Je, Rais Magufuli amevunja Katiba kwa kumteua Jaji Zepherine Nyalugenda Galeba kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa?

Je, Rais Magufuli amevunja Katiba kwa kumteua Jaji Zepherine Nyalugenda Galeba kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa?

Tunashukuru sana kama kaivunja maana ilikuwa mbovu sana.

Naomba kujua katiba mpya tutaanza kuandika lini?


Utavunjaaje nyumba yako mbovu wakati huna pesa wala mpango wa kujenga nyumba mpya??!!😒
 
Please look at my post number 66.

Nilishapitia hiyo point katika mjadala na kajekudya.

Saw your comment. I think the author brought that issue up in error. Contrary to what he thought and implied, the 15-year experience clock doesn’t start running only after one is appointed judge of the High Court of Tanzania!
 
Hata haki ya kufungua kesi sasa hivi Watanzania hatuna tena Mkuu,
The other Justices of Appeal shall be appointed by the President after consultation with the Chief Justice, from amongst persons who qualify to be appointed Judges of the High Court of the United Republic as provided for in Article 109 of this Constitution, or from amongst persons who qualify to be appointed Judges of the High Court of Zanzibar in accordance with the laws applicable in Zanzibar and have possessed such qualifications for a period of not less than fifteen years.


1. Consultation haikufanyika
2. 15 yrs hajatimiza


---
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapish Bw. Zepherine Nyalugenda Galeba Kuwa Jaji wa Mahakama ya Kuu . Hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam. Januari 29,2019



Kila kitu kimeandikwa humu, just read!
 
Hata haki ya kufungua kesi sasa hivi Watanzania hatuna tena Mkuu,


Alichosema ni sahihi isipokuwa kimetoka kwenye mhimili ambao sio sahihi.

Kimsingi, kuna taratibu za admission za mashauri, ambazo wasajiri wa mahakama wanapaswa kuzifuata, lakini wamekuwa hawazifuati. Kwa mfano, uamuzi mdogo (interlocutory ruling/order) ni uamuzi ambao haumalizi kesi ya msingi; hivyo, kisheria, haukatiwi rufaa, lakini bado unakuta msajiri amekubali kusajili rufaa kama hiyo. Ni aibu kwa mahakama kushindwa kujisimamia!
 
Sio tatizo lake ni letu Watanzania. Katiba yetu inampa Rais wa JYMTZ maamlaka makubwa kiasi kwamba anaweza kuwa mungu mtu. Kwa pamoja tumuombee amuue kwa hiari yake kuruhusu mchakato katiba ya wananchi.
Hii kali
 
Mkuu, kiutaratibu appointment inakamilika pale mhusika anakapokabidhiwa barua ya uteuzi na kusaini kukubali uteuzi huo. So, kwa kuwa process hiyo haijakamilika maana yake hakuna uteuzi uliofanyika na, kwa maana hiyo, Rais hajavunja Katiba.

Atashauriana na wahusika hapo baadaye kama Katiba inavyotaka na mhusika kuteuliwa rasmi kwa barua kukamilisha process. Ni mtazamo wangu tu lakini.
Utaratibu hata kama haujafika mwisho, kama hizi tararibu za mwanzo hazijafuatwa, ni kwamba katiba imevunjwa....
 
L'État, c'est moi - King Lous XIV

Uncle anaendesha nchi kifalme
 
Mkuu, kiutaratibu appointment inakamilika pale mhusika anakapokabidhiwa barua ya uteuzi na kusaini kukubali uteuzi huo. So, kwa kuwa process hiyo haijakamilika maana yake hakuna uteuzi uliofanyika na, kwa maana hiyo, Rais hajavunja Katiba.

Atashauriana na wahusika hapo baadaye kama Katiba inavyotaka na mhusika kuteuliwa rasmi kwa barua kukamilisha process. Ni mtazamo wangu tu lakini.
Am sure wale chawa wake watakuja kubeba majibu yako haya na kumpa mkulu ili ayatumie kama majibu akiwa public.
 
or from amongst persons who qualify to be appointed Judges of the High Court of Zanzibar in accordance with the laws applicable in Zanzibar and have possessed such qualifications for a period of not less than fifteen years.


Mimi ambae sijasoma sheria nimeelewa kwamba anaweza kumteua yeyote ambae amekua na vigezo vya kuwa Jaji wa mahakama kuu kwa miaka 15 ama zaidi.

Haisemi ambae amekua Jaji wa mahakama kuu kwa miaka 15 ama zaidi.

Labda utupatie hivyo vigezo vinavyotajwa ili tujue kama hiyo 2005 huyu jaji alikua navyo ama Lah.
 
Nani huyo aliyeROPOKA??!!
Amezoea kuteua na kutengua wateule wake kwa kuropoka jukwaani.

Anaidhalilisha mahakama na kuigeuza kuwa uwanja wake wa kisiasa wa kujidai.

Huwezi kumteua jaji kwa mihemko!! Kuna procedures za kikatiba.

Hata kama ana nia njema ya kukitangaza Kiswahili, angetafuta namna bora nyingine.

Mihemko haisaidii.
 
kwa kitendo cha kutamka mbele ya Jaji Mkuu ni wazi kabisa tayari amewasiliana naye(impliedly),yuko sawa kabisa.

kumbuka pia Rais anashauriwa tu na halazimishwi wala hapingwi kwa alicho kiona yeye ni sawa.

yuko sahihi kikatiba, hakuna katiba wala sheria yoyote iliyo vunjwa.
tusimuonee wivu mteule Jaji wa rufaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunashukuru sana kama kaivunja maana ilikuwa mbovu sana.

Naomba kujua katiba mpya tutaanza kuandika lini?
Katiba mpya sio issue,issue ni content zitakazikuwepo humo.....
hata mkulu nae unaweza kukuta anatamani katiba mpya....
 
Ukitaka maajabu njoo Tanzania na fuatilia kauli na teuzi za Rais. Huyo Jaji Zephania anajua kabisa kuwa lugha ya Mahakama Kuu ni Kiingereza. Kwa hiyo kitendo cha kuandika hukumu kwa Kiswahili alipaswa achukuliwe hatua.

Wasiojua kuandika na kuongea English wanapeana shavu. Kwa kuwa yeye Meko anaongea broken English anahalalisha udhaifu wake kwa kubariki makosa. Kimsingi huyo Jaji hakupaswa kuwa JAJI wa Mahakama Kuu, instead alipaswa kuwa Hakimu wa Mahakama za chini tu.
nisikilize vizuri hukumu ya kiswahili sio ya kwanza, na kwa mahakama kuu kitengo cha kazi hukumu inaweza kua ya kiswahili au kiingereza na zimeshaandikwa nyingi kadhaa miaka ya nyuma.Nilimshangaa Rais kusema kitendo cha kuandika hukumu ya kiswahili ni ushujaa wakati sheria inaruhusu, kifungu cha 4 cha the Labour Court Rules of 2007 kinasema lugha ya makahakama itakua bi-lingual kiswahili au kiingereza.Hivyo jaji hakufanya jambo jipya bali alitumia mamlaka aliyopewa kisheria.Angeweza kupewa tuzo ya kukuza kiswahili lakini si kuteuliwa kua jaji wa mahakama ya Rufani kwa kigezo tu cha kuandika hukumu kwa kiswahili,toka uhuru mahakama za mwanzo hazijawahi andika hukumu kwa kiingereza bali huandika kwa kiswahili.Inafurahisha mheshimiwa kila siku anasaini miswada na sheria kwa kiingereza sijawahi sikia akitaka iandikwe kwa kiswahili.
 
Back
Top Bottom