Je, nitumie dili niliyopewa ukweni hata kama wife ananitambia?

Itakuwa hata hela ya mboga inatoka ukweni. We golikipa endelea kudaka mipira kutoka kwa wakwe, unataka kumsusia nani wakati wenyewe washaamua kukupa matonge uendelee kutoa ushuzi
 
We tumia hyo fursa utoke kimaisha,hacha umaskini jeuri.Cku hz hata ndugu yako akikusaidia atabrag tu,so mkeo kusema wamekusaidia inakuuma nn wakati ni kweli wamekusaidia.
Ajifunze Akina Mwijaku, Kitenge,Baba levo ,Doto Magari..wakiongea Ila pesa inaingia Haina shida...ndio Dunia YA sasa
 
Nenda kasome mkuu,itakuja kujusaidia badae,halafu chukulia tu kuwa ni madhaifu ya mke wako
 
Kaka achana na Maneno, Pga kaz tu. Turkey ww nenda
 
Sasa hapa karibuni kuna fursa ya kwenda kusoma Uturuki chuo fulani ambacho wanakufund na unalipwa ukienda kusoma, na hiyo fursa imetoka ukweni.

Je, niikubali hii fursa wakuu ama niikatae kutokana na wife na kujigamba kwamba wananisaidia sana?
Wacha ujinga baba kwani hiyo elimu ukishaipata watafaidika wao au wewe mwenyewe? Hiyo itabaki kwako mpaka uondoke duniani.

Tena wewe umepata wakwe wema kweli lakini bado malalamiko. Zungumza na mkeo ikiwa hawezi kunyamaza basi wewe endelea na shughuli zako.

Lakini nakushauri hata siku moja usiiwache hiyo nafasi ya kwenda masomoni, tena kwa kulipiwa, hapo ndiyo mwanzo wa kujikomboa kijana.
 
Asante sana mkuu kwa ushauri mwema
 
Nchi tu inapewa msaada na wafadhili na mabango kibao , mfano, kwa ufadhili wa watu wa marekani. Hakuna mtu yoyote hapa duniani ambaye hajasaidiwa kitu na mtu.
Tumia fursa hiyo, ila mwambie mkeo aache umbea.
 
Kubali fedheha baada ya muda tembea mbele hapo hamna mke kama backup ndogo ndogo kama hzo anazipigia kelele kwenye makubwa itakuaje
 
Hizo ni miradi huyo manzi sababu zinatoka kwa baba yake,
Jiandae kuolewa soon utakuwa chini ya milki ya huyo kimbelembe wako,
Huna mke umepigwa
 
Nchi tu inapewa msaada na wafadhili na mabango kibao , mfano, kwa ufadhili wa watu wa marekani. Hakuna mtu yoyote hapa duniani ambaye hajasaidiwa kitu na mtu.
Tumia fursa hiyo, ila mwambie mkeo aache umbea.
Mkuu nimekuelewa kwa vizuri hasa .
Uamuzi wangu niliochukua ni kesmba.
FURSA HII SITOIWACHA NA WIFE NITAMUAMBIA AACHE UMBEA WAKE WA KUSEMASEMA HUKO NJE.
MAAMUZI YANGU NDIO HAYO.
 
Ufungue biashara kariakoo halafu uende Uturuki ukasome!!! Kidogo ni ngumu, labda uchague kimoja. Fusa usiache.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…