Je! Pesa za Mshindi wa BBA Idris zinapaswa kukatwa kodi?

Andrew123

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2012
Posts
8,358
Reaction score
10,976
Wataalamu wa masuala ya kodi na sheria hebu tujuzeni kama pesa za mshindi wa BBA season 9 Idris Sultan zinapaswa kutozwa kodi kwa mujibu wa sheria zilizopo Hapa nchini. Nauliza kwa sababu nataka kujifunza.
 
Kwa uelewa wangu mdogo nadhani hapana. Ila kule azipatapo atakatwa kodi (Afrika ya kusini). Ngoja tusubiri weledi wa haya mambo.
 
Haziwezi kukatwa Kodi.
Kumbuka kipindi kile wakwati wa sakata ushiriki wa Big brother kwa Tanzania na maadili ya mle,
Kama unakumbuka vizuri,kundi la kina Lotus,walikuwa wanafanya ufuska mle,na yule mwenzie,pia mwisho,na Richard,na clips zote za mambo ya ngono yamo kwenye yupu tube na hata ukitafuta zinakuja.
Hii ni kuashiria hado wanakuwa wazee,basi uchafu wao utakuwemo mle,na dunia nzima kwa ujumla,hadi wanaingia kaburini basi laana ile bado inawafikia hukohuko maana kizazi kimechobakia kinabakia na uchafu badala na kumbukumbu nzuri.Na sipati picha kwamba na wao wanakuja kuwa na watoto,na hao watoto lazima waathirike kisaikolojia,maana hata wakiwa shuleni wenzao watakuwa wanachokoza na kuwaonyesha clips za baba zao au mama zao.Ni Mbaya sana

Sasa kuna kipindi waziri alifafanua kwamba hawawezi kuzuia mtanzania kushiriki Big brother maana hawana mamlaka ya kumzuia kwakuwa ni nje ya nchi na kibali hakitolewi Tanzania.
Licha ya kwamba Office za Multi choice zipo Tanzania,sasa kwa maana hiyo hata hizo pesa serikali wawe wapole,maana haziwahusupia
 

Mkuu acha siasa hoja ni kuwa ni taxable income au vipi? me nadhan inategemea source na sheria ya huko south inakolipiwa yan kama south sheria zao za kodi ya mapato inajumuisha pia fedha zinazopatikana kama prize then BBA ata withhold kiasi cha kodi kabla hawajamlipa, swala la vizazi na vitaona uchafu wa video itategemea na degree of exposure ya vijana wa wakat huo, mbona wakina Rambo walikuwa wanacheza movie wakati mwingine zina x scene hatusikii watoto wao wakilalamika cku izi?
 
amefanya kazi nje ya tz amelipwa pesa nje ya tz kodi ya tra inahusikaje hapo? inamaana nikifanya kazi ujapan nikalipwa hukohuko ujapan, natakiwa nilipe kodi ya tra tz au ya tra ya ujapani??!! kama nikulipa kodi basi niya south africa ndio anatakiwa alipe sio ya tz.

yani kodi kibao za kampuni zinazofanya kazi humu ndani ya tz na kupata mapato yake huku tz, mnazisamehe kodi na wengine wanakwepa kama sinema ya escrow mnatolea macho kodi ya BBA ambayo ni mapato ya nje ya tz! punguani nyinyi!!
 
Nauliza maana kuna wakati nilisafiri kwenda Canada nikatakiwa kudeclare amount niliyobeba ikiwa imezidi Dola 10,000, nikajuliza sababu hasa ni nini? Je hawatataka kunichanja kodi?
 
Kna watu walisema swala big brother ni la kishetani ila sasa hivi mnaanza kuzungumuza mara pesa kukatwa.
 
Nauliza maana kuna wakati nilisafiri kwenda Canada nikatakiwa kudeclare amount niliyobeba ikiwa imezidi Dola 10,000, nikajuliza sababu hasa ni nini? Je hawatataka kunichanja kodi?
Sio kwa sababu ya kodi, ni kuzuia money laundering, drug money na terrorist financing.
 
KODI ni kama PAI. Any income earned by residents either abroad or within the country is Taxable. To avoid Double taxation carefuully consideration of the differences in tax rates in two countries will apply. Pia kuna KODI ya KURUDISHA HELA NYUMBANI (Parent country of a firm or an Individual).
 

too long to understand..
 

nice maelezo mkuu..
 
Sio kwa sababu ya kodi, ni kuzuia money laundering, drug money na terrorist financing.


Asante wakuu nimejifunza kitu, ngoja niendelee kuperuzi comment
 
Mwache mwenzako ale mpunga wake kwa raha kuna watu kibao hawalipi kodi wameachwa we unakodolea za Idriss
 
Swali dogo tu, hizo hela atazitumia hukohuko SA?
 
Wataalamu wa masuala ya kodi na sheria hebu tujuzeni kama pesa za mshindi wa BBA season 9 Idris Sultan zinapaswa kutozwa kodi kwa mujibu wa sheria zilizopo Hapa nchini. Nauliza kwa sababu nataka kujifunza.


Kwanini ikatwe kodi wakati fedha haijazalishwa hapa nchini?
Unapaswa uulize Je, ni kwa nini Wanamuziki wanaokuja hapa na kulipwa mpaka Dola laki moja (100 000) na kuondoka mbona hawakatwi kodi? haya mambo ya fiesta watu wanavuna mabilioni lkn hakuna hata shilingi inakatwa kodi, sasa kwa nini fedha iliyopatika Afrika Kusini illipiwe kodi TZ? Itakatwa kodi huko AK lkn SIYO hapa Bongo!
Akina Diamond wanafanya show mlimani City kiingilio 50 000 watu wanajaa mpaka wanarudishwa na hakuna hata shilingi inayokatwa kodi, yote inaenda mifukoni mwa watu, hiyo ya BBA haina uhusiano wowote na TZ, kama unataka hayo mambo unafaa ukomae na akina Clouds media &Co. hawalipi hata ndururu!
 
Ndugu wachangiaji usicomment kwa kutumia personal judgement comment according to tax act
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…