Je, ni sahihi kwa starlet yenye cc1300 kutembea kilomita 8 kwa lita moja ya petroli?

Wataalamu naombeni jibu maana nahisi iinakula sana wese. nikitumia harrier inakula lita 4 kwa 40km, starlet si ndogo ya harrier?
1. Weka mafuta ya taa 1/4l kwenye engine. Badala ya mafuta ya taa unaweza kutumia engine flush
2. Washa gari yako na iache silence kwa dakika 10 au 15
3. Mwaga engine oil yote
4. Fungua sample na isafishe vizuri kwa kutumia mafuta ya taa
4. Baada ya kuisafisha sample irudishie na ifunge vizuri
5. Funga oil filter mpya
6. Weka oil mpya hasa castrol kwenye engine
7. Funga plugs mpya -ziwe original
8. Badilisha fuel filter kwa kuweka mpya
9. Badilisha air filter/cleaner
10. Hakikisha distributor iko set properly
11. Weka petrol -hasa ya total energy
12. Anza kupiga misele
13. Usipopata 20km/l nipeleke kwenye mahakama ya wahujumu uchumi
 
asante sana mkuu, ubaya mafundi wetu hawa maneno mengi wanafanya kazi kwa mazoea na haya mambo yanahitaji ujuzi.
nitamsimamia afanye hizo step.
 
Wataalamu naombeni jibu maana nahisi iinakula sana wese. nikitumia harrier inakula lita 4 kwa 40km, starlet si ndogo ya harrier?
Mzee achana na hivi vigari vidogo havifai mafuta vinakula mpaka unashangaa hata kama kina engine ndogo ya 1000cc
 
Mkuu hii Elimu nimeichukua Itanisaidia. Kwenye hizi gereji za akina fundi Maiko huu ujuzi hawana. Wanatudanganya tu.
 
Fundi alikiosha osha nikaweka lita 42 nimetembea km 708 kutoka dar hadi arusha bado nazunguka nacho.
Nimeweka dumu la mafuta kwenye buti. mpaka kizime ndo ntaongeza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…