’bar
limeuawa kimyakimya
MVUTANO: Werema, Maswi, Kafulila
ngoma nzito
Kp Juni
Email Privacy Policy Wasiliana nasi RSS
MCL Blog | Daily Nation | NTV | Business Daily |
The East African | Daily Monitor | KFM |
Mwanaspoti | The Citizen | Nation Media Group
Juni 28, 2014
false
false
 
Back
Top Bottom