Je, ni sahihi kwa Mwana FA kujiita Gwiji wakati Fatuma Binti Baraka na fahari zake zote mpaka umauti unamfika hajawahi jiita gwiji?

Diamond hata akifulia hawezi ishi kama shetani. Nadhani zamani mziki ulikuwa haulipi, afadhali sasa hivi mtu anaweza jenga hata kibanda
 
Ugwiji wake bi kidude ulimsaidia nini? Niliona kama vile anaishi maisha ya chini sana..nikosolewe kama nilichosema sio sahihi
Ugwiji katika fani ni jambo moja na kuwa na maisha mazuri ni jambo lingine.

Ubora wake kwenye fani utaendelea kukubali kwa miongo kadhaa.

Ni kweli aliishi maisha ya chini na Ugwiji wake wa muziki haukumsaidia kuwa na maisha ya kitajiri.

Wanamuziki wengi wa miaka ya nyuma hawakupata maisha ya kitajiri kama wa sasa ni kwa sababu muziki wa sasa umekuwa wa kibiashara zaidi kuliko wa miaka ya nyuma.
 
Sawa mkuu umeeleweka. Nadhani wasanii wa sasa wana afadhali kidogo kwenye mapato
 
Hapo umedhihilisha ww umemjua bibi kidude akiwa kazeeka. Nyimbo zake nyingi unazozisikia kwenye audio vision sio kwamba aliingia studio akaanza kurekod bali zilirekodiwa akiwa jukwaani anaperform
 
Wewe acha ata ajiite mwajuma.
 
Acha tu ajiite hvyo wapo wenzake wanajiita had majina ya wanyama lakin ukiwaangalia uoni ata hizo sifa za majina yao
 
Braggadocio is part of hip hop.

 
Sawa mkuu umeeleweka. Nadhani wasanii wa sasa wana afadhali kidogo kwenye mapato
Umesema kweli.

Wasanii wa sasa wanapata Pesa zaidi ya wa zamani.

Vijana wengi wanakimbilia huko kwa ajili ya kutoka kimaisha wanajua pesa ipo.

Muziki wa sasa ni Biashara kwanza burudani baadae.

Zamani Muziki ulikuwa Burudani zaidi na kugangia maisha kidogo.
 
Ni sawa tu wasipokupa sifa jipe mwenyewe.
And if a man wants to be called Muhammad Ali, Goddamit, this is a free country, you should respect his wishes, and call the man Muhammad Ali! Morris - Coming to America
 
Uko sahihi sana.
 
wacha utani ni Sawa na Leo kumchukua Jide akashindane na kina Zuchu
 
Ashawahi jiita "Michael scoefield wa bongo"[emoji1] baada ya Michael scoefield wa marekani kukumbwa na scandal ya ushoga akaacha kujiita

Pia ashawahi jiita FAscobar yaani alijipa undugu na Pablo Escobar Gaviria .(nafikiri baada ya kuzitembela mkwanja wa yule don aliefungwa marekani)[emoji1]

So usiumie Sana

Majina yote makali ,ya kibabe babe ni yake so we chill tu

Atakuja lingine very soon[emoji1][emoji1][emoji12]
 
Kujiita jina kuna dhambi gani jameni.

Hivi hata kila Mtu akitaka kujiita Raisi si anajiita tu?...mwishi wa siku Wananchi ndio waamuzi wa mwisho, wakiridhika na umahiri wako basi watakupa jin linalokufaa kama kina "Golden Boy" Zamoyoni Mogela, "Jabali la Muziki" Marijani Rajabu n.k.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…