Uchaguzi 2020 Je, ni nani alikuwa nyuma ya biashara ya waunga juhudi? Je, imemlipa ama kala hasara kubwa?

Uchaguzi 2020 Je, ni nani alikuwa nyuma ya biashara ya waunga juhudi? Je, imemlipa ama kala hasara kubwa?

Hii biashara ilikuwa ya Mr. Magufuli na Pole pole huku wakitumia fedha za ofisi ya rais ambazo kwa sasa CAG haruhusiwi kuzikagua.

Sasa, sawa na biashara zingine kwa kweli haikuleta matokeo yaliyokusudiwa na ni hasara kubwa kwa walioiasisi.

But what can they do now, it was the ultimate gamble designed to eliminate the opposition to easily pave the way for the incumbent president to change the constitution to enable him to stay in power indefinitely.
 
Nasubiri maamuzi ya wajumbe WA uchaguzi mkuu WA rais ,wabunge na madiwan tar 28 Oct 2020.maana wajumbe Sikh hiz hawatabirik
 
Mungu awasamehe bure waliounga juhudi..malipo ni hapa hapa duniani na adhabu zingine huwa zimo kwenye kitendo ... Hawakujua walitendalo , ila waliowaingiza mkenge walijua bila kujua ya kesho... Ndo hasara ya kufanya biashara pasipo kufikiri kwa kina.
Kuna UKAKASI katika statement yako.... moja katika nchi huru na haki/uhuru wa Binadamu kufanya chochote anachokiona sawa kwake sioni kosa au kuwashupalia wale waliofanya maamuzi hata kama kwa upeo wetu maamuzi hayo ni ya kipuuzi

Pili unavyosema kufanya biashara (mentality hii ya hata sisi wapiga kura kukubali kwamba siasa, au kuwapa kura wawakilishi wetu watuwakilishe ni biashara na sio utumishi...) ni kwamba tumekubaliana na kuona ni sawa huu upuuzi unaofanyika
 
Ila madalali wamefaidi sana tu aaaaiiisseee! Yaaani mkuu wa mkoa anamnunulia bmw mkewe zawadi ya birthday!!!! Brand New kabsa wanachana nylon kwenye seat
[emoji44][emoji44][emoji44][emoji44][emoji44][emoji848][emoji848][emoji848][emoji2827][emoji2827][emoji2827]
 
Waliobuni mradi wa kununua wapinzani lazima walikuwa ni watu wenye akili ndogo sana. Hawakuwa na uwezo wa kuyaona mambo kwa mbele.

KILICHOPO

Ununuzi wa wapinzani haujaleta matokeo waliyoyatarajia. Kitu ambacho hawakukijua ni kuwa wengi wa walionunuliwa walikuwa viongozi kwa sababu tu wananchi walitaka mabadiliko, na hao viongozi wala hawakuwa sababu ya wananchi kutaka mabadiliko. Walinunua matokeo bila kugusa kisababishi. Uwezekano mkubwa ni kwamba majimbo yote yaliyokuwa ya wapinzani, yatarudi tena upinzani.

Walionunuliwa walikuwa wanajua kuwa wao si chochote ndani ya majimbo yao. Kwao kununuliwa kulikuwa na faida mbili. Moja, watapata fedha. Pili, waliamini mfumo wa demokrasia unafikia mwisho, demokrasia inauawa, hivyo ni vema kuungana na muuaji wa demokrasia ili waendelee kuwepo kwenye siasa bila ya kujali watakuwepo kwenye saisa za mfumo gani. Waliangalia zaidi maslahi binafsi.

MATOKEO

1) Majimbo yaliyokuwa ya upinzani yanarudi tena upinzani

2) Walionunuliwa toka upinzani hawatakuwa wagombea kupitia chama chochote, na Mwenyekiti wa CCM akilazimisha wawe wagombea, kutaleta mtafaruku na chuki kubwa ndani ya CCM kiasi cha baadhi ya wanaCCM kupigia kampeni upande wa pili kwa siri na kwa uwazi.

3) Wachache walionunuliwa na kupitishwa na CCM kuwa wagombea, hawatashinda kwenye kura za wananchi.

MAHESABU

Mradi wa CCM wa ununuzi wa wapinzani umekuwa na hasara kwa CCM na kwa walionunuliwa. Hakuna hata mmoja kati yao aliyepata faida. Ni mradi uliobuniwa na watu wenye IQ ndogo, utekelezaji ukasimamiwa na wenye upeo duni, ukashangiliwa na wajinga wengi. Umetoa funzo kubwa kwa wenye akili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Biashara imefeli na mtaji umeliwa 😂😂😂😂
Kwa CCM mission accomplished................wameweza kupunguza imani ya wananchi kwa wapinzani.............kwa namna walivyokua wananunuliwa yale majimbo yote ya wapinzani waliounga juhudi effect lazima zitaonekana
 
. Ni mradi uliobuniwa na watu wenye IQ ndogo, utekelezaji ukasimamiwa na wenye upeo duni, ukashangiliwa na wajinga wengi. Umetoa funzo kubwa kwa wenye akili
emoji87.png
emoji848.png
emoji848.png
emoji848.png
emoji2827.png
emoji2827.png
emoji2827.png
emoji2827.png
emoji28.png
emoji28.png
emoji28.png
 
Kwa CCM mission accomplished................wameweza kupunguza imani ya wananchi kwa wapinzani.............kwa namna walivyokua wananunuliwa yale majimbo yote ya wapinzani waliounga juhudi effect lazima zitaonekana
Sidhani...kwa kile walichofanya wajumbe sidhani
 
Hiii biashara iliasisiwa na baba na mwana( Cha zero),mtoto alikuwa anaratibu ununuzi kwa bei kubwa sana,huku akimdanganya baba yake kuwa atasambalatisha upinzani wote nchini. Na kila aliyempinga baba yake hadharani au kwa kificho alitishwa na Kama alikaidi alipotezwa( r.i.p Ben Saanane),kwa sababu mtoto nicha zero akawa anatumia hovyo vyombo vilivyo chini ya ofisi ya baba yake(tiss) kutekeleza utekaji na utesaji,na badae maiti kuokotwa Coco Beach, wakashindwana na Makungu aliyekuwa naibu Mkurugenzi wa tiss,ikabidi Makungu ahamushiwe Tabora kuwa Ras. Mradi wa waunga juhudi kadri ulivyokolea BASHITE ndo kadri alivyozidi kubadili magari ya kifahari,kelele zikawa nyingi mradi ukarasimishwa rasmi Lumumba( kwa watu wachache)wakaujua wakausimamia,muulizeni baba Levo alifatwa akachomoa,pamoja na mbunge wa kilwa( Bwege). Bashite akabaki na jukumu moja tu lililoendelea kumfanya awe na bond na baba yake wa kufikia na jukumu hilo ndilo ambalo Pompeo aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa CIA na Sasa waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani aliiambia dunia kuwa Bashite ananyima watu haki ya kuishi ( IN OTHER WORDS BASHITE NI MUUWAJI).
Wamarekani wanavyopenda kuingilia cases kama hizi kwenye mataifa mengine, now wanaendelea kukusanya ushahidi tu. Siku utashangaa file linakuwa disclosed na mpaka waliokuwa wanamwagiza na kiasi cha pesa alichokuwa akikabidhiwa kitatajwa.
Hapo ndipo patakapokuwa patamu, kumbe kwa njia nyingine watu wanaichafua madhabahu unapofika muda wa kutubu wanalia haswa dhamira zikiwachoma ila madaraka yanapofusha
 
Sidhani...kwa kile walichofanya wajumbe sidhani
Wajumbe hawana shida............shida ipo kwa wapiga kura maana watu walioawaamini wakajiuza wataamini tena wachague wa upande ule ule halafu waje kununuliwa tena??? Kwa CCM naona hii ilikua planned kwa sababu maalum
 
M
Kwenye biashara yoyote usipokuwa makini unaangukia pua na kupata hasara kubwa..lakini si biashara tu tunakosea na kupatia mengi maishani mwetu kuanzia kwenye elimu,siasa,ajira mpaka mahusiano

Ukikosea binafsi unaweza kujiadhibu ama kujisamehe mwenyewe lakini vipi kama ukikosea kitaasisi?kwa hakika sheria itachukua mkondo hasa kwa mambo yale yaliyo rasmi.

Kwenye harakati hizi za siasa kama chama cha siasa kisipofuata taratibu na kanuni...mfumo huvurugika na matokeo yake kufanya mambo ambayo hata likitokea kosa ni vigumu kuwajibishana.

Mwaka 2018 ilianza biashara ya siri ya kununua viongozi wa upinzani katika kada mbalimbali..ni wazi lengo lilikuwa kuvuruga na pengine kuusambaratisha upinzani walioasisi mpango huo wakidhani upinzani ni viongozi wakatenga bajeti ya kueleweka kwa ajili ya kutimiza huo mradi

Bajeti hiyo na mradi huo havikuwa rasmi ndani ya chama na kwa hisia za wengi hilo lilikuwa jambo la wachache na pengine kwa maslahi yao binafsi bila kutafakari ya mbeleni

Hakuna biashara inayokosa dalali ama mtu wa kati duniani...HAKUNA....Hii ni ajira inayoendesha maisha ya wengi....chochote kikishakuwa biashara ni ngumu kuepuka dalali labda tu iwe ni moja kwa moja kati ya muuzaji na mnunuzi

Kwenye siasa pia kuna madalali hasa pale siasa inapogeuka biashara..madalali wa kisiasa ndio waliochombeza kwa karibu na kusimamia zoezi zima la biashara ya waunga juhudi

Leo ile biashara ya siri iko upenuni peupe..badala ya faida mradi umekula hasara kubwa lakini huku madalali wakivimbiwa percent !!! Kwakuwa haikuwa biashara rasmi na ya wazi hivyo tunawajibishana chini kwa chini na kisirisiri.

Halisi kamwe haiwezi kuongozwa na bandia leo ule wimbo maarufu wa waunga juhudi na tafrija za mapokezi hatuvioni tena na vimeshazikwa kwenye makaburi ya sahau..waunga juhudi wale waliokuwa na tambo za kila aina sasa wamekuwa kama wendawazimu ndio sasa wanajua nini maana ya ile methali ya Waswahel. Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti.

Fundisho hili gumu na muhimu tunalipata katika awamu hii na uwekezaji huu ulioshindwa na kutia hasara kubwa huku mwananchi akikosa huduma muhimu.Sasa ni wakati wa kuadhibu.

Adhabu ya kwanza ni kwa wale waliorubuniwa almaarufu kama waunga juhudi.

Adhabu ya pili ni kwa warubuni..hawa kiama chao ni kwenye sanduku la kura.
Makubaliano ya awali ndiyo siri ingawa ya watu wengi,lakini wanapomaliza kuunga mkono juhudi hewa,wameliingiza Taiga hasara ya kurudia chaguzi zilizokuwa na maigizo kulikoni Comedy. Watu waliruka sarakasi,usipime.Niliyaona pale Duka Bovu kwa late kalanga,kuna Mbunge moja wa CCM Mpya toka Mbulu aaah.Huyo jamaa ni Acrobat,kitambi hakikuwa kikwazo cha kubinuka kwake.
Leo Kalanga hawezi itisha mkutano hata wa kitongoji chake,hana tena ile bashasha ya kuunga mkono juhudi za Jiwe.
Gharama za chaguzi hizi tulibeba Watanzania kupitia Force Account sawa na miradi mingine ya Ujenzi wa Vituo vya Tiba.
 
M
Makubaliano ya awali ndiyo siri ingawa ya watu wengi,lakini wanapomaliza kuunga mkono juhudi hewa,wameliingiza Taiga hasara ya kurudia chaguzi zilizokuwa na maigizo kulikoni Comedy. Watu waliruka sarakasi,usipime.Niliyaona pale Duka Bovu kwa late kalanga,kuna Mbunge moja wa CCM Mpya toka Mbulu aaah.Huyo jamaa ni Acrobat,kitambi hakikuwa kikwazo cha kubinuka kwake.
Leo Kalanga hawezi itisha mkutano hata wa kitongoji chake,hana tena ile bashasha ya kuunga mkono juhudi za Jiwe.
Gharama za chaguzi hizi tulibeba Watanzania kupitia Force Account sawa na miradi mingine ya Ujenzi wa Vituo vya Tiba.
Aliyekuwa Mbunge wa Monduli, Julius Kalanga akamatwa na kikosi kazi kwa madeni
 
Ahahhaha kaka Mshana Jr umejaribu sana kusokota maneno umetumia sitiari kwa umakini kaka, siku hizi umekuwa sana kiuandishi.
 
Aliyekula hasara ni wale waunga juhudi ambao pengine hata dau waliloahidiwa hawajapewa lote na wajumbe wamefanya yao.
Ccm hawana hasara sababu hatumii pesa zao za mfukoni ila ni kodi ya watanzani ndio wanajivunia ujinga
 
Biashara ile ilikuwa ni mradi halali ya mpangaji mkuu bila idhini ya wenye nyumba hivyo ilifanyika kwa siri bila ridhaa na mwisho ikawa ngumu sana kutakatisha faida aliyoipata kutokana na kuwa wenye mali hawakushirikishwa na mradi umekufa kimya kimya ili kwenda na wakati
Pesa ya manunuzi ilitokea mfuko gani?Au ni pesa walionyanganywa watuhumiwa wa kifisadi?
 
Kwenye biashara yoyote usipokuwa makini unaangukia pua na kupata hasara kubwa, lakini si biashara tu tunakosea na kupatia mengi maishani mwetu kuanzia kwenye elimu, siasa, ajira mpaka mahusiano.

Ukikosea binafsi unaweza kujiadhibu ama kujisamehe mwenyewe lakini vipi kama ukikosea kitaasisi? Kwa hakika sheria itachukua mkondo hasa kwa mambo yale yaliyo rasmi.

Kwenye harakati hizi za siasa kama chama cha siasa kisipofuata taratibu na kanuni, mfumo huvurugika na matokeo yake kufanya mambo ambayo hata likitokea kosa ni vigumu kuwajibishana.

Mwaka 2018 ilianza biashara ya siri ya kununua viongozi wa upinzani katika kada mbalimbali, ni wazi lengo lilikuwa kuvuruga na pengine kuusambaratisha upinzani walioasisi mpango huo wakidhani upinzani ni viongozi wakatenga bajeti ya kueleweka kwa ajili ya kutimiza huo mradi.

Bajeti hiyo na mradi huo havikuwa rasmi ndani ya chama na kwa hisia za wengi hilo lilikuwa jambo la wachache na pengine kwa maslahi yao binafsi bila kutafakari ya mbeleni.

Hakuna biashara inayokosa dalali ama mtu wa kati duniani, HAKUNA. Hii ni ajira inayoendesha maisha ya wengi, chochote kikishakuwa biashara ni ngumu kuepuka dalali labda tu iwe ni moja kwa moja kati ya muuzaji na mnunuzi.

Kwenye siasa pia kuna madalali hasa pale siasa inapogeuka biashara, madalali wa kisiasa ndio waliochombeza kwa karibu na kusimamia zoezi zima la biashara ya waunga juhudi.

Leo ile biashara ya siri iko upenuni peupe, badala ya faida mradi umekula hasara kubwa lakini huku madalali wakivimbiwa percent! Kwakuwa haikuwa biashara rasmi na ya wazi hivyo tunawajibishana chini kwa chini na kisirisiri.

Halisi kamwe haiwezi kuongozwa na bandia leo ule wimbo maarufu wa waunga juhudi na tafrija za mapokezi hatuvioni tena na vimeshazikwa kwenye makaburi ya sahau, waunga juhudi wale waliokuwa na tambo za kila aina sasa wamekuwa kama wendawazimu ndio sasa wanajua nini maana ya ile methali ya Waswahel. Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti.

Fundisho hili gumu na muhimu tunalipata katika awamu hii na uwekezaji huu ulioshindwa na kutia hasara kubwa huku mwananchi akikosa huduma muhimu. Sasa ni wakati wa kuadhibu.

Adhabu ya kwanza ni kwa wale waliorubuniwa almaarufu kama waunga juhudi.

Adhabu ya pili ni kwa warubuni, hawa kiama chao ni kwenye sanduku la kura.

Kinachoniuma ni upoteaji wa mamilion ya fedha za wananchi kuwanunua wanasiasa kumbe fedha zile zingetumika kuwaongezea wakandarasi wanaojenga barabara ya morogoro eneo la mbezi Luis na daraja la Sinza Mugabe shekilango road, wakandarasi hao wangeweza kujenga usiku na mchana ili kuwahi kumaliza ujenzi na kuwapunguzia shida ya foleni wanayoipata wananchi kwa sasa.
 
Back
Top Bottom