Je, nyumba bado ni asset ya uhakika kuliko asset zingine zote?

Je, nyumba bado ni asset ya uhakika kuliko asset zingine zote?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Baada ya tetemeko kuikumba mikoa kadhaa ya kanda ziwa,nimeanza kujiuliza kama kumilki nyumba bado ni asset ya kuaminika kama tulivyozoea.

Ni kawaida kusikia mtu anasema ukitaka kuwekeza na hela yako isipotee kirahisi,wekeza katika majengo na wala si vyombo vya moto au kitu kingine chochote.

Sometimes ni bora hata chombo cha moto unaweza kukikarabati kwa gharama ndogo na kikatengamaa kuliko hekalu lililoporomoka kutokana na tetemeko.

Baada ya tukio hili la tetemeko, nimeamini asset ni ile tu iliyowekewa bima na hata kama una jumba lako lakini halina bima, basi ujue unajidanganya tu maana moto nao hauwezi kukuacha salama.

Nasema hivi kwasababu naamini inawezekana zaidi ya asilimia 97 ya nyumba zilizobomoka hazikuwa na bima yoyote ikiwemo bima ya moto na wengi wao waliamini wameshajikomboa kimaisha kwa kumiliki nyumba bila kujali ni ya ukubwa gani ili mradi tu ana nyumba.

Tukio hili liwe funzo kwa watu kuwekea bima mali zao zikiwemo nyumba zao.
===========

Maoni ya WanaJF kuhusu mjadala huu yamesomwa pia kwenye kipindi cha JAMII LEO
 
Ili uiite nyumba yako ni asset lazima ujiulize inakuzalishia kitu gani kwa mwaka na thamani yake ya kuiuza kwa haraka ni kiasi gani kulingana na gharama za kuipata hiyo nyumba.

Kwa hiyo swali la msingi tu, ni kwamba watu wengi wamepigwa upofu na kuamini kwamba nyumba ni asset akati sio hivo.

Kuna vitu ni quality asset kuliko nyumba
 
Kuna maafa mengine kama tetemeko,mafuriko na majanga yanayosababiswa na ''act of God''...bima hazikingi.
Kama ndio hivyo basi ni shida na sababu huenda ni kutokana na ukweli kuwa majanga ya asili huharibu vitu vingi kwa mara moja kiasi kwamba si rahisi kwa kampuni za bima kufidia watu wote na kwa wakati mmoja.
 
Bado ni asset....zikikumbwa na majanga makubwa kama hayo...jamii kwa ujumla inasaidia kurebuld....lakin pia jiulize haya majanga yanatokea mara ngap katika kipindi cha uhai wako?!
Wewe hata bima ya moto umeweka kama unamiliki nyumba?
 
Kama ndio hivyo basi ni shida na sababu huenda ni kutokana na ukweli kuwa majanga ya asili huharibu vitu vingi kwa mara moja kiasi kwamba si rahisi kwa kampuni za bima kufidia watu wote na kwa wakati mmoja.
Hakika ndio maana bima kwa mashirika ya ndege; kampuni ya bima nayo hukata bima kwenye kampuni kubwa zaidi...reinsurance...ndio maana hata bima kwenye kilimo inakuwa ngumu kwani ikitokea ukame kampuni ya bima inaweza kufilisika kwa kulipa fidia.
 
Bado itabaki kuwa asset muhimu sana. Kwanza unafanya savings masuala ya pango.
Kikubwa ambacho watanzania tu waoga kukitumia ni kukopea bank. Ni collateral ya kuaminika sana.
Tatizo tukisha kopa tunaishia kuongeza wake au nyumba ndogo na kujenga heshima Bar!
Ngumu sana kulifanya gari kuwa collateral hasa hii mitumba tunayo nunua
 
Sure...nyumba unajenga milion 80....kisha unapangisha laki mbili kwa mwez...kwa mwaka milion 2.4, kuirudisha hiyo 80milion yataka miaka kedekede kama miaka 33 hivi...na hapo hiyo ni mtaji uliowekeza sio faida.....na hapo bado unahitaji ukarabati...inakuwa imezeeka....pili hiyo hela haiwez kukaa tu hapo had kufika 80m....so mm binafsi huwa siamin kuchukua hela yako yote na kujenga nyumba eti asset....80milion unaweza fanya biashara kubwa na ukapata faida two times ndani ya miaka 2.
Otherwise kuwa na nyumba ya kuishi ni muhimu bt not kama ideology ilivyo kwa wabongo wengi kwamba ukiwa na nyumba ww ni tajiri..
 
Wewe hata bima ya moto umeweka kama unamiliki nyumba?
Nimeweka ful package yaan hata weww ukidhurika kwa tukio lilitokea kwangu bima inakufidia.

Gharama ya bima si ghali kiivo..mfano hyo full package kwa nyumba ya mil 90...nililipa kama lak na 28 elf kwa mwaka jana...mwaka huu pamoja na vat itaongezeka kidogo...ingawa sidhan kama itavuka lak unusu.
 
Sure...nyumba unajenga milion 80....kisha unapangisha laki mbili kwa mwez...kwa mwaka milion 2.4, kuirudisha hiyo 80milion yataka miaka kedekede kama miaka 33 hivi...na hapo hiyo ni mtaji uliowekeza sio faida.....na hapo bado unahitaji ukarabati...inakuwa imezeeka....pili hiyo hela haiwez kukaa tu hapo had kufika 80m....so mm binafsi huwa siamin kuchukua hela yako yote na kujenga nyumba eti asset....80milion unaweza fanya biashara kubwa na ukapata faida two times ndani ya miaka 2.
Otherwise kuwa na nyumba ya kuishi ni muhimu bt not kama ideology ilivyo kwa wabongo wengi kwamba ukiwa na nyumba ww ni tajiri..

Nyumba gani hiyo milion 80 unapangisha laki 2[emoji23][emoji23][emoji23] ?! Kijitonyma tu chumba laki Choo cha ku share...labda Iyo nyumba iko madongo poromoka.... Nyumba ya milion 80 ukipangisha chini laki 7 or milion
 
Sure...nyumba unajenga milion 80....kisha unapangisha laki mbili kwa mwez...kwa mwaka milion 2.4, kuirudisha hiyo 80milion yataka miaka kedekede kama miaka 33 hivi...na hapo hiyo ni mtaji uliowekeza sio faida.....na hapo bado unahitaji ukarabati...inakuwa imezeeka....pili hiyo hela haiwez kukaa tu hapo had kufika 80m....so mm binafsi huwa siamin kuchukua hela yako yote na kujenga nyumba eti asset....80milion unaweza fanya biashara kubwa na ukapata faida two times ndani ya miaka 2.
Otherwise kuwa na nyumba ya kuishi ni muhimu bt not kama ideology ilivyo kwa wabongo wengi kwamba ukiwa na nyumba ww ni tajiri..
Umesema sahihi kabsa....but hujawatendea haki watu wasiokuwa na skills za busness...yaan wapo watu hata ummpe business iliyosimama kama kampuni ya cocacola...baada ya muda atafilisika.

My take ni kwamba kama mtu ana access ya pesa lakin hana busn skill bora kuwekeza katika majumba...ni bora kwao...
 
Nyumba gani hiyo milion 80 unapangisha laki 2[emoji23][emoji23][emoji23] ?! Kijitonyma tu chumba laki Choo cha ku share...labda Iyo nyumba iko madongo poromoka.... Nyumba ya milion 80 ukipangisha chini laki 7 or milion
Hujui ukiongeacho kaka...hakuna hizo garama otherwise unamezeshwa......hata kama ni majohe as long ujenzi umegarim 80m inakupaswa kuliwazia
 
Hujui ukiongeacho kaka...hakuna hizo garama otherwise unamezeshwa......hata kama ni majohe as long ujenzi umegarim 80m inakupaswa kuliwazia

Sijamezeshwa nasema ninachokijua nina nyumba mikocheni na makumbusho karibu na kituo...
 
Nyumba bado ni asset kubwa na muhimu kuliko assets nyingine zote.
Mkuu kweli ni asset lakini pasipo bima, ni kujidanganya tu.

Leo hii hakuna mabenki yaliyokuwa yanayotegemea nyumba zilizowekwa kama dhamana ya mikopo huko Bukoba na sasa hayaamini kilichotokea?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Sijamezeshwa nasema ninachokijua nina nyumba mikocheni na makumbusho karibu na kituo...
Hongera kujenga maeneo hayo.....bt kuna majumba ya maana kitunda, tandika...mbagala na hata mkuranga ndani ndani vichochoroni....all in all kila mtu abaki na iman yake mkuu.
 
Back
Top Bottom