Je, ni sawa kuchangisha michango ya harusi kabla ya Kupata mchumba?

Je, ni sawa kuchangisha michango ya harusi kabla ya Kupata mchumba?

Rabbon

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2022
Posts
21,625
Reaction score
33,688
Salaam,Shalom!!

Ndugu mmoja akapita Kwa jamaa zake katika eneo alilokuwa akifanyia biashara, akawashirikisha kuwa amepata mchumba na ataoa hivi karibuni, hivyo anaomba michango Kutoka Kwa wadau.

Jambo Hilo likawa kheri masikioni mwa Rafiki zake. Ndugu huyo, akachangisha michango pesa nyingi sana na kuahidi kuleta kadi ya harusi Kwa wote waliochangia.

Ilipobaki wiki Moja kabla ya tarehe ya harusi ndugu muoaji aliyoahidi wachangiaji, alisafiri na kupotea kusikojulikana Kisha akaja kuonekana baada ya miezi miwili kupita,

Alipohojiwa kuwa kwanini hakuleta kadi za harusi Kwa wachangia harusi kama alivyoahidi, alijibu kimkato kuwa mchumba alibadili maamuzi hivyo ndugu muoaji akaamua kutumia pesa aliyokusanya kama michango kuongeza mtaji wa biashara yake.

Kwa kuwa wachangiaji, hawakulazimiashwa Kutoa michango, waliishia kuguna na kufyonza na kununa!!!

Nakifananisha kisa hiki na watia nia wanaokusanya michango ilhali " UCHAGUZI"Bado.

Cc: Lucas Mwashambwa na johnthebaptist

Karibuni🙏
 
Jimbo la Tuliii pia ameanza compaign, ichapishwe pia fomu Moja pekee!!
 
Safi, nimeipenda akili ya jamaa. Kwann utumie mamilioni kwenye ujinga unaoitwa sherehe ya harusi wakati una biashara inahitaji mtaji na fursa ya mtaji unao 😂
 
Safi, nimeipenda akili ya jamaa. Kwann utumie mamilioni kwenye ujinga unaoitwa sherehe ya harusi wakati una biashara inahitaji mtaji na fursa ya mtaji unao 😂
Kwani angeomba achangiwe mtaji Si angefanikiwa, kulikuwa na ulazima Gani kuhadaa watu?
 
Kwani angeomba achangiwe mtaji Si angefanikiwa, kulikuwa na ulazima Gani kuhadaa watu?
Hakuna kitu kama hicho, hakuna mbongo atakayekupa pesa ya mtaji ila ukimwambia ujinga ujinga mwngn anakupa pesa chap tuu na ndio akili ya jamaa yetu alipoitumia.
 
Hakuna kitu kama hicho, hakuna mbongo atakayekupa pesa ya mtaji ila ukimwambia ujinga ujinga mwngn anakupa pesa chap tuu na ndio akili ya jamaa yetu alipoitumia.
Hilo Lina UKWELI,

Kuna wengine walimchangia kwenye kikundi Hadi ml 200 Eti Ili waje kulewa chakari siku ya harusi wakaambulia patupu!!
 
Back
Top Bottom