Habari zenu wakuu
Nimerudi tena kuomba ushaurii tena juu ya hatima ya mahusiano yangu
Kwanza mtanisamehe mwanzo sikuwaweka wazi kuhusu kurudiana kwangu mimi na Salim
Ukweli nimekuja kuomba ushaurii ikiwa tayari nilishaingia kwenye mahusiano na Salim….
Labda niwaelezee kwa kifupi kabla ya Salim hajatokea kwenye maisha yangu nilishakuwa na mahusiano na kijana mmoja ambae ndo alinizuzua nikashindwa kumkubali Salim kipindi kile ananitongoza
Sasa tulikuwa tunapendana tu na huyo kijana ila baadae tukashindwana tukaachana… hata mwezi haukuisha nikaja kuwa na kijana mwinginee nae tulidumu kama miaka miwili hivi tumekuja kuachana mwaka huu mwanzoni nililetaga kisa humu ila kilikuwa open sana nikawaza mwenyewe anaweza kujijua ukizingatia ni mtu wa social media nikaomba moderate waufute ule uzi so hamtoweza kuufufua
Huyu kijana wa pili niliekuwa nae ndani ya mahusiano yetu nilijikuta nakuwa na kijana mwinginee kwaiyo nikawa nina wa double wote wawili na kwakuwa tulikuwa mikoa tofauti haijanipa shida wala hawajawai kushtukiaa
Najua unajiuliza why nilikuwa na wanaume wawili kwa wakati mmoja
Tuwape majina Alex na frank
Alex ndo mwanaume wangu wa pili na Frank ni huyo alioingia katikati ya mahusiano yetu
Sababu ya mimi ku date na wote wawili ni kwakua tuligombaa na Alex na tukakaushiana miezi 3 Hakuna aliemtafuta mwenzie.. nakumbuka ulikuwa pasaka mwaka jana tuligombana hatukuambiana tuachane ila tulinyamaziana… haikupita hata mwezi tuseme tarehe 25/4/2021 ndio mwezi niliokutana na Frank.. kijana mcha Mungu mwenye misimamo yake mlokolee haswa basi tulizoeana tukajikuta tuna mahusiano na kusema kweli huyu ndo mwanaume ninae jisikia amani sana kwake
Frank sio mtu wa bata nikisema mlokolee namaanisha,,, ana pesa yaani kiufupi ni mtu mwenye maisha yake tatizo lake ni moja ana kama dharau za chini chini sasa sijui ndo ulokole ama jeuri ya pesa
Turudi huku
Niliendelea kuwa na Frank nikiamini Alex tumeshaachana na kweli hatukutafutana mpk mwezi wa 7 /2021 tena nilikuta Email yake akisema kwamba kapoteza namba yangu ndo maana yupo kimya et akatuma na namba yake mpya ni mcheki nayo
Niseme tu ukweli huyu Alex nilikuwa nampenda sana (nilikuwa ila sio kwa sasa) basi nilivomcheck ndio nilifufua mahusiano yangu na yeye tukajikuta tumeanza upya na mimi nikashindwa kumuacha kijana wa watu Frank kwasababu hakukua na sababu ya mimi kumuachA ukizingatia nilikuwa simuelewi Alex
Alex amenizidi miaka 7 ni mkubwa tu nilikuwa nampenda kwasababu ni mtu charming sana yaani hata Kama amekukosea namna anaongea na wewe unajikuta unamsamehe ila ni mwanaume mmoja tapeli na Muongo mno tulikuja kuachana kwasababu ya utapeli wake hiyo ilikuwa ni mwezi wa 1/2022 ndio nimeachana na Alex nikabaki na Frank
Sasa Frank shida ilianza mwaka jana mwezi wa 12 alipofiwa na mama yake basi alibadilika mno yaani akawa tena hana muda na mimi hivo yeye na kanisa kanisa na yeye
Mara anataka kuwa mchungaji yaani mambo yakawa mengi tukaenda hivo hivo mpk mwezi wa 2 nikaona yananishinda mahusiano hakuna kuitana hata Love, mpnz na majina mengine ya romantic nikamkaushia akituma sms sijibu akipiga sipokei yaani hivo nikauchuna mwezi mzima baadae akawa kunitafuta akasema yeye ameona amtumikie Mungu kwanza asiyape mahusiano kipaumbele sijui tumuombe Mungu kama tumeandikiwa kuwa wote tutakuwa mimi sikujibu hata hiyo sms nikamkaushia
Sasa mwezi wa 3 wakati nimekaa zangu sina hata mahusiano nimeboreka hata wakuniliwaza Sina ndipo simu yangu kuita kuangalia namba ngeni nikawaza nani huyu na mimi huwa sipokei namba ngeni siku hiyo nikaona bora nipokee
Kupokea nikasikia sauti ya Salim moyo ukadunda maana sikutegemea… ila nikajifanya simjui akijielezea baadae tukaelewana salamu kibao na kutumiana mapicha maana hatukuonana muda mrefu
Mwezi wa 3 mwishoni tukajikuta tumeanza mahusiano upya penzi limenogaa hivi mpk saivi napoongea tupo na huba zito
Kusema ukweli sijui kama nampenda ama ni vile naogopa kuwa mpweke
Ndani ya hiyo miezi tumeshaonana mara nyingi sana ananitumia nauli na mimi nakwea pipa mpk alipo
Mpk sasa hatujawahi fanya chochote na Salim zaidi ya Kukiss tu na kukumbatiana ila nataka nimpe tunda sema naogopa tunda langu bado bichi nilikuwa namtunzia baba mchungaji wangu Frank sasa na yeye ndio kama hivo haelewekii
Week ilopita Frank kanitafuta kuniuliza naendaa lini Dar ili tuonane maaana hatujaonana tangu mwaka jana nikamwambia mimi najua tumeshaachana so hasaau kuhusu kuniona,,, kaniuliza yeye lini alinambia ameniacha hajawahi niacha sema amejipa muda wa kujitafakari nikamwambia aendelee kujitafakari mimi najua tumeachana)
Kilichonileta humu ni mnipe tena ushaurii
Nibaki na Salim ambae anataka kunioa mke mdogo
Ama niendelee kumsubiri Frank wangu ambae haelewiki anataka nini
Note
Kuanzia mwanaume wa kwanza mpk Salim Hakuna niliewai kukulana nae ni yale mahusiano ya mbali so tunaishia kuchart na hata wakiniomba tunda nawachenga
Katika hao wa 4 Salim ndio amebahatika kunikiss tu nafikiria nimpe na mbususa ila namuwaza baba mchungaji wangu atarudi kweli mimi na yeye tuna maagano yetu tukasema tunasubiri wakati wa Bwana shida Iliopo ni kwamba simuelewi Kama ananipenda ama anajaribu kucheza na akili yangu… yaani hanipi ushirikiano ambao utanionesha kwamba bado tupo pamoja sijui nielezeeje hapa
Miaka yangu ni juu ya 24 chini ya 28[emoji45][emoji45]