Je, niolewe naye? Baba yake alizaa na Mama yangu

Big up mamaa, naamini mwisho wa siku utajua usimamie wapi, mimi hapa nimechemsha kabisa, inanikumbusha hesabu za mlinganyo enzi zile primary. Ukichuja ushauri uchanganye na zako uje utupe jibu hapahapa kwamba umeamua nini, all da best

Umeona eeeh, lakini naanza kupata Mwanga kutokana na ushauri ninaopata.
 
Nimekusoma, ila ingekuwa vema kama ungeandika 'katika harusi ya Binti mwingine wa baba yake A (yaani B) ambaye alizaa na Mwanamke mwingine tena'...

Noted. Ila bado hujatoa ushauri wako katika mada husika.
 

Duh! Hili darasa zuri sana. Nilikuwa na wasiwasi kidini. Ila naona hiyo Genesis 28: 2 Jacobo Mtoto wa Isaack alienda kumwoa binti ya Kaka ya Mama yake (Binti ya Mjomba) au Binamu. Haaaaa haaaa hapo poa, Binamu nyama ya hamu.

Swali langu ni je, agano la kale na jipya mapokeo yake ni sawa katika hilo? Je restrictions katika kitabu cha Walawi nadhani haina mgogoro?
 

Asante Mkuu. Nimekusoma.
 
Akati mnaanza kupigana sound kwanini hamkujiuliza hayo maswali kwanza?
Acha unafiki we binti.
Ningekua nakujua ningekucharaza mboko kwanza!

Acha noma Pillu, wakati tunaanza nini? Soma post uielewe Mkuu.

Ndo tunaanza sasa ndo maana nauliza yote haya.
 
Big up mamaa, naamini mwisho wa siku utajua usimamie wapi, mimi hapa nimechemsha kabisa, inanikumbusha hesabu za mlinganyo enzi zile primary. Ukichuja ushauri uchanganye na zako uje utupe jibu hapahapa kwamba umeamua nini, all da best

Poa Mkuu wangu, sasa hivi kama asilimia 50% ya homework nimemaliza. Nitarudi kuwajuza.
 


mgogoro unaotokea katika ndoa za ndugu, ni pale panapokuwa na genetics conflict. we all inherit genetics from our fathers, in this case marriage btn two who relating from some father, will have this conflict.
 
mgogoro unaotokea katika ndoa za ndugu, ni pale panapokuwa na genetics conflict. we all inherit genetics from our fathers, in this case marriage btn two who relating from some father, will have this conflict.

Nimekusoma best. Sasa inabidi wewe uwepo kama kutakuwa na vikao vigumu haaaaaa haaaa (joke!).

Sasa hawa wadau waliokuwa na maoni tofauti na yako mbona wamekomaa tu kuwa ni Laana, Kaka yako, haikubaliki, kidini noma, kijamii kitanuka, nk. nk. Au hawana hoja zenye upako?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…