LGE2024 Je, ni sawa kwa Viongozi wetu wa Mtaa kututoza pesa ili watupigie mihuri kwenye shida zetu?

LGE2024 Je, ni sawa kwa Viongozi wetu wa Mtaa kututoza pesa ili watupigie mihuri kwenye shida zetu?

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Rabbit au Rubbish utajua utakapochajiwa 2000/3000/5000 na lazima utoe bila hivyo karatasi yenyewe yenye muhuri haupewi sio hapo TU hata ukienda mahakamani shughuli ni hio hio lazima ulipie muhuri na Saini
Mahakamani inatakiwa upewe risiti unapopata huduma ya notary public.
 
Swali moja hua unaulizwa umeishia hapa kwa muda gani? Km ni chini sana ya umri wako lazima wakuchaji kimfano una miaka 30 unaulizwa umeishia hapa kwa mda gani ukisema miaka yote 30 hawana tatizo na wewe unapigiwa bure ukisema miaka 2 au 3 wewe unaonekana wa kuja lazima uchajiwe tu na kweli lazima ikutoke maana huna namna
Huwez kudanganya kwamba umeishi eneo hlo miaka yote 30 wakati huyo kiongozi kaongoza huo mtaa kwa miaka zaidi ya 20, kwa hyo huwez kudanganya kwa sabab ye anawajua wakaz wake WALIOZALIWA HAPO almost wote.
 
Na hili agizo la Jerry Slaa kutaka hao viongozi wa mitaa wasitumike kwenye mchakato wa mauziano ya ardhi itasababisha hiyo mihuri wagonge hata kwa 50K.

Maana mrija nuo umekatwa!
Kwan hlo ni tamko au sheria kamili?? Mana hii nchi ina matamko kibao afu ukifika pale ofcn ukiwa man to man yaan ww na mhudumu anakwambia "hlo ni tamko la kisiasa"
 
Huwez kudanganya kwamba umeishi eneo hlo miaka yote 30 wakati huyo kiongozi kaongoza huo mtaa kwa miaka zaidi ya 20, kwa hyo huwez kudanganya kwa sabab ye anawajua wakaz wake WALIOZALIWA HAPO almost wote.
Kwa hio lazima ulipie tu hauna namna hata mahakamani wanachaji kupiga muhuri Ila ukiwa wa hapo hapo huchajiwi hata 100 mbovu wewe unavuta muhuri unagonga unapelekwa kwa Muheshimiwa anatia Saini akiona ni ya kwako hakuombi hata 100 nyeusi kwa hio wakuja lazima wachajiwe inabidi uelewe inamaanisha nini
 
Na hili agizo la Jerry Slaa kutaka hao viongozi wa mitaa wasitumike kwenye mchakato wa mauziano ya ardhi itasababisha hiyo mihuri wagonge hata kwa 50K.

Maana mrija nuo umekatwa!
Siyo agizo lake bali kisheria hawatambuliki wala siyo kazi yao. Ukienda mahakani na document ya mauziano ya ardhi iliyosimamiwa na kiongozi wa mtaa haitatambulika. Hii ni sheria ya siku tangu zamani japo ni watu wengi walikuwa wanawatumia bila kujua. Na pia huyo Jerry hana mamlaka ya kutoa agizo la namna hiyo.
 
Mahakamani inatakiwa upewe risiti unapopata huduma ya notary public.
Ndio risti unapewa Ila zingine sio lazima risti zinapita juu kwa juu tu, mchezo umeishia hapo
 
Rabbit au Rubbish utajua utakapochajiwa 2000/3000/5000 na lazima utoe bila hivyo karatasi yenyewe yenye muhuri haupewi sio hapo TU hata ukienda mahakamani shughuli ni hio hio lazima ulipie muhuri na Saini
Mnakubali huo ujinga ndio maana dhuluma na rushwa haziishi
 
Huelewei maana ya kujitolea, ukijitolea haupangi utalipwa nini au kiasi gani, unayemhudumia ndio anaamua.
Yoda zipo kazi za kujitolea lakini huambatana na motisha wa kazi ndani yake. Motisha kama huu unaweza kuwa haupo bayana kutokana mazingira ya kazi husika.

Lakini kwa malipo ya mishahara huainishwa wazi katika mkataba wa kazi ambao muajili anaingia na muajiliwa wake. Nahisi katika hili ni wewe ambaye hulitambui vizuri
 
Ni kweli maeneo mengi huwa inafanyika kinyume na Sheria.

Na huu ni udhaifu wa kimfumo.

Ilitakiwa hawa wenyeviti walipwe hata kama wamegombea wenyewe.

Mbona Diwani analipwa, Mbunge analipwa, waziri na Rais analipwa na wao si wachaguliwa?

Kwanini huyu Mwenyekiti wa mtaa asilipwe na ndiye anaeweza kuwa anafanya kazi nzito katika mazingira magumu yasiyo na nyenzo wala kuwezeshwa kuliko hao wote juu.

Kwahiyo yanayofanyika ni Makosa, na endapo ukiwa na ushahidi madhubuti unaweza kuripoti Takukuru na akashtakiwa.

Lakini tambua mazingira yao halisi ya utendaji Kazi wao na mfumo uliopo nchini.
 
Mleta mada we ni fisi Maji!

Hiyo karatasi unayopewa na wino unadhani znatoka wapi?

Usipende vitu vya bure utakuja kubafilishwa jina
 
Back
Top Bottom