Je, online betting inaweza kuwa chanzo cha kipato?

Je, online betting inaweza kuwa chanzo cha kipato?

Maneno mengi ambayo ni pumba tupu mimi nimewashuhudia wengi tu waliopiga pesa hii Jackpot ya juzi kuna washkaji hapa kitaa wameshinda mechi 11 wakapata laki 7 na waliweka buku tu
Hii ndio inadhihirisha ni vipi Hesabu zinakupiga chenga..., Wengi ni wangapi ? Unajua ni wangapi wanacheza na wangapi mpaka leo wameshashinda ile top prize ?

Unajua inaweza ikawa rahisi kwa wewe kupigwa na radi mara mbili kuliko kushinda Jackpot top prize hao washikaji zako kitaa walishacheza mara ngapi na wameshinda mara ngapi na una washikaji wangapi ambao huenda wakacheza maisha yao yote na wasipate ? Unajua kwanini yule Mkenya aliyeshinda top prize alitangazwa kila Kona ? (ili wewe uone kwamba ni rahisi)

Kama kuna zawadi moja wakacheza watu trillioni moja akapata mmoja haimaanishi kwamba hakuna anayepata ila uwezekano wa huyo mmoja kuwa wewe ndio hapo tunapoongelea the odds being stack against you; By the way sidhani kama hao washikaji wako wanatumia jackpot kama njia ya kipato chao
 
Niliwahi kumshuhudia mshkaji fainali ya uefa kati ya Chelsea na Manchester city jamaa akaweka laki 5 akampa chelsea akaipiga laki 8 faida
Vipi unajua ni Laki ngapi alishaweka na kupoteza au milioni ngapi ? Au haujawahi kushuhudia watu wanapoteza mamilioni ?
 
Vipi unajua ni Laki ngapi alishaweka na kupoteza au milioni ngapi ? Au haujawahi kushuhudia watu wanapoteza mamilioni ?
Hebu nikuambie kitu kimoja kuhusu huo mfanano unaouweka wewe kuhusu kupoteza betting,mimi nimeshashuhudia watu wengi wanawekeza kwenye kilimo kwa mitaji mirefu na mwisho wanaangukia pua
 
Hii ndio inadhihirisha ni vipi Hesabu zinakupiga chenga..., Wengi ni wangapi ? Unajua ni wangapi wanacheza na wangapi mpaka leo wameshashinda ile top prize ?

Unajua inaweza ikawa rahisi kwa wewe kupigwa na radi mara mbili kuliko kushinda Jackpot top prize hao washikaji zako kitaa walishacheza mara ngapi na wameshinda mara ngapi na una washikaji wangapi ambao huenda wakacheza maisha yao yote na wasipate ? Unajua kwanini yule Mkenya aliyeshinda top prize alitangazwa kila Kona ? (ili wewe uone kwamba ni rahisi)

Kama kuna zawadi moja wakacheza watu trillioni moja akapata mmoja haimaanishi kwamba hakuna anayepata ila uwezekano wa huyo mmoja kuwa wewe ndio hapo tunapoongelea the odds being stack against you; By the way sidhani kama hao washikaji wako wanatumia jackpot kama njia ya kipato chao
Watu wanashinda bonus kibao, kwa mazingira ambayo mimi nipo vijana wanapasua vizuri tu japo sio kila siku laiti ingekuwa hawampigi muhindi wasingekuwa wanacheza
 
Hebu nikuambie kitu kimoja kuhusu huo mfanano unaouweka wewe kuhusu kupoteza betting,mimi nimeshashuhudia watu wengi wanawekeza kwenye kilimo kwa mitaji mirefu na mwisho wanaangukia pua
Ngoja twende polepole; kuwekeza kwenye kilimo huku ukitegemea mvua ambayo haitabiliki sehemu ambazo ukame ni kawaida nadhani haina tofauti na betting; ila kuwekeza kwenye kilimo sehemu ambayo hakuna ukame; na kuna uwezo wa kumwagilizia na una uhakika wa soko hio sio betting...

Tukija kwenye odds ukipanda mchicha odds za kuvuna bangi ni non existent..., ingawa inaweza ikatokea sungura wakaja wakala mchicha wako au aliyekuuzia mbegu alikuuzia mbovu ila odds za kuuziwa mbegu mbovu mara kumi ukipanda mara 100 ni ndogo sana unless unahitaji kubadilisha supplier...

Tukija kwenye odds za wewe kuweza kushinda Jackpot Main Prize ya Super sports ya kuchagua timu 17 (na sio wewe tu bali wewe na ukoo wako mzima) mnaweza mkacheza kwa generation 20 kila wiki na bado msipate kitu
 
Uliza kama anaendelea kubet?? Ndo utajua why mtu apatr faida ya laki 5 alafu aache[emoji1787][emoji1787]
Huwa anabet pale anapojisikia mfano leo hapa kitaa kuna mwamba kabeti kampa simba,lile,Dortmund na bochum akatia 20000 na mzigo umeingia tayari
 
Ngoja twende polepole; kuwekeza kwenye kilimo huku ukitegemea mvua ambayo haitabiliki sehemu ambazo ukame ni kawaida nadhani haina tofauti na betting; ila kuwekeza kwenye kilimo sehemu ambayo hakuna ukame; na kuna uwezo wa kumwagilizia na una uhakika wa soko hio sio betting...

Tukija kwenye odds ukipanda mchicha odds za kuvuna bangi ni non existent..., ingawa inaweza ikatokea sungura wakaja wakala mchicha wako au aliyekuuzia mbegu alikuuzia mbovu ila odds za kuuziwa mbegu mbovu mara kumi ukipanda mara 100 ni ndogo sana unless unahitaji kubadilisha supplier...

Tukija kwenye odds za wewe kuweza kushinda Jackpot Main Prize ya Super sports ya kuchagua timu 17 (na sio wewe tu bali wewe na ukoo wako mzima) mnaweza mkacheza kwa generation 20 kila wiki na bado msipate kitu
Sasa hichohicho kilimo cha kutegemea mvua sehemu hizohizo zenye ukame watu wanapiga pesa na maisha yanaendelea safi tu,mimi niko mikoa ya kusini na hakuna sehemu yenye shida ya mvua kama wilaya ya masasi ila japo kuna hizo changamoto ila watu wanafanikiwa tu hivyohivyo
 
Watanzania siku hizi ni kama wamechanganyikiwa sana; sijui ni sababu ya umaskini au vipi. Wanatumia raslimali nyingi sana kwa kucheza kamali wakitegemea kupata hela ya haraka haraka na kuishia kuwa maskini zaidi. Ndiyo maana makampuni ya kamali yamekuwa lukuki, na wamiliki wa makampuni hayo wametajiriaka sana.
Acha watu wabet lolote laweza kutolea Ila betting ukiamua kwa siku haukosi elfu 50
 
Nimepitia Hii Trending kwa uchache
Nikutulia siku moja nitaeleza uhalisia wa betting.
Kwa uchache tu...Kuna Useen power behind this company...unseen force.
Inatumia tamaa ya Binadamu maana always Binadamu anataa...hivyo hapo Kuna mwanya wa kwanza.
Kuna nguvu isiyo onekana nyuma ya hizi kampuni Kuna mikataba msiyo ijua Nyinyi.
Sasa Kuna stage1- 5 mpaka 6 za ulimwengu wa betting.
Stage 1 una bet unaliwa unaacha..
Hapa umeshawishiwa au umejishawishi mwenyewe...kwa nguvu usiyo iju ww.
Stage 2 unabet unaliwa unaacha Kisha unarudi Tena Baada ya maumivu ya kuliwa kuisha...unarudi Tena kuja kukomboa pesa zako.
Ulkipata pesa unarudi..na matumaini ya kushida unasahau kilicho chenga Hizo mechi bado kipo unarudi Tena kuja kushinda....sio Kama unavyowaza.
Stage 3 una bet unaliwa , unaliwa, unaliwa Tena na Tena ,na Tena ukija kupata unakuwa chambo ya kuleta wengne kwenye mchezo.
Huyu mtu kuacha Ni Hadi Maombi kasha wekwa kwenye mtungi wa kubet tu.
Stage 4 huyu pesa anayopata karibu Yote Anavutiwa kubet tu huyu Ni mtumwa Hawezi Toka Tena Ni lango la kupitisha pesa kwenda kwenye hizi kampuni! Ukishinda ww Ni member wao wamekuzawadia ili kuleta wafuasi wengi.
Stage 5. Official member/Mimiliki ..huyu ni member wa betting ' ni wahusika wa hizi kampuni wenyewe tayari yuko kwenye mkataba akikenguka tu kampuni yake inapigwa hasara na Hawezi acha hiyo biashara.
Stage 6. Kampuni kwa kampuni hizi kampuni waendesheji Kuna saa wanaviziana kwa Kuangaliana yaani
Kampuni A wanachunguza weakness za kampuni B.
Kisha A anaweka mzigo wa maana kupitia watendaji wake.
Hii kimjini inaitwa mbwa kala mbwa.
Sasa kampuni iliyo weak utakuta anachukua pea zenu, anachukua pesa za wanao bet. inaenda kulipa kampuni iliyo na nguvu zaidi.
....Haya Huwezi kuyaelewa kirahisi...Ni spiritual.
Tafuta Msaada wa Maombi ukiwa kwenye Stage 2 , au 3 Tena kuazia hiyo 3 ndio mbaya zaidi maana kila pesa lazima utoe fungu la kumi kwa wakuu wanao simamia bettingDarkpower.
Kuna mengi Sana Ila kwa Leo nishie Hapa.
Tafadhali rudi ufafanue zaidi ikibidi anzishia uzi kabisa usaidie taifa

Najua wapo wabishi ila wapo utakaowaokoa.
 
Si kupoteza tu, na kupata pia. Hapa unasema tu itatokea penati katika mechi. Isipotokea unapoteza afu tano yako, ikitokea unapata afu ishirini na tano. Hiyo afu ishirini na tano, tano nazirudisha pembeni, ishirini zinatumika kwenye mikeka mingine, tunaita kumkaanga papa kwa mafuta yake, yaani natumia faida iliyopatikana kutafutia faida nyingine

View attachment 2547541
Mkuu, kampuni gani hii
 
Back
Top Bottom